Sabi Sanda
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 409
- 31
Ni ukweli usipingika kuwa asilimia 100 ya uendeshaji vyuo vikuu vya Serikali inatokana na fedha toka Serikalini kuu. Kwa hali ilivyo sasa na huko tuendako hii ni hali ya hatari na inayofaa kufanyiwa kazi mapema ili katika kipindi cha miaka 10 mpaka 15 ijayo vyuo vyetu vikuu vya Serikali viwe na uwezo wa kujitegemea kwa angalau asilimia 60 kama sio 100.
Ili lengo hili litimie inapendekezwa vyuo vya Serikali vifanye yafuatayo
1. Vyuo vyote vikuu vya Serikali vianzishe Mifuko ya Akiba na Uwekezaji. Lengo liwe ni kwa kila Mwanachuo husika na aliyepitia katika chuo hicho awe anawekeza angalau shilingi 5,000 kila wiki katika Mfuko wa Akiba na Uwekezaji wa chuo chake.
2. Vyuo vyote vya Serikali viombe maeneo makubwa hapa nchini yaliyo na madini na gasi na kuyamiliki na kisha kuanzisha uchimba wake.
3. Vyuo vikuu vya Serikali vianzishe ukulima wa Mashamba Makubwa ya Miti ya Aina mbalimbali za Mbao. Lengo la chuo kimoja liwe ni kupanda angalau Ekari 150,000 za miti ya mbao kila mwaka kwa miaka 15 mfululizo. Iwapo uwekezaji huu katika mashamba makubwa ya miti ya mbao utafanyika, baada ya miaka 10 mpaka 12, kwa bei za sasa, chuo kikuu husika kitakuwa na ukakika wa kupata faida isiyopungua shilingi bilioni 3,900 kila mwaka kutoka katika mashamba yake ya miti ya mbao pekee. Kiwango hiki cha fedha kinaweza kuendesha Chuo kama Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa Zaidi ya Miaka 300 au Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 30.
Ili lengo hili litimie inapendekezwa vyuo vya Serikali vifanye yafuatayo
1. Vyuo vyote vikuu vya Serikali vianzishe Mifuko ya Akiba na Uwekezaji. Lengo liwe ni kwa kila Mwanachuo husika na aliyepitia katika chuo hicho awe anawekeza angalau shilingi 5,000 kila wiki katika Mfuko wa Akiba na Uwekezaji wa chuo chake.
2. Vyuo vyote vya Serikali viombe maeneo makubwa hapa nchini yaliyo na madini na gasi na kuyamiliki na kisha kuanzisha uchimba wake.
3. Vyuo vikuu vya Serikali vianzishe ukulima wa Mashamba Makubwa ya Miti ya Aina mbalimbali za Mbao. Lengo la chuo kimoja liwe ni kupanda angalau Ekari 150,000 za miti ya mbao kila mwaka kwa miaka 15 mfululizo. Iwapo uwekezaji huu katika mashamba makubwa ya miti ya mbao utafanyika, baada ya miaka 10 mpaka 12, kwa bei za sasa, chuo kikuu husika kitakuwa na ukakika wa kupata faida isiyopungua shilingi bilioni 3,900 kila mwaka kutoka katika mashamba yake ya miti ya mbao pekee. Kiwango hiki cha fedha kinaweza kuendesha Chuo kama Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa Zaidi ya Miaka 300 au Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 30.