Vyuo Vikuu Vya Serikali Badilikeni na Kufanya Yafuatayo

Sabi Sanda

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
409
31
Ni ukweli usipingika kuwa asilimia 100 ya uendeshaji vyuo vikuu vya Serikali inatokana na fedha toka Serikalini kuu. Kwa hali ilivyo sasa na huko tuendako hii ni hali ya hatari na inayofaa kufanyiwa kazi mapema ili katika kipindi cha miaka 10 mpaka 15 ijayo vyuo vyetu vikuu vya Serikali viwe na uwezo wa kujitegemea kwa angalau asilimia 60 kama sio 100.

Ili lengo hili litimie inapendekezwa vyuo vya Serikali vifanye yafuatayo

1. Vyuo vyote vikuu vya Serikali vianzishe Mifuko ya Akiba na Uwekezaji. Lengo liwe ni kwa kila Mwanachuo husika na aliyepitia katika chuo hicho awe anawekeza angalau shilingi 5,000 kila wiki katika Mfuko wa Akiba na Uwekezaji wa chuo chake.

2. Vyuo vyote vya Serikali viombe maeneo makubwa hapa nchini yaliyo na madini na gasi na kuyamiliki na kisha kuanzisha uchimba wake.

3. Vyuo vikuu vya Serikali vianzishe ukulima wa Mashamba Makubwa ya Miti ya Aina mbalimbali za Mbao. Lengo la chuo kimoja liwe ni kupanda angalau Ekari 150,000 za miti ya mbao kila mwaka kwa miaka 15 mfululizo. Iwapo uwekezaji huu katika mashamba makubwa ya miti ya mbao utafanyika, baada ya miaka 10 mpaka 12, kwa bei za sasa, chuo kikuu husika kitakuwa na ukakika wa kupata faida isiyopungua shilingi bilioni 3,900 kila mwaka kutoka katika mashamba yake ya miti ya mbao pekee. Kiwango hiki cha fedha kinaweza kuendesha Chuo kama Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa Zaidi ya Miaka 300 au Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 30.
 
Ni ukweli usipingika kuwa asilimia 100 ya uendeshaji vyuo vikuu vya Serikali inatokana na fedha toka Serikalini kuu. Kwa hali ilivyo sasa na huko tuendako hii ni hali ya hatari na inayofaa kufanyiwa kazi mapema ili katika kipindi cha miaka 10 mpaka 15 ijayo vyuo vyetu vikuu vya Serikali viwe na uwezo wa kujitegemea kwa angalau asilimia 60 kama sio 100.

Ili lengo hili litimie inapendekezwa vyuo vya Serikali vifanye yafuatayo

1. Vyuo vyote vikuu vya Serikali vianzishe Mifuko ya Akiba na Uwekezaji. Lengo liwe ni kwa kila Mwanachuo husika na aliyepitia katika chuo hicho awe anawekeza angalau shilingi 5,000 kila wiki katika Mfuko wa Akiba na Uwekezaji wa chuo chake.

2. Vyuo vyote vya Serikali viombe maeneo makubwa hapa nchini yaliyo na madini na gasi na kuyamiliki na kisha kuanzisha uchimba wake.

3. Vyuo vikuu vya Serikali vianzishe ukulima wa Mashamba Makubwa ya Miti ya Aina mbalimbali za Mbao. Lengo la chuo kimoja liwe ni kupanda angalau Ekari 150,000 za miti ya mbao kila mwaka kwa miaka 15 mfululizo. Iwapo uwekezaji huu katika mashamba makubwa ya miti ya mbao utafanyika, baada ya miaka 10 mpaka 12, kwa bei za sasa, chuo kikuu husika kitakuwa na ukakika wa kupata faida isiyopungua shilingi bilioni 3,900 kila mwaka kutoka katika mashamba yake ya miti ya mbao pekee. Kiwango hiki cha fedha kinaweza kuendesha Chuo kama Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa Zaidi ya Miaka 300 au Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 30.

wakifanya hivyo wajasiria mali watafanya kazi gani?
Nani atagundua maarifa mapya uzalishaji? Tunataka tuendelee kutumia vizuri rasli mali zetu kuzalisha kwa tija.
Hii ndio kazi yao.
Tunataka tuongozwe kwa kanuni bora, tutibiwe kwa njia sahihi na bora, tujenge nchi kwa mbinu bora zaidi.

Badala ya kuwatoa wasomi kwenye maabara na madarasani wakafanye hizo kazi, afadhali tuwachukue wamachinga woote tuwape hiyo ardhi na vitendea kazi wakapande miti na kuzalisha. Sio kuchuuza mali za wakwepa kodi.

Serikali nao wasimamie suala la nishati ya umeme ili wale jamaa wa mkaa wasiendelee kukata miti watakayopanda waungwana.
 
Mkuu si kweli kua public universities zote zinaitegemea serikali kwa 100%. Ingekua ivyo shughuli na majukumu yasingetimizwa kwa 100% na vyuo hivyo. Kwani pesa toka serikali ni ndogo sana na mara nyingi hutumika kwa kulipia mishahara.

Vyuo vikuu kama UDSM na SUA vina vyanzo vingine vya pesa hususani kutokana na shughuli za research and consultancy. Shughuli izi zinaviingizia vyuo mapato makubwa. Pia vyuo ivyo hupata pesa kutokana na grants na aids kutoka kwa wajomba (marafiki wa maendeleo).
 
Utekelezaji wake ni mgumu ssana, wengine hiyo pesa wanatumia siku tano
 
Aise hapo vitakua vyuo au makapuni ya biashara? Ni kama useme muhimbili ili kujitegemea wafungue shamba la mizabibu waanze kutengeneza wine
 
Aise hapo vitakua vyuo au makapuni ya biashara? Ni kama useme muhimbili ili kujitegemea wafungue shamba la mizabibu waanze kutengeneza wine

Wala simaanishi hivyo. Vyuo vyetu imefikia hatua vipunguze sana utegemezi toka Serikalini na kwa Wafadhili. Tunakokwenda si kuzuri hata kidogo. Ni muhimu sana Vyuo Vyetu na wahitimu wake wakatuongoza katika namna bora ya kutumia rasilimali za nchi yetu badala ya kuwaachia wageni toka nje.
 
Mkuu si kweli kua public universities zote zinaitegemea serikali kwa 100%. Ingekua ivyo shughuli na majukumu yasingetimizwa kwa 100% na vyuo hivyo. Kwani pesa toka serikali ni ndogo sana na mara nyingi hutumika kwa kulipia mishahara.

Vyuo vikuu kama UDSM na SUA vina vyanzo vingine vya pesa hususani kutokana na shughuli za research and consultancy. Shughuli izi zinaviingizia vyuo mapato makubwa. Pia vyuo ivyo hupata pesa kutokana na grants na aids kutoka kwa wajomba (marafiki wa maendeleo).

Sawa mkuu. Lakini ukweli unabaki palepale kuwa vyuo vyetu vikuu ni tegemezi mno. Naomba uangalie Facts and Figures za vyuo vyetu ndiyo utaona ukweli wa kile ninachokisema na umuhimu na mantiki ya mapendekezo niliyoyatoa.
 
Back
Top Bottom