Vyuo vikuu, mavazi na hadhi ya taifa

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Wakati huu ambapo vyuo vyetu vya elimu ya juu vimegubikwa na matatizo makubwa ya uongozi na sera mbovu za uchangiaji na ukopeshwaji kiasi wanafunzi hawapati nafasi ya kusoma kwa utulivu, MBUNGE wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM), amelalamikia kuwepo kwa mavazi yasiyo ya heshima kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na kuitaka serikali kuzuia hali hiyo.

“Mheshimiwa Spika, mavazi haya ya wanavyuo yanalishushia hadhi taifa letu hivyo ni vema serikali iweke sheria ya mavazi yanayotakiwa kutumiwa na Watanzania ili kuliongezea hadhi taifa,” alisema. Mh. Zambi haoni mambo lukuki muhimu yanayoishushia hadhi taifa letu bali nguo wanazovaa wanafunzi - na hili ameamua kulivalia njuga.

Mh. Zambi haoni habari ya FFU kuyazingira maeneo ya hivyo vyuo kama vile tuko kwenye uwanja wa mapambano kama inatudhalilisha mbele ya dunia - utafikiri tuko Gaza ?. Mh. Zambi, mbunge wa CCM, haoni kama tendo la watoto wetu kudahiliwa mbele ya mtutu wa bunduki linatudhalilisha mno kama taifa.

Mh. Zambi haoni sera duni za elimu ya juu zinavyofanya vyuo hivi kufungwa holela kwa visingizio visivyo na vichwa wala miguu kama vinatudhalilisha kama wazazi. Mh. Zambi haoni watoto wetu wanavyonyimwa fursa ya kupata elimu kwa sababu tu wazazi wao hawana uwezo kwenye karne hii ya 21 kama kitendo cha kulaaniwa ?

Hivi vyote Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM), havioni ila katumwa na wapiga kura wake kulalamikia nguo wanazovaa wanavyuo wetu. Hivi hao wapiga kura wake wameona wapi nguo zinazovaliwa kwenye vyuo vingine duniani ikilinganishwa na za wanetu. Je, hili linawaumiza kuliko hoja za maendeleo jimboni Mbozi ?

Kwa hakika namshangaa Mh. Zambi - kwa mtindo huu hatufiki.
 
“Mheshimiwa Spika, mavazi haya ya wanavyuo yanalishushia hadhi taifa letu hivyo ni vema serikali iweke sheria ya mavazi yanayotakiwa kutumiwa na Watanzania ili kuliongezea hadhi taifa,” alisema.

Dress codes hadi uni...
And you wonder why I just looove Tanzania!
Of course,tukivaa ''vizuri'' productivity inaongezeka.
Mbona watu wanakula tai na wanaibia taifa vilevile?
Hadhi ya taifa,my foot!Hivi anadhani wawekezaji pay heed to our dressing style?
And if that's the case,itabidi waheshimiwa wote bungeni waanze kuvaa bukta na khanga maana suti zao haziendani na ufanisi wao.
Hadhi?Radhi tupu!
 
........ha ha ha swala la dress code ni ngumu kidogo...


lakini naungana na Mbunge, ukweli sio swala la mavazi tuu kimsingi wasichana wa vyuo vikuu bongo wamechetuka au wamedata. Mara utasikia wanapiga picha za uchi --tunaona mtandaoni, mara mabibo hostel ni dangulo., nadhani maadili yamepungua au kasi ya ngono imeshika hatamu vyuo vikuu or utandawazi umekomaa.

..anyway nawaachia wenyewe waamue maana ukizama sana utakutana na maswala ya hki yakufanya lolote ila usivunje sheria. ..?..??
 
........ha ha ha swala la dress code ni ngumu kidogo...


lakini naungana na Mbunge, ukweli sio swala la mavazi tuu kimsingi wasichana wa vyuo vikuu bongo wamechetuka au wamedata. Mara utasikia wanapiga picha za uchi --tunaona mtandaoni, mara mabibo hostel ni dangulo., nadhani maadili yamepungua au kasi ya ngono imeshika hatamu vyuo vikuu or utandawazi umekomaa.

..anyway nawaachia wenyewe waamue maana ukizama sana utakutana na maswala ya hki yakufanya lolote ila usivunje sheria. ..?..??

Bolded part...Breaking it down huh?Well,it takes two to ngono!
But,what these students do in the secrecy of their dorm rooms is a different issue all together.
Wadada wataachaje kudress to kill iwapo wakaka bado mnaendorse such attitudes?Until it is of no social importance for one to dress for attention,tutabaki tunatwanga maji kwenye kinu.
All in all,I see it more of a moral cry than anything else and when it comes to morals,who is to decide?
 
Hili ni moja yamakosa mengi ayanayofanywa na viongozi wetu, au baadhi yetu .Hatupendi kujua mzizi wa tatizo

Mwanafunzi wa chuo kikuu hajatokea tu hewani-ameanzia vidudu(chekechea/nursey school) mtaani kwao, primary kasoma Tanga, O-level kasoma Dodoma, A-level kasoma Mwanza. Chuo kikuu anakuja DSM.(mfano)

Huko kote anaruhusiwa kuvaa kwa staili yeyote kwani sio kioo cha taifa? mpaka afike chuo kikuu? Hivi nani anaona watoto wa sekondari wanavyovaa siku hizi? au kuvaa mpaka iwe siku za shule tu.

Taifa linaanzia, nyumbani, mtaani, kitongojini, kata, tarafa, wilaya, mkoa , zone, na ndio taifa!!!!! wanafunzi hawa wanatoka huko walikotoka na tabia zao, leo hii mnataka muwabadilishe CHA AJABU WENGI WANAJISAHAU WAKIDHANI HAWA NI WATOTO KUNA WENGINE WANA FAMILIA, NI BABA NA AKINA MAMA FULANI.

Kama mtoa maada alivyosema, kuna mengi ya kutatua kwa sasa, hili tumechelewa mno, maana ni dunia ya 'domokrachia' sio demokrasia, haki za binadamu-ubepari , at least tungekuwa na ujamaa wetu, enzi zile mtoto analelewa na jamii na sio baba na mama tu. Siku hizi thubutu, nyoshea kidole mtoto wa mtu uone-Morogoro mpaka wazazi wanawapiga walimu!!

Mh. Mbunge-tuanze na ngazi ya familia pengine utaona ugumu wa hili swala, anza na hapo bungeni , mawaziri wangapi na wabunge wangapi watoto wao wanaishi maisha ya 'kizungu' ?? yes -no nyingi, beach kila wikendi na baba zao huku wamevaa nguo fupi na zinatisha(eti maendeleo) , wamepata approve za wazazi wao! leo waziri unaamka usingizini! watoto wameruhusiwa na wazazi wao kuvaa nguo fupi leo hii unataka kuzuia!

pengine anzisheni uniform, au maadamu mmeanza na hili la maaskari, wekeni shift ya maaskari kila hall/residents kuzuia nguo fupi! kazi ni wale wanaotoka makwao! au au askari kushindwa uzalendo!

wakatabau
 
Unirvity is the hill of intellectuals but now days itis the hill of stupidity ,inakuwaje msomi anayesoma elimu,sheria, kuvaa huku anabaki yuko uchi ,ni kweli aliseyesema elimu ni ujinga kakukosea.msomi wa chuo kikuu ambaye ni kioo cha jamii.leo anafanya mambo haya>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>..
 
Back
Top Bottom