Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wana-JF wenzangu, nisaidieni, maana nimechanganyikiwa. Hivi karibuni vyombo vya habari, hususan magazeti, vimekuwa vikiripoti vituko, vurugu, umafia na ufisadi katika kampeni za uchaguzi za CCM zilizoanzia katika uchukuaji fomu za kugombea.
Aidha mara kwa mara tumekuwa tunasikia akina Makamba, Msekwa, Dr Shein, Pinda na viongozi/makada wengine wakuu wa chama hicho wakisema kwa kuwa CCM ni nambari wani, basi CCM ni chama bora kinachopaswa kuigwa na vyama vya wapinzani katika kufanya kampeni za kistaarabu zisizokuwa na vurugu.
Swali langu: Mbona mawili haya hayaendani? Kweli vyama vya upinzani vinapaswa kuiga mfano wa CCM, au CCM wana maana gani hasa wanaposema wao ni mfano bora wa kuigwa? Malaria Sugu, labda tuanze na wewe ni kweli chama chako ni mfano mzuri wa kuigwa?
Jibu nisilolitarajia ni kwamba vurugu, umafia na ufisadi wote huu ni ukomavu wa siasa/demokrasia. Siamini iwapo yuko kiongozi wa CCM anaweza kutamka hivyo hadharani.