Akilihuru
JF-Expert Member
- May 20, 2022
- 1,444
- 2,833
Vipi wakuu.
Ki ukweli inashangaza sana raisi wa nchi ambayo ina jeshi, polisi na serikali, lakini anakosa kupata habari za kiintelejensia kuhusu kile kinachoweza kumtokea mbeleni endapo atataka kutumia mamlaka yake kama raisi kupambana na mtu au nchi inayomshinda kila kitu.
Najua fika kuwa Burundi ni nchi yenye nguvu za wastani kijeshi, hii ni kutokana na uzoefu waliokuwa nao pindi walipokuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka zaidi ya ishirini iliyopita. Lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya kujiona kuwa wanaweza kuingia vitani na Rwanda hata kidogo. Kufanya hivyo itakuwa ni kujichimbia kaburi yenyewe au raisi Ndayishimiye kukata kuti alilokalia mwenyewe na msumeno.
Katika East Africa nzima ukiitoa Kenya na Tanzania, hakuna nchi nyingine ambayo inaweza kusimama na Rwanda vitani ikashinda, hata hiyo Uganda yenyewe inaweza kuhenyeshwa na kutepeteshwa vibaya, achilia mbali nchi ambazo ni nyepesi kupigwa kama Burundi au Congo.
Kama kuna tatizo lolote kutoka Rwanda, ni vizuri ndugu Ndayishimiye alipeleke hilo swala katika vikao vya EAC community wakae walijadili na kama wakiona inafaa kulichukulia hatua watafanya hivyo bila kupendelea upande wowote maana wote ni wanachama wa EAC, lakini swala la kuingia vitani ni Rwanda, litakiweka kiti chake na maisha yake kwa ujumla hatarini, alafu baada ya kichapo Kagame akiwaruhusu wale waliokimbilia nchini Rwanda warudi wakaendeshe nchi yao, watu wataanza kulalamika kuwa Rwanda ilikuwa inafanya choko choko ili baadae iweke watutsi.
Muda ni huu wa kulishughulikia hili swala kwa njia za kidiplomasia, asingoja kuwa too late, akaja kujuta baadae huku akiwa njiani na familia yake wakitimkia Tanzania kupata hifadhi ya kikimbizi. Burundi ipo uchi sana mbele ya intelejensia ya Rwanda, hivyo ni rahisi kuangamizwa vibaya nchini mwao wenyewe.
Afunge mpaka wake na Rwanda, hilo ni sawa, lakini asithubutu kutuma jeshi likathubutu kuingia Rwanda kwa kisingizio cha kwenda kuwatafuta wabaya wake, ataangamia vibaya mno na sisi kwa vile tuko na yetu ya umeme, uchaguzi wa serikali za mitaa na ule wa 2025 basi hatutakuwa na muda wa kwenda kumsaidia kama tulivyomsaidia kurudi madarakani raisi Ngurunziza katika mapinduzi ya mwaka 2015.
Ki ukweli inashangaza sana raisi wa nchi ambayo ina jeshi, polisi na serikali, lakini anakosa kupata habari za kiintelejensia kuhusu kile kinachoweza kumtokea mbeleni endapo atataka kutumia mamlaka yake kama raisi kupambana na mtu au nchi inayomshinda kila kitu.
Najua fika kuwa Burundi ni nchi yenye nguvu za wastani kijeshi, hii ni kutokana na uzoefu waliokuwa nao pindi walipokuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka zaidi ya ishirini iliyopita. Lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya kujiona kuwa wanaweza kuingia vitani na Rwanda hata kidogo. Kufanya hivyo itakuwa ni kujichimbia kaburi yenyewe au raisi Ndayishimiye kukata kuti alilokalia mwenyewe na msumeno.
Katika East Africa nzima ukiitoa Kenya na Tanzania, hakuna nchi nyingine ambayo inaweza kusimama na Rwanda vitani ikashinda, hata hiyo Uganda yenyewe inaweza kuhenyeshwa na kutepeteshwa vibaya, achilia mbali nchi ambazo ni nyepesi kupigwa kama Burundi au Congo.
Kama kuna tatizo lolote kutoka Rwanda, ni vizuri ndugu Ndayishimiye alipeleke hilo swala katika vikao vya EAC community wakae walijadili na kama wakiona inafaa kulichukulia hatua watafanya hivyo bila kupendelea upande wowote maana wote ni wanachama wa EAC, lakini swala la kuingia vitani ni Rwanda, litakiweka kiti chake na maisha yake kwa ujumla hatarini, alafu baada ya kichapo Kagame akiwaruhusu wale waliokimbilia nchini Rwanda warudi wakaendeshe nchi yao, watu wataanza kulalamika kuwa Rwanda ilikuwa inafanya choko choko ili baadae iweke watutsi.
Muda ni huu wa kulishughulikia hili swala kwa njia za kidiplomasia, asingoja kuwa too late, akaja kujuta baadae huku akiwa njiani na familia yake wakitimkia Tanzania kupata hifadhi ya kikimbizi. Burundi ipo uchi sana mbele ya intelejensia ya Rwanda, hivyo ni rahisi kuangamizwa vibaya nchini mwao wenyewe.
Afunge mpaka wake na Rwanda, hilo ni sawa, lakini asithubutu kutuma jeshi likathubutu kuingia Rwanda kwa kisingizio cha kwenda kuwatafuta wabaya wake, ataangamia vibaya mno na sisi kwa vile tuko na yetu ya umeme, uchaguzi wa serikali za mitaa na ule wa 2025 basi hatutakuwa na muda wa kwenda kumsaidia kama tulivyomsaidia kurudi madarakani raisi Ngurunziza katika mapinduzi ya mwaka 2015.