GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Ndani ya ccm na hata huko upinzani kumetawaliwa na vita tu, Watu wengi ambao sio wanachama wa vyama hivi vya siasa huona vita wakati wa kura za maoni na uchaguzi tu. Kiuhalisia vita inatokota wakati wote usipokuwa makini unaangushiwa jumba bovu
Hakuna mwana CCM au wa upinzani anayeridhika jina lake kukatwa au kuenguliwa na watu wanaojiita kamati kuu ya ccm au kamati kuu ya Chadema, Act wakati alishinda kura za maoni
Nashangaa kuona wakati wa vita wanajitokeza watu kushauri aina za mbinu za kumdhoofisha adui
Kuna watu wanasema aachiwe huru bila masharti yeyote na kuna Wengine wanasema amekosa kitu gani abaki huko huko ndani mpaka pale wazungu watakapotoa ripoti kama ile inayosema Tanzania ni nchi maskini, choka mbaya, hoe hae na imeelemewa na madeni na Umaskini uliotopea kama Ethiopia na Eritrea
Tangu lini watu wakapangiana silaha za kutumia katikati ya vita ambavyo havijulikana lengo lake na mwisho wake
Ndani ya ccm watu kutumia fimbo kuchapana wakati wa uchaguzi ni jambo la kawaida, Na hata Wengine huchapana kwa njia za giza kwa kutumia masangoma na mambo ya giza ni muendelezo wa kila siku
Vita ni vita tu hakuna kuchagua silaha na kupangiana mbinu, Kuna wakati pesa imetumika kama fimbo za kuchapia na kumdhoofisha adui kwa kuhonga wajumbe na kukodi watu wa Kuandika na kuchafuana, Hizi kamati hujulikana kama Kamati za fitina na majungu na zina Mwenyekiti, Katibu na mtunza hazina
Ni ngumu sana kuingilia vita usiyoijua Chanzo chake, Chimbuko, uhalisia na muanzilishi wa vita husika,
Marekani ni Taifa kubwa sana lenye silaha na nguvu za kila aina kutafuta adui duniani, Lakini kuna wakati ameamua kuondoka Afghanistan na Iraq sio kwa kupenda au kulazimisha bali baada ya mbinu kushindwa , hasara ya kupoteza wanajeshi, Na kuongezeka kwa wanajeshi wazawa wasaliti wa nchi husika aliowafunza mmerekani mwenyewe
Tambua vita hudumu kwa wakati mrefu kama adui hajulikani vizuri au kama adui anatumia Raia kama ngao ya kumkinga au anaanzisha mashambulizi katikati ya Makazi ya Raia wema na wasiokuwa na hatia
Kuna mifano mingi ya vita imekwisha tokea ndani ya vyama vya siasa na Wengine walisalimu amri na kuna Wengine mpaka Leo wamegoma kuomba msamaha au kusalimu amri
Vita ya Humprey Polepole na hao wahuni
Vita ya Bernard Membe na Bashiru and the Company
Vita ya Zito Kabwe and the company VS Chadema
Vita ya Tundu lissu na Marehamu JPM
Vita ya kambi ya lowasa na kambi ya Membe na JK
Vita ya Job Ndugai na Yule kada aliyepigwa Rungu
Vita ya Makamba Yusufu, Kinana you VS Bashiru and the company
Vita ya Nape Nnauye, Makamba January, Membe VS JPM
Vita ya Sofia Simba, Emanuel Nchimbi Vs Kambi ya JPM
Wakati wa vita hakuna kupangiana silaha za kumteketeza adui, Vita haina urafiki,Katikati ya vita hakuna mawasiliano wala majadiliano. Majadiliano hufanyika kabla ya vita au baada ya vita mmoja anapoamua kusalimu amri
Aachiwe huru au asiachiwe huru inategemea lengo la vita kama muanzilishi anafahamu nguvu ya adui au haifahamu, Na hata kama anafahamu nguvu ya adui itategemea uwezo wake wa kuhifadhi silaha na kuzitumia vizuri, Huwezi endesha vita kwa Fedha za mikopo na misaada muda wowote mikopo na misaada ikikata utasababisha maafa makubwa kwa Raia na wapiganaji wanaokuunga mkono
Hakuna mwana CCM au wa upinzani anayeridhika jina lake kukatwa au kuenguliwa na watu wanaojiita kamati kuu ya ccm au kamati kuu ya Chadema, Act wakati alishinda kura za maoni
Nashangaa kuona wakati wa vita wanajitokeza watu kushauri aina za mbinu za kumdhoofisha adui
Kuna watu wanasema aachiwe huru bila masharti yeyote na kuna Wengine wanasema amekosa kitu gani abaki huko huko ndani mpaka pale wazungu watakapotoa ripoti kama ile inayosema Tanzania ni nchi maskini, choka mbaya, hoe hae na imeelemewa na madeni na Umaskini uliotopea kama Ethiopia na Eritrea
Tangu lini watu wakapangiana silaha za kutumia katikati ya vita ambavyo havijulikana lengo lake na mwisho wake
Ndani ya ccm watu kutumia fimbo kuchapana wakati wa uchaguzi ni jambo la kawaida, Na hata Wengine huchapana kwa njia za giza kwa kutumia masangoma na mambo ya giza ni muendelezo wa kila siku
Vita ni vita tu hakuna kuchagua silaha na kupangiana mbinu, Kuna wakati pesa imetumika kama fimbo za kuchapia na kumdhoofisha adui kwa kuhonga wajumbe na kukodi watu wa Kuandika na kuchafuana, Hizi kamati hujulikana kama Kamati za fitina na majungu na zina Mwenyekiti, Katibu na mtunza hazina
Ni ngumu sana kuingilia vita usiyoijua Chanzo chake, Chimbuko, uhalisia na muanzilishi wa vita husika,
Marekani ni Taifa kubwa sana lenye silaha na nguvu za kila aina kutafuta adui duniani, Lakini kuna wakati ameamua kuondoka Afghanistan na Iraq sio kwa kupenda au kulazimisha bali baada ya mbinu kushindwa , hasara ya kupoteza wanajeshi, Na kuongezeka kwa wanajeshi wazawa wasaliti wa nchi husika aliowafunza mmerekani mwenyewe
Tambua vita hudumu kwa wakati mrefu kama adui hajulikani vizuri au kama adui anatumia Raia kama ngao ya kumkinga au anaanzisha mashambulizi katikati ya Makazi ya Raia wema na wasiokuwa na hatia
Kuna mifano mingi ya vita imekwisha tokea ndani ya vyama vya siasa na Wengine walisalimu amri na kuna Wengine mpaka Leo wamegoma kuomba msamaha au kusalimu amri
Vita ya Humprey Polepole na hao wahuni
Vita ya Bernard Membe na Bashiru and the Company
Vita ya Zito Kabwe and the company VS Chadema
Vita ya Tundu lissu na Marehamu JPM
Vita ya kambi ya lowasa na kambi ya Membe na JK
Vita ya Job Ndugai na Yule kada aliyepigwa Rungu
Vita ya Makamba Yusufu, Kinana you VS Bashiru and the company
Vita ya Nape Nnauye, Makamba January, Membe VS JPM
Vita ya Sofia Simba, Emanuel Nchimbi Vs Kambi ya JPM
Wakati wa vita hakuna kupangiana silaha za kumteketeza adui, Vita haina urafiki,Katikati ya vita hakuna mawasiliano wala majadiliano. Majadiliano hufanyika kabla ya vita au baada ya vita mmoja anapoamua kusalimu amri
Aachiwe huru au asiachiwe huru inategemea lengo la vita kama muanzilishi anafahamu nguvu ya adui au haifahamu, Na hata kama anafahamu nguvu ya adui itategemea uwezo wake wa kuhifadhi silaha na kuzitumia vizuri, Huwezi endesha vita kwa Fedha za mikopo na misaada muda wowote mikopo na misaada ikikata utasababisha maafa makubwa kwa Raia na wapiganaji wanaokuunga mkono