Mtoboasiri
JF-Expert Member
- Aug 6, 2009
- 5,101
- 1,946
Imebidi niandike makala hii baada ya tukio la kihistoria la siku tatu zilizopita juu ya anga ya Israel, na kuona kuwa huenda wengi hapa hawatakuwa na nyenzo au taarifa zitakazowasaidia kuli-analyse ipasavyo tukio hilo. Ni dhahiri kuwa SAI iliyoweza kupenya mazindiko ya anga (radar) ya Israel yasiyo na mfano popote duniani, na kusafiri kwa zaidi ya saa tatu hadi kwenye ncha ya vituo vya nuklia vya Israel....hii si hatua ndogo hasa ukiangalia uwezo mkubwa wa Israel na Marekani.
Ni dhahiri, baada ya bw Nasrallah kukiri kuwa ni Hizbullah kwa msaada wa Iran ndio waliotuma UAV, au SAI (Unmanned Aerial Vehicle- Safina ya Angani Ijiendeshayo = SAI), hakuna mtu atakayetia shaka sasa juu ya uwezo mkubwa wa Kiteknolojia walio nao Waajemi (Wa-Irani). Kwani kwa anayefuatia mambo, ni mara nyingi sasa Iran imetuonjesha weledi wake wa kiteknolojia. Chukua kwa mfano vita ya 2006 ya Hizbullah na Israel, ambapo kwa kweli Hizb ilimwendesha puta Mwisraeli kwa kuvunja vifaru maarufu vya Merkava (Kitanda cha Mungu:kutokana na wanavyoamini kuwa kina amani), na pia kuishambulia na kuichoma kwa kombora Meli ya kisasa zaidi Saur kwenye mwambao wa Lebanon, ambayo Waisrel waliamini hakuna yeyeto angeweza kuigusa na ndiyo maana wakaiegesha kando ya Lebanon.
Pili ni hekaya mashuhuri ya Iran kuitungua 5-generation SAI ya Marekani, Sentinel RQ-170 (the beast of Kandahar: mnyama wa Kandahar) ambayo haigunduliwi na Radar (kiasi iliposhiriki katika mauaji ya Osama huko Pakistan, Wapakistan hawakuwa na habari yeyote)--ambayo Wairan waliitungua kwa teknolojia bila ya kufyatua kombora na kuweza kuishusha ikiwa na mikwaruzo midogo dogo tu, jambo lililowatia aibu kubwa Wamarekani.
Tatu ni uwezo wa Wairan kupigana na kushinda virusi vikali vya Komputa (tarakilishi) viitwavyo Stuxnet na Flame bila ya msaada wa yeyote.
Nne kutuma kwao, kwa kulipiza kisasi, virusi vilivyofuta kumbukumbu zote za mashirika mawili makuu ya petroli katika Saudi Arabia na Qatar na kuambukiza komputa zaidi ya elfu 40 za mashirika hayo na hadi leo si Wamarekani wala Waarabu wameweza kuviondoa virusi hivyo, kiasi Leon Panetta, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Alhamisi ilibidi awaite wafanyibiashara wakuu wa Marekani na kuwaonya juu ya vita ya kibemasa (tafsiri yangu ya cyberwarfare, kama mchezo wa kibemasa)!
Yote haya yananionesha kuwa Iran, katika baadhi ya nyanja za Teknolojia, iko mbele hata ya Marekani (Jambo hili si rahisi kulichuuza maana watu wengi bado twawaangalia wazungu kama miungu watu, hawashindwi!).
Natija ninayotoka nayo ni kuwa vita ijayo itageuza kabisa sura ya Mashariki ya Kati, ikiwa si dunia nzima. Kwa kweli kuna nchi zitafutika kabisa katika uso wa dunia zizaliwe nyingine mpya- yaani haidhuru eneo litakuwepo lakini mfumo mzima kama tunavyoujua sasa hautakuwepo. Mithili ya yaliyotokea baada ya vita kuu za dunia ya kwanza na ya pili na vita vya hivi karibuni vya Balkani, ambapo nchi mpya zilizuka. Jambo muhimu zaidi, mfumo wa dunia 'world sytem' kama tunavyoujua hivi sasa, nao pia utatoweka.
Jee, una idea nchi gani zitatoweka na zipi zitabakia?
Ndugu, unachokiamini kamwe hakitatokea. Kumbuka vita vya siku sita, Israel pia ilionekana kuwa dhaifu, what happened? Mungu atalilinda taifa lake siku zote hata mbele ya mwisho wa dunia hii! Mungu si mwanadamu hata aseme uongo, na kila alichomuahidi Ibrahim, Isaka na Israel kitatimizwa.