Vita ijayo mashariki ya kati

Sijali

JF-Expert Member
Sep 30, 2010
2,586
1,678
Imebidi niandike makala hii baada ya tukio la kihistoria la siku tatu zilizopita juu ya anga ya Israel, na kuona kuwa huenda wengi hapa hawatakuwa na nyenzo au taarifa zitakazowasaidia kuli-analyse ipasavyo tukio hilo. Ni dhahiri kuwa SAI iliyoweza kupenya mazindiko ya anga (radar) ya Israel yasiyo na mfano popote duniani, na kusafiri kwa zaidi ya saa tatu hadi kwenye ncha ya vituo vya nuklia vya Israel....hii si hatua ndogo hasa ukiangalia uwezo mkubwa wa Israel na Marekani.
Ni dhahiri, baada ya bw Nasrallah kukiri kuwa ni Hizbullah kwa msaada wa Iran ndio waliotuma UAV, au SAI (Unmanned Aerial Vehicle- Safina ya Angani Ijiendeshayo = SAI), hakuna mtu atakayetia shaka sasa juu ya uwezo mkubwa wa Kiteknolojia walio nao Waajemi (Wa-Irani). Kwani kwa anayefuatia mambo, ni mara nyingi sasa Iran imetuonjesha weledi wake wa kiteknolojia. Chukua kwa mfano vita ya 2006 ya Hizbullah na Israel, ambapo kwa kweli Hizb ilimwendesha puta Mwisraeli kwa kuvunja vifaru maarufu vya Merkava (Kitanda cha Mungu:kutokana na wanavyoamini kuwa kina amani), na pia kuishambulia na kuichoma kwa kombora Meli ya kisasa zaidi Saur kwenye mwambao wa Lebanon, ambayo Waisrel waliamini hakuna yeyeto angeweza kuigusa na ndiyo maana wakaiegesha kando ya Lebanon.
Pili ni hekaya mashuhuri ya Iran kuitungua 5-generation SAI ya Marekani, Sentinel RQ-170 (the beast of Kandahar: mnyama wa Kandahar) ambayo haigunduliwi na Radar (kiasi iliposhiriki katika mauaji ya Osama huko Pakistan, Wapakistan hawakuwa na habari yeyote)--ambayo Wairan waliitungua kwa teknolojia bila ya kufyatua kombora na kuweza kuishusha ikiwa na mikwaruzo midogo dogo tu, jambo lililowatia aibu kubwa Wamarekani.
Tatu ni uwezo wa Wairan kupigana na kushinda virusi vikali vya Komputa (tarakilishi) viitwavyo Stuxnet na Flame bila ya msaada wa yeyote.
Nne kutuma kwao, kwa kulipiza kisasi, virusi vilivyofuta kumbukumbu zote za mashirika mawili makuu ya petroli katika Saudi Arabia na Qatar na kuambukiza komputa zaidi ya elfu 40 za mashirika hayo na hadi leo si Wamarekani wala Waarabu wameweza kuviondoa virusi hivyo, kiasi Leon Panetta, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Alhamisi ilibidi awaite wafanyibiashara wakuu wa Marekani na kuwaonya juu ya vita ya kibemasa (tafsiri yangu ya cyberwarfare, kama mchezo wa kibemasa)!
Yote haya yananionesha kuwa Iran, katika baadhi ya nyanja za Teknolojia, iko mbele hata ya Marekani (Jambo hili si rahisi kulichuuza maana watu wengi bado twawaangalia wazungu kama miungu watu, hawashindwi!).
Natija ninayotoka nayo ni kuwa vita ijayo itageuza kabisa sura ya Mashariki ya Kati, ikiwa si dunia nzima. Kwa kweli kuna nchi zitafutika kabisa katika uso wa dunia zizaliwe nyingine mpya- yaani haidhuru eneo litakuwepo lakini mfumo mzima kama tunavyoujua sasa hautakuwepo. Mithili ya yaliyotokea baada ya vita kuu za dunia ya kwanza na ya pili na vita vya hivi karibuni vya Balkani, ambapo nchi mpya zilizuka. Jambo muhimu zaidi, mfumo wa dunia 'world sytem' kama tunavyoujua hivi sasa, nao pia utatoweka.
Jee, una idea nchi gani zitatoweka na zipi zitabakia?
 
Imebidi niandike makala hii baada ya tukio la kihistoria la siku tatu zilizopita juu ya anga ya Israel, na kuona kuwa huenda wengi hapa hawatakuwa na nyenzo au taarifa zitakazowasaidia kuli-analyse ipasavyo tukio hilo. Ni dhahiri kuwa SAI iliyoweza kupenya mazindiko ya anga (radar) ya Israel yasiyo na mfano popote duniani, na kusafiri kwa zaidi ya saa tatu hadi kwenye ncha ya vituo vya nuklia vya Israel....hii si hatua ndogo hasa ukiangalia uwezo mkubwa wa Israel na Marekani.
Ni dhahiri, baada ya bw Nasrallah kukiri kuwa ni Hizbullah kwa msaada wa Iran ndio waliotuma UAV, au SAI (Unmanned Aerial Vehicle- Safina ya Angani Ijiendeshayo = SAI), hakuna mtu atakayetia shaka sasa juu ya uwezo mkubwa wa Kiteknolojia walio nao Waajemi (Wa-Irani). Kwani kwa anayefuatia mambo, ni mara nyingi sasa Iran imetuonjesha weledi wake wa kiteknolojia. Chukua kwa mfano vita ya 2006 ya Hizbullah na Israel, ambapo kwa kweli Hizb ilimwendesha puta Mwisraeli kwa kuvunja vifaru maarufu vya Merkava (Kitanda cha Mungu:kutokana na wanavyoamini kuwa kina amani), na pia kuishambulia na kuichoma kwa kombora Meli ya kisasa zaidi Saur kwenye mwambao wa Lebanon, ambayo Waisrel waliamini hakuna yeyeto angeweza kuigusa na ndiyo maana wakaiegesha kando ya Lebanon.
Pili ni hekaya mashuhuri ya Iran kuitungua 5-generation SAI ya Marekani, Sentinel RQ-170 (the beast of Kandahar: mnyama wa Kandahar) ambayo haigunduliwi na Radar (kiasi iliposhiriki katika mauaji ya Osama huko Pakistan, Wapakistan hawakuwa na habari yeyote)--ambayo Wairan waliitungua kwa teknolojia bila ya kufyatua kombora na kuweza kuishusha ikiwa na mikwaruzo midogo dogo tu, jambo lililowatia aibu kubwa Wamarekani.
Tatu ni uwezo wa Wairan kupigana na kushinda virusi vikali vya Komputa (tarakilishi) viitwavyo Stuxnet na Flame bila ya msaada wa yeyote.
Nne kutuma kwao, kwa kulipiza kisasi, virusi vilivyofuta kumbukumbu zote za mashirika mawili makuu ya petroli katika Saudi Arabia na Qatar na kuambukiza komputa zaidi ya elfu 40 za mashirika hayo na hadi leo si Wamarekani wala Waarabu wameweza kuviondoa virusi hivyo, kiasi Leon Panetta, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Alhamisi ilibidi awaite wafanyibiashara wakuu wa Marekani na kuwaonya juu ya vita ya kibemasa (tafsiri yangu ya cyberwarfare, kama mchezo wa kibemasa)!
Yote haya yananionesha kuwa Iran, katika baadhi ya nyanja za Teknolojia, iko mbele hata ya Marekani (Jambo hili si rahisi kulichuuza maana watu wengi bado twawaangalia wazungu kama miungu watu, hawashindwi!).
Natija ninayotoka nayo ni kuwa vita ijayo itageuza kabisa sura ya Mashariki ya Kati, ikiwa si dunia nzima. Kwa kweli kuna nchi zitafutika kabisa katika uso wa dunia zizaliwe nyingine mpya- yaani haidhuru eneo litakuwepo lakini mfumo mzima kama tunavyoujua sasa hautakuwepo. Mithili ya yaliyotokea baada ya vita kuu za dunia ya kwanza na ya pili na vita vya hivi karibuni vya Balkani, ambapo nchi mpya zilizuka. Jambo muhimu zaidi, mfumo wa dunia 'world sytem' kama tunavyoujua hivi sasa, nao pia utatoweka.
Jee, una idea nchi gani zitatoweka na zipi zitabakia?

P.U.M.B.A.V.U Hujuhi unachoongea wewe.
 
una madharau ya kiseng,e,sasa kama hajui analoongea hebu lete point yako kuhusiana na vita inayokuja
Haukuna nchi itakayoweza kuipiga Israel. Teknolojia ya Israel na iran ni sawa na kufananisha mbingu na ardhi, Israel iko mbali sana kuliko Irani, Hilo jamaa linaongea kishabiki
 
Iran inatapa tapa sasa waulize dollar ecchange ni rial ngapi,pia detection ya UAV inamaana radar iko active na kama ingekuwa weak hakika isingekuweza detect.
Pili tuweke ushabiki pembeni cyber war najua iko active sio kiasi cha wao kushindwa toa hao virus

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Msimvamie mtoa mada kwa matusi ya kishabiki, mimi nadhani mngemuomba alete link ya hizo information, na kama ni mambo ya millitary confidential alizipataje.Wakati mwingine sio lazima ziletwe Topic zinazowafurahisha tuu!
 
Haukuna nchi itakayoweza kuipiga Israel. Teknolojia ya Israel na iran ni sawa na kufananisha mbingu na ardhi, Israel iko mbali sana kuliko Irani, Hilo jamaa linaongea kishabiki

Prisoner exchange admits Israeli defeat in 2006 Lebanon war

Lebanese government noted correctly that Hezbollah pushed Israel to the very same terms it refused before the 2006 Israeli war with Lebanon. Hezbollah was asking Israel to release Samir Kuntar. After Israel’s repeated refusals Hezbollah attacked an IDF outpost, took Regev and Goldwasser prisoners, and now exchanged their bodies for Kuntar.
Had Israeli government released Kuntar in early 2006, more than a hundred Israelis including Regev and Goldwasser would have been alive.

Source: Israeli News: Prisoner exchange admits Israeli defeat in 2006 Lebanon war
 
Ktk Top 10 ya majeshi yenye nguvu duniani,israel ipo na cha kushangaza ina wanajeshi wachache kupindukia,kombora dogo kuliko yote duniani limevumbuliwa na israel mwaka huu na wamemuuzia teknolojia mrusi kombora lenyewe lina uzito wa kilo nne na ni dogo kama rula na effect zake ni kama kombora linalobebwa na magari makubwa ya kijeshi...toa udini wako hv ufikirii kwa middle east nchi zinazoizunguka israel zikiweka silaha chini amani itakuja,ila israel akiweka silaha chini kifo kitamjia,for years wamemshindwa,sasa subiri soon uone iran itakavyobamizwa baada ya hapo mataifa ya kiarabu pamoja na urusi watakapovamia israel na kuharibiwa kabla ya kuingia mpinga kristo
 
kabla ya kuingia mpinga kristo??hebu dadavua
Ktk Top 10 ya majeshi yenye nguvu duniani,israel ipo na cha kushangaza ina wanajeshi wachache kupindukia,kombora dogo kuliko yote duniani limevumbuliwa na israel mwaka huu na wamemuuzia teknolojia mrusi kombora lenyewe lina uzito wa kilo nne na ni dogo kama rula na effect zake ni kama kombora linalobebwa na magari makubwa ya kijeshi...toa udini wako hv ufikirii kwa middle east nchi zinazoizunguka israel zikiweka silaha chini amani itakuja,ila israel akiweka silaha chini kifo kitamjia,for years wamemshindwa,sasa subiri soon uone iran itakavyobamizwa baada ya hapo mataifa ya kiarabu pamoja na urusi watakapovamia israel na kuharibiwa kabla ya kuingia mpinga kristo
 
Inawezekana kweli kuwa muisrael ameishiwa nguvu na hana mvuto tena na ushawishi kwenye jumuia za kimataifa,hilo ni kawaidia kabisa.Mrusi naye halikadharika keshachoka.Sasa tunazungumzia EU ambaye juzi kapewa noble price,ni ukweli usiopingika kuwa amani ya dunia sasa itashikiliwa na muungano wa nchi za ulaya,nchi za mashariki ya kati zitalazimika kufuata mkumbo na zitatii kwa kulazimishwa na america chini ya utawala wa roma
 
Imebidi niandike makala hii baada ya tukio la kihistoria la siku tatu zilizopita juu ya anga ya Israel, na kuona kuwa huenda wengi hapa hawatakuwa na nyenzo au taarifa zitakazowasaidia kuli-analyse ipasavyo tukio hilo. Ni dhahiri kuwa SAI iliyoweza kupenya mazindiko ya anga (radar) ya Israel yasiyo na mfano popote duniani, na kusafiri kwa zaidi ya saa tatu hadi kwenye ncha ya vituo vya nuklia vya Israel....hii si hatua ndogo hasa ukiangalia uwezo mkubwa wa Israel na Marekani.
Ni dhahiri, baada ya bw Nasrallah kukiri kuwa ni Hizbullah kwa msaada wa Iran ndio waliotuma UAV, au SAI (Unmanned Aerial Vehicle- Safina ya Angani Ijiendeshayo = SAI), hakuna mtu atakayetia shaka sasa juu ya uwezo mkubwa wa Kiteknolojia walio nao Waajemi (Wa-Irani). Kwani kwa anayefuatia mambo, ni mara nyingi sasa Iran imetuonjesha weledi wake wa kiteknolojia. Chukua kwa mfano vita ya 2006 ya Hizbullah na Israel, ambapo kwa kweli Hizb ilimwendesha puta Mwisraeli kwa kuvunja vifaru maarufu vya Merkava (Kitanda cha Mungu:kutokana na wanavyoamini kuwa kina amani), na pia kuishambulia na kuichoma kwa kombora Meli ya kisasa zaidi Saur kwenye mwambao wa Lebanon, ambayo Waisrel waliamini hakuna yeyeto angeweza kuigusa na ndiyo maana wakaiegesha kando ya Lebanon.
Pili ni hekaya mashuhuri ya Iran kuitungua 5-generation SAI ya Marekani, Sentinel RQ-170 (the beast of Kandahar: mnyama wa Kandahar) ambayo haigunduliwi na Radar (kiasi iliposhiriki katika mauaji ya Osama huko Pakistan, Wapakistan hawakuwa na habari yeyote)--ambayo Wairan waliitungua kwa teknolojia bila ya kufyatua kombora na kuweza kuishusha ikiwa na mikwaruzo midogo dogo tu, jambo lililowatia aibu kubwa Wamarekani.
Tatu ni uwezo wa Wairan kupigana na kushinda virusi vikali vya Komputa (tarakilishi) viitwavyo Stuxnet na Flame bila ya msaada wa yeyote.
Nne kutuma kwao, kwa kulipiza kisasi, virusi vilivyofuta kumbukumbu zote za mashirika mawili makuu ya petroli katika Saudi Arabia na Qatar na kuambukiza komputa zaidi ya elfu 40 za mashirika hayo na hadi leo si Wamarekani wala Waarabu wameweza kuviondoa virusi hivyo, kiasi Leon Panetta, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Alhamisi ilibidi awaite wafanyibiashara wakuu wa Marekani na kuwaonya juu ya vita ya kibemasa (tafsiri yangu ya cyberwarfare, kama mchezo wa kibemasa)!
Yote haya yananionesha kuwa Iran, katika baadhi ya nyanja za Teknolojia, iko mbele hata ya Marekani (Jambo hili si rahisi kulichuuza maana watu wengi bado twawaangalia wazungu kama miungu watu, hawashindwi!).
Natija ninayotoka nayo ni kuwa vita ijayo itageuza kabisa sura ya Mashariki ya Kati, ikiwa si dunia nzima. Kwa kweli kuna nchi zitafutika kabisa katika uso wa dunia zizaliwe nyingine mpya- yaani haidhuru eneo litakuwepo lakini mfumo mzima kama tunavyoujua sasa hautakuwepo. Mithili ya yaliyotokea baada ya vita kuu za dunia ya kwanza na ya pili na vita vya hivi karibuni vya Balkani, ambapo nchi mpya zilizuka. Jambo muhimu zaidi, mfumo wa dunia 'world sytem' kama tunavyoujua hivi sasa, nao pia utatoweka.
Jee, una idea nchi gani zitatoweka na zipi zitabakia?

Please ongea ukweli, nikwamba hiyo UAV au SAI ilionekana mapema wakati inakaribia southern border ya Israel nawao walikuwa tayari washajua na hawakutaka kuitungua mapema vile sababu ya makazi ya watu, wenzetu wanajali utu, hivyo walisubiri mpaka eneo lisilo na makazi ya watu ndipo waitungue.

vita ya hizbullah na Israel, Hizbullah wanajichanganya kwenye makazi ya watu-walebanoni, raia, kwahiyo ulitaka IDF iue raia??

Unajua nini juu ya DEMONA REACTOR?? angekuwepo Rais ambaye marehemu, Rais Kennedy angekueleza na kwanini hadi leo rais anayeingia madarakani wa marekani lazima aiheshimu Israel??

Tusiwe washabiki wa upande wowote!
 
Back
Top Bottom