- iKuimarisha huduma za kinga dhidi ya magonjwa;
- Kuimarisha upatikanaji na ubora wa huduma za afya zinazotolewa na vituo vya kutolea huduma za afya kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Taifa;
- Kuimarisha mifumo ya ugharamiaji wa huduma za afya nchini;
- Kuimarisha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto ili kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga;
- Kuimarisha upatikanaji na uendelezaji wa wataalam katika Sekta ya Afya kwa fani za kati, ubingwa na ubingwa bobezi;
- Kuimarisha huduma za matibabu ya ubingwa na ubingwa bobezi nchini;
- Kuendeleza na kusimamia afua za Tiba Asili na Tiba Mbadala;
- Kuimarisha upatikanaji wa huduma za magonjwa ya kuambukiza, magonjwa yasiyoambukiza na magonjwa ya mlipuko;
- Kuimarisha huduma za afya ya akili, huduma za utengamao hususan kwa watoto, wazee na watu wenye ulemavu;
- Kusimamia Tafiti na matumizi ya matokeo ya tafiti mbalimbali za afya
============