Pendragon24
Member
- Aug 8, 2018
- 36
- 65
Mkurugenzi mpya wa masoko, wanachama na mashabiki wa klabu ya Young Africans ndugu Ibrahimu Samweli anatoa wapi mamlaka na uhalali wa kuvunja uongozi wa kuratibu shughuli za matawi ya yanga mkoani Morogoro..!!!? Ikiwa yeye mwenyewe ni mwajiriwa tu pale klabuni.
Kitendo cha kumtoa Mratibu wa mkoa wa Morogoro nje ya utaratibu wa kikatiba na kumuweka mtu ambaye inasadikika ni ndugu yake kinyume na matakwa ya watu je hii ni sawa..!!?
Mbona hatuoni mikoa mingine viongozi wao wa mkoa wakiondolewa pamoja na kiwango cha chini cha utendaji wao wa kazi nani yuko nyuma ya hili au ni maelekezo kutoka juu au ni nini..!!?
Tangu afanye uharibifu huo siku ya jumapili tarehe 18.02.2024 baada ya Mechi ya Young African na KMC katika Ukumbi wa Midland hotel mkoani Morogoro utendaji wa matawi umedolola na hamasa ya mashabiki imeshuka kwa kiwango kikubwa na tukiendelea hivi taswira ya yanga mkoani morogoro itapotea kabisa kwa sababu ya mratibu dhaifu aliowekwa kwenye nafasi si kwa uwezo wake kiutendaji bali kwa undugurism,fitina,majungu na husda.
Young African ni klabu ambayo bado inakua kupitia mchakato wa mabadiliko kama tukiruhusu Majungu,Fitna,Undugu,ubabe na maneno maneno ambayo hayana msingi katika uendeshaji wa klabu mapema namna hii tutajiharibia na kamwe hatutofika tunapokwenda.
Tunataka ndungu Ibrahimu Samwel awajibike katika Utovu wake wa nidhamu wa kuikanyaga Katiba ya klabu yetu. Viongozi na wanachama mkoani morogoro wanataka uongozi uliochaguliwa kwa kura za watu wengi urudi haraka. kufahamu,
1. Alivunja uongozi wa mkoa yeye kama nani..!?
2. Alipata wapi uhalali wa kufanya hivyo kinyume na katiba ya klabu..!?
3. Kapata wapi ujasiri wa kumtoa mratibu aliyechaguliwa kwa kura za watu wengi..!!?
4. Mbona ajafanya hivyo mikoa mingine..!!?
Wapenzi,mashabiki na wanachama wa klabu ya Young Africans mkoani morogoro wamechoka kuburuzwa na kikundi cha watu wachache kinachokanyaga katiba kwa maslai yao na ndugu zao na sio maslai ya wana yanga.
~Rungulukware.
Mwisho,.
Kitendo cha kumtoa Mratibu wa mkoa wa Morogoro nje ya utaratibu wa kikatiba na kumuweka mtu ambaye inasadikika ni ndugu yake kinyume na matakwa ya watu je hii ni sawa..!!?
Mbona hatuoni mikoa mingine viongozi wao wa mkoa wakiondolewa pamoja na kiwango cha chini cha utendaji wao wa kazi nani yuko nyuma ya hili au ni maelekezo kutoka juu au ni nini..!!?
Tangu afanye uharibifu huo siku ya jumapili tarehe 18.02.2024 baada ya Mechi ya Young African na KMC katika Ukumbi wa Midland hotel mkoani Morogoro utendaji wa matawi umedolola na hamasa ya mashabiki imeshuka kwa kiwango kikubwa na tukiendelea hivi taswira ya yanga mkoani morogoro itapotea kabisa kwa sababu ya mratibu dhaifu aliowekwa kwenye nafasi si kwa uwezo wake kiutendaji bali kwa undugurism,fitina,majungu na husda.
Young African ni klabu ambayo bado inakua kupitia mchakato wa mabadiliko kama tukiruhusu Majungu,Fitna,Undugu,ubabe na maneno maneno ambayo hayana msingi katika uendeshaji wa klabu mapema namna hii tutajiharibia na kamwe hatutofika tunapokwenda.
Tunataka ndungu Ibrahimu Samwel awajibike katika Utovu wake wa nidhamu wa kuikanyaga Katiba ya klabu yetu. Viongozi na wanachama mkoani morogoro wanataka uongozi uliochaguliwa kwa kura za watu wengi urudi haraka. kufahamu,
1. Alivunja uongozi wa mkoa yeye kama nani..!?
2. Alipata wapi uhalali wa kufanya hivyo kinyume na katiba ya klabu..!?
3. Kapata wapi ujasiri wa kumtoa mratibu aliyechaguliwa kwa kura za watu wengi..!!?
4. Mbona ajafanya hivyo mikoa mingine..!!?
Wapenzi,mashabiki na wanachama wa klabu ya Young Africans mkoani morogoro wamechoka kuburuzwa na kikundi cha watu wachache kinachokanyaga katiba kwa maslai yao na ndugu zao na sio maslai ya wana yanga.
~Rungulukware.
Mwisho,.