Viongozi wote waliotufikisha kwenye mtanziko huu Watengwe na Kanisa?

gstar

JF-Expert Member
Jun 19, 2011
759
1,250
Sauti ya watu ni sauti ya Mungu, "Vox populi vox Dei." Nimefurahishwa na tamko la Maaskofu wa kanisa Katoliki juu ya mtanziko huu ulio tupata juu ya kusainiwa kwa makubaliano ya uendeshaji wa bandari kupitia kampuni ya DP-World yaliyotuletea wasiwasi mkubwa juu ya mustakabali wa Taifa letu.

Maaskofu 37 wa Tanzania nzima wamepinga mkataba huo kupitia tamko hilo, jambo la kushangaza zaidi ni kwamba viongozi tulio wapa mamlaka bado wameshupaza shingo na kubaki kimya bila kuongea jambo lolote kana kwamba hawakusikia tamko hilo!

Kwakuwa baadhi ya viongozi hao ni waumini wa kanisa Katoliki akiwemo spika wa bunge Tulia Akson na mkamu wa raisi Dk Philip Mpango, ningependa kulishauri baraza la maaskofu kuwafungia sakramenti viongozi hawa (kuwatenga na kanisa) kwani kwa mujibu wa andiko hilo bila shaka wametenda dhambi kubwa sana iliyowapelekea Watanzania wengi kuingia kwenye mtanziko huu.

Ikiwa watatubu na kurudi kwa kukataa mkataba huu basi wasamehewe na warudishwe kwenye ushirika, ama la wakiendelea kusimamia msimamo wao huo wa kuendelea na mkataba huu basi mamlaka ya kikanisa iwahukumu kutokana na matendo yao, wawe 'Excommunicated!' Naamini kwamba kwa kufanya hivyo italeta funzo na heshima kubwa kwa jamii. Mababa zetu wasiishie kutoa tamko tu waende extra miles kwa kuwachukulia hatua waumini wote walio tufikisha hapa kwa kuwa excommunicate.

Hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yao ikiwemo kuwazuia kukaa viti vya mbele, na pia wale wasio Wakatoliki wazuiwe kuhudhuria matamasha ya kikanisa wasije wakatumia majukwaa ya kikanisa kuendelea kusambaza propaganda zao kama alivyofanya mstaafu Kikwete huko mkoa wa Mara kwenye tamasha la Wasabato.

Haya ni maoni yangu binafsi.
 
Kwani Tanzania ni nchi ya watu wa dini moja ya Katoliki?

Sauti hiyo ya mungu inayotajwa na Maaskofu ni Mungu yupi?

Maana Waislamu wao Allah wao ni mmoja, hana mshirika, wala hana mtoto.

Wakatoliki mungu wao ana mtoto wake, na pia ni ushirikiano wa Mungu baba, mungu mwana (Yesu), na Mungu roho mtakatifu.

Wapagani wao wana miungu yao kama Mizimu, miti, mawe, wanyama mbalimbali.

Ni dhahiri kila mdau ana mungu wake tofauti kabisa, sasa hii sauti ya mungu ni mungu yupi
 
Kwani Tanzania ni nchi ya watu wa dini moja ya Katoliki?

Sauti hiyo ya mungu inayotajwa na Maaskofu ni Mungu yupi?

Maana Waislamu wao Allah wao ni mmoja, hana mshirika, wala hana mtoto.

Wakatoliki mungu wao ana mtoto wake, na pia ni ushirikiano wa Mungu baba, mungu mwana (Yesu), na Mungu roho mtakatifu.

Wapagani wao wana miungu yao kama Mizimu, miti, mawe, wanyama mbalimbali.

Ni dhahiri kila mdau ana mungu wake tofauti kabisa, sasa hii sauti ya mungu ni mungu yupi
Mungu mmoja aliyeko mbinguni
 
Sio Kazi ya kanisa kumtenga mdhambi bali wote wenye dhambi wakiwemo mashoga,wezi, makahaba wanaaitwa kanisan wakapate tiba.
 
Hakuna dini ya taifa na serikali yetu haina dini ila wananchi wanauhuru wa kuabudu dini yeyote ile ,hivyo basi viongozi wa dini hawataamua nakuingilia masuala ya kisiasa, na huko mbeleni ni lazima kuweka vifungu vya kisheria vya kuwabana maana umoja wetu ni wa maana zaidi kuliko dini zetu na pia umoja wetu hasa ndio sauti ya mungu.
 
Nadhani wakatoliki na hata madhehebu mengine wanaelewa maana ya kutengwa na huduma za kanisa.
Mtu kama Dr Mpango anaelewa vizuri sana maana ya neno kutengwa. Na kama ni mkatoliki wa kweli kama anavyojinasibu, basi kwake atakuambia bora hata ajiuzulu umakamu kuliko kutengwa na kanisa lake, ni adhabu kubwa sana kiroho.
 
Back
Top Bottom