Viongozi wa kuwalaumu Kwa hasara za majengo Dar na Ufanisi wa Bandari ni hawa

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,464
4,145
Kumetokea tabia ya baadhi ya viongozi na wanasiasa kudai hasara au matatizo ya Tanzania ya Mosi kuhamia Dodoma kuliko fanywa na Hayati Magufuli, ni kukosa ueledi wa uongozi, bila kujua Mpango wa Nchi alioacha Mwalimu ilikuwaje.

Kuhusu Dodoma, Mwalimu aliacha Ofisi za Waziri Mkuu na Wizara kadha kuwa zimehamia Dodoma mojawapo ukiwa ni serikali za Mitaa. Sasa ilikuwa ni jukumu la viongozi walifuata kulitekeleza Hilo, lakini badala yake Ofisi wa Waziri Mkuu na serikali za Mtaa wakarudi Dar, na baadae wizarabzote na kuanza kujenga Offisi za taasisi tofauti tofauti DAR. Na hiyo ilikuwa Awamu ya Pili (Ya Ali Hassan) ikafuata ya Mkapa na Kikwete.

Kulikuwa hakuna haja ya kujenga Offisi za NHC , LATRA n.k DAR , na za hii mifuko ya kijamii , wakati Waziri Husika anahudhuria vikao vya Baraza la mawaziri hivyo kuelewa uelekeo wa Nchi katika kuhamia Dodoma. Ya Bandari nayo , Mipango ya Bandari kavu ya kwala na kabla ya hapo ilikuwa Kimara/Mbezi kulitekeleza mapema ili watu wafaidike na ICD badala ya nchi.

Hata mongo wa isaka Bandari kavuu ulikuwa mpango WA siku nyingi lakini haikuwa ikitekelezwa Kwa sababu binafsi. Hivyo hata hitaji la DP weldi lisinge kuwepo kama viongozi waliotangulia wangetekeleza Mpango wa Bandari Kavu, na viongozi hao wanatakiwa kumshukuru Marehemu JPM Kwa uthubutu alioonyesha.

Jingine ni kutokuwepo Mpango wa muda mrefu WA kueaongoza wa Tanzania wengi kwenye mfumo wa Kodi na NHIF.

Hivyo alikuwa na Nia ya kukimbia ili kufidia miongo mitatu tuliopoteza, Kwa kutofuata Mpango wa Nchi ikiwemo Bwawa la Rufiji.
 
Nachukizwa na watu vyeti bandia (Vilaza) wezi, wanufaikaji wa wafanyakazi hewa, wazembe maofisini, mafisadi, wauza ngada,wala rushwa na takataka nyinginezo kama hizo!

Siku yao na dawa yao iko jikoni inachemka!
 
Ofisi za serikali na watumishi hawapo kama mapambio, ni kwa ajili ya kutoa huduma wa wananchi.
Kwa hiyo, lazima kuangalia kati ya eneo fulani na jingine, wapi penye wananchi wengi wahitaji wa huduma hizo?
 
Back
Top Bottom