Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamezidi kubanwa na mahakama baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kuwafungulia mashitaka mapya yanayohusu maandamano ya Arusha.
Hata hivyo, DPP pia amewaachia huru washitakiwa wengine 11 baada ya kubaini kuwa hawahusiki na kesi iliyowafikisha mahakamani hapo.
Viongozi waliofunguliwa mashitaka mapya manane ni Mwenyekiti Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na Mbunge wa Moshi Mjini Philemon Ndesamburo.
Wanasiasa hao wanaungana na wanachama na wafuasi wengine 16 akiwamo mchumba wa Slaa, Josephine Mushumbusi kujibu mashitaka hayo.
Kwa mujibu wa Mwendesha Mashitaka wa Serikali, walioachiwa huru ni Edwin Kakolaki ni Kenneth Bundala, Pochesi Kimario, Eusebia Akaro, Bakari Issa, Goodluck Kimaro, Elisante Noel, Calvin Daudi, Michael Kimario, Mevorongori Lukumay, Prosper Kimaro na Pancras Kimario.
Akizungumza nje ya mahakama, Lema alisema, haitakuwa ajabu kufungwa akitolea mfano wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, kwamba alifungwa, lakini bado akawa shujaa wa nchi yake.
Kakolaki alitaja mashitaka hayo mapya dhidi ya viongozi hao na wenzao, kuwa ni kula njama ya kutenda makosa ya kufanya mkusanyiko, kukaidi amri ya Jeshi la Polisi, kufanya mkusanyiko isivyo halali na kufanya vurugu baada ya kutolewa amri ya Polisi.
Mashitaka mengine ambayo yanamhusu Slaa peke yake ni kutoa maneno ya uchochezi Januari 5 katika viwanja vya NMC, Arusha, akiwa Katibu Mkuu wa Chadema.
Mashitaka mengine yanamhusu Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo, ambayo ni ya kutoa maneno ya uchochezi na kejeli dhidi ya Rais Jakaya Kikwete. Mengine ambayo yanawahusu Ndesamburo, Slaa na Samson Mwigamba ni ya kuchochea na kutaka kutorosha watu waliokuwa chini ya ulinzi Januari 5 kwenye viwanja vya NMC, Arusha.
Pia washitakiwa hao 19 kwa pamoja wanadaiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kusababisha taharuki kwa jamii. Baada ya kusomewa mashitaka hayo, mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Judith Kamala, washitakiwa kwa pamoja walikana mashitaka.
Kakolaki alidai mahakamani hapo kwamba, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba tarehe ya usikilizwaji wa awali wa kesi hiyo. Hakimu Kamala aliamua kesi hiyo ianze kusikilizwa Aprili 29.
Hata hivyo, wafuasi wa Chadema waliokuwa nje ya mahakama waliendelea kutoa maneno ya kejeli baada ya kusikia mashtaka mapya dhidi ya viongozi hao. Baadhi yao walisema mahakama inapaswa kutenda haki wakidai kuwa, mashitaka yamepindishwa na kutenganisha baadhi ya washitakiwa.
Lema alipotoka mahakamani baada ya kesi kuahirishwa, aliwatuliza wafuasi wa chama hicho kwa kuwaambia kuwa hata Mandela alifungwa kwa kupigania haki hivyo wasubiri uamuzi wa mahakama. Aliwasihi wafuasi wa Chadema kutawanyika na kwenda kwenye shughuli zao na warudi mahakamani hapo Aprili 29.
Viongozi hao wa Chadema walifanya maandamano Januari 5 licha ya Polisi kukataza kwa misingi ya kiusalama, lakini pia wafuasi wao wakataka kuvamia kituo kikuu cha Polisi kuwatoa viongozi waliokuwa wanashikiliwa. Katika ghasia hizo, watu watatu walipoterza maisha kwa kupigwa risasi na polisi akiwamo raia mmoja wa Kenya.
Source: Habari Leo
Hata hivyo, DPP pia amewaachia huru washitakiwa wengine 11 baada ya kubaini kuwa hawahusiki na kesi iliyowafikisha mahakamani hapo.
Viongozi waliofunguliwa mashitaka mapya manane ni Mwenyekiti Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na Mbunge wa Moshi Mjini Philemon Ndesamburo.
Wanasiasa hao wanaungana na wanachama na wafuasi wengine 16 akiwamo mchumba wa Slaa, Josephine Mushumbusi kujibu mashitaka hayo.
Kwa mujibu wa Mwendesha Mashitaka wa Serikali, walioachiwa huru ni Edwin Kakolaki ni Kenneth Bundala, Pochesi Kimario, Eusebia Akaro, Bakari Issa, Goodluck Kimaro, Elisante Noel, Calvin Daudi, Michael Kimario, Mevorongori Lukumay, Prosper Kimaro na Pancras Kimario.
Akizungumza nje ya mahakama, Lema alisema, haitakuwa ajabu kufungwa akitolea mfano wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, kwamba alifungwa, lakini bado akawa shujaa wa nchi yake.
Kakolaki alitaja mashitaka hayo mapya dhidi ya viongozi hao na wenzao, kuwa ni kula njama ya kutenda makosa ya kufanya mkusanyiko, kukaidi amri ya Jeshi la Polisi, kufanya mkusanyiko isivyo halali na kufanya vurugu baada ya kutolewa amri ya Polisi.
Mashitaka mengine ambayo yanamhusu Slaa peke yake ni kutoa maneno ya uchochezi Januari 5 katika viwanja vya NMC, Arusha, akiwa Katibu Mkuu wa Chadema.
Mashitaka mengine yanamhusu Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo, ambayo ni ya kutoa maneno ya uchochezi na kejeli dhidi ya Rais Jakaya Kikwete. Mengine ambayo yanawahusu Ndesamburo, Slaa na Samson Mwigamba ni ya kuchochea na kutaka kutorosha watu waliokuwa chini ya ulinzi Januari 5 kwenye viwanja vya NMC, Arusha.
Pia washitakiwa hao 19 kwa pamoja wanadaiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kusababisha taharuki kwa jamii. Baada ya kusomewa mashitaka hayo, mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Judith Kamala, washitakiwa kwa pamoja walikana mashitaka.
Kakolaki alidai mahakamani hapo kwamba, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba tarehe ya usikilizwaji wa awali wa kesi hiyo. Hakimu Kamala aliamua kesi hiyo ianze kusikilizwa Aprili 29.
Hata hivyo, wafuasi wa Chadema waliokuwa nje ya mahakama waliendelea kutoa maneno ya kejeli baada ya kusikia mashtaka mapya dhidi ya viongozi hao. Baadhi yao walisema mahakama inapaswa kutenda haki wakidai kuwa, mashitaka yamepindishwa na kutenganisha baadhi ya washitakiwa.
Lema alipotoka mahakamani baada ya kesi kuahirishwa, aliwatuliza wafuasi wa chama hicho kwa kuwaambia kuwa hata Mandela alifungwa kwa kupigania haki hivyo wasubiri uamuzi wa mahakama. Aliwasihi wafuasi wa Chadema kutawanyika na kwenda kwenye shughuli zao na warudi mahakamani hapo Aprili 29.
Viongozi hao wa Chadema walifanya maandamano Januari 5 licha ya Polisi kukataza kwa misingi ya kiusalama, lakini pia wafuasi wao wakataka kuvamia kituo kikuu cha Polisi kuwatoa viongozi waliokuwa wanashikiliwa. Katika ghasia hizo, watu watatu walipoterza maisha kwa kupigwa risasi na polisi akiwamo raia mmoja wa Kenya.
Source: Habari Leo