vioja vya makonda wa daladala jijini Dar

sunshine1

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
539
289
Hii nimeikuta mchuzi. Inachekesha ila ina ka ukweli ndani yake!


Mlokole: "Nyimbo gani mnapiga?!? Wekeni nyimbo za yesu.."Konda: "Vunga wewe, Yesu bado hajatoa album..."

********************************Abiria: "Kuna Kiti au unasema panda tu!?"Konda: "We taahira nini,hao wengine wamekaliandoo?! "

*******************************Abiria: "Embu punguzeni sauti ya redio..."Konda: "Sheria za nchi tu ziko za kutosha, tusikilize na zako!?"

*******************************Mmama: "Bwana ondoa gari joto sana!!"Konda: "Uctuzingue wewe,shuka upande fridge...."

******************************Konda: "Anti, kuna siti pale nyuma,ingia...." Anti: "Siwezi kaa siti za nyuma..."Konda: "Kwenda zako wewe, sio muendaji!!! Kwani za nyuma ziko nje ya gari?!"

******************************** Sister duu: "Konda unanibana bwana..."Konda: "Zinabanana ndizi haziongei, kama ulitaka kujiachia si ungekodi treni pekeyako!!!"

*******************************Sharobaro: "Kuna kiti?!kama hamna sipandi..."Konda: "Mpuuzi kweli, wa wapi wewe... Kama ulikuwa unaogopa kukosa kiti si ungebeba chako?
 
tumblr_kyf2dgeIQH1qat0kfo1_400.gif
 
konda ana mdomo mchafu sana huyo sidhani kama huwa anapiga mswaki
 
Back
Top Bottom