Vimimika vya mwili, zana mahiri za mvuto

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,845
http://www.luckymojo.com/rattle-viper-sperm-incense-salt.jpg
Inawezekana kabisa kuwa hii ikawa mada ya kushangaza mno kwako lakini ni kwakuwa hukuwahi kudhani wala kusikia juu ya hili jambo lakini at least ukiwa na mifano hai watu waliotekwa kimapenzi wakatekeka hata kufikia kusahau familia zao.

Dawa za mvuto wa mapenzi hazitengenezwi na vitu vya ajabu bali kwa sehemu kubwa vimimika toka mwilini mwa mtu na baadhi ya vimimika hivi hutumika pia kwenye kuleta laana na mikosi kwenye hayo hayo mahusiano ili mtu aachwe au aachike.

Vimimika hivi muhimu ni damu ya hedhi, manii mkono nk (manii tulishaijadili
Vingine ni mate , machozi , kinyesi , nywele za kichwani, nywele za sehemu za siri , kwapani na sehemu zinazoonekana , na kucha (rejea andiko la Aleister and his cohorts) bingwa wa mambo ya ndele na mvuto.

Kwenye ushirikina wa kiafrika na America na visiwa vya Cicily, damu ya hedhi hutumika kumwekea mwanaume kwenye chai au kahawa ambayo huleta kichocheo chanya cha mapenzi Ladha na hamu ya upendo kwenye ufahamu

Lakini vile vile kama damu ya hedhi ikikosekana pengine kutokana na kunyonyesha au kwa sababu zingine zozote basi mwanamke hutumia vaginal fluids(ute wa ukeni) baada ya kujichua wakati wa kipindi cha mwezi mkomavu. .huu ute wa ukeni ni mbadala wa damu ya hedhi.

Vivyo hivyo kinyesi na mkojo usio wa mimba kwa mchanganuo na mchanganyo wa dawa nyingine na kwa kutumia chakula hutengeza nuksi mikosi na balaa na kumfanya mtu awe na chuki kwa mwenzake.
1454929086049.jpg


Nisiwachoshe na post ndefu lakini jitahidini kulinda vimimika vyenu, ukiona mtu kashikwa tena vibaya hasa usikimbilie kumlaumu ujue kapatikana baadhi ya maeneo ya Tanga hata kutema mate ni ishu utafikiri ni kwasababu za kiafya kumbe watu wana yao.

Jihadhari na nyumba ndogo yako usikubali kula kitu alichokuandilia pekeyako kuleni wote na kama ni chai kunyweni wote.
 
kaka mshana kwakweli hapana, yote hii kutafuta laana tu, maana ukifanikiwa kumpumbaza mtu hao watakaohangaika nyuma yake kwakweli karma haitakuacha, dah!
 
Mwanamke ukishafikia hatua hiyo hata kuua unaua tu

kaka mshana kwakweli hapana, yote hii kutafuta laana tu, maana ukifanikiwa kumpumbaza mtu hao watakaohangaika nyuma yake kwakweli karma haitakuacha, dah!
Kuna watu ni majambazi acheni kabisa...kuna wanaume na akili wamekimbia ndoa na nyumba zao wakaacha kila kitu ukiwauliza kwanini wanakwambia hawajui au wanakuwa wakali kama pilipili
 
Na ile ya kuweka kinyango cha nyama ukeni kwa siku kadhaa kisha kumuandalia mpenzi (Kama tusiavyo mitaani) nayo imo kundi hiki?
 
Na ile ya kuweka kinyango cha nyama ukeni kwa siku kadhaa kisha kumuandalia mpenzi (Kama tusiavyo mitaani) nayo imo kundi hiki?
Haina ukweli kihivyo! Hiyo nyama huwekwa kwa dakika kadhaa na si siku kadhaa
 
Back
Top Bottom