Vijana Wasomi Wapewa Changamoto ya Kujiajiri Badala ya Kusubiria Kuajiriwa!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,503
113,616
Vijana wasomi kote nchini na haswa wahitimu wa vyuo vikuu, wamepewa changamoto ya kuutumia usomi wao kubaini fursa mbalimbali zilizopo kwa kujiajiri, badala ya kubweteka kwa kusubiria kuajiriwa rasmi au kuendelea kusotea kusaka ajira rasmi ambazo ni finyu kulinganisha na idadi ya wasomi.

Changamoto hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko, wakati wa Semina maalum ya Uhamasishaji vijana wasomi Kujiajiri, iliyofanyika ukumbi wa JK Nyerere, TanTrade, Kilwa RD, jijini Dar es Salaam, hivi karibuni.

Bibi Maleko, Tanzania inazo fursa nyingi za kujiajiri, ambapo watu kutoka nchi za wenzetu wanakuja kuzitumia, huku Watanzania tukibaki kama watazamaji, hivyo ni muhimu kwa vijana wasomi, wahitimu wa vyuo vikuu nchini, kuutumia usomi wao kubaini fursa na kuzichangamkia.

Bibi Maleko amesema, anashangazwa na idadi kubwa ya wahitimu wa vyuo vikuu wanaojitokeza kusaka ajira, na kutolea mfano ameshangaa kuona waombaji zaidi ya 3,000 wamejitokeza kufanya interview ya kazi kugombea nafasi 30 tuu za kazi, hivyo kati ya hao, watakaopata ajira ni watu 30 tuu na wale wengine 2, 970 wataendelea kusubiria ajira nyingine zitangazwe na kujikuta wakiendelea kubweteka kusotea ajira, wakati kuna fursa nyingi za wao kutengeneza ajira.

Bibi Maleko amesema, hakuna sababu kwa vijana wasomi waliohitimu vyuo vikuu, kubweteka kusubiria ajira rasmi wakati Tanzania umezungukwa na fursa nyingi za kujiajiri, hivyo kupata maisha bora kuliko hata kusubiria ajira na kutegemea mshahara ambao nao siku zote ni kiduchu tuu.

Kufuatia hali hii, Bibi Maleko, amesema kupitia TanTrade, kila kukifanyika usahili wa nafasi za ajira, Tan Trade itakuwa inaendesha semina elekezi za fursa za kujiajiri kwa vijana wasomi, kwa kuwatumia wakufunzi wa vitendo, wale wasomi vijana walioamua kujiajiri mara baada ya kuhitimu masomo yao, ili wasomi wapya wayatumie mafanikio ya wenzao kama hamasa ya kujiajiri, na kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

Wakizungumza kwenye semina hiyo, wasomi vijana waliojijiri kwa mafanikio makubwa, walitoa ushuhuda siri ya mafanikio yao, kwa kueleza jinsi walivyoanza kwa mwanzo mgumu, lakini sasa wanavuna mafanikio makubwa.

Akielezea mafanikio yake, mmoja wa wasomi vijana waliofanikiwa kujiajiri ni mwana dada ambaye ni mmiliki wa saloon ya Maznat, Bi. Maza Sinare, ameeleza yeye ni msomi wa sharia ngazi ya shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, baada ya kuhitimu, hakutafuta ajira bali alifungua saloon ya kuwapamba ma bibi harusi, hadi sasa amepata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuajiri wafanyakazi zaidi ya 20, ambapo ndoto yake sasa ni kutengeza bidhaa za urembo toka Tanzania zenye nembo ya Maznat.

Mwingine mwenye mafanikio ni Emelda Mwamanga mwenye kampuni ya Realim Entertainment ambayo ni wachapishaji wa jarida la Bang, amesema mwanzo aliajiriwa, kasha akaamua kuachana na ajira na kujiajiri katika fani ya uchapishaji wa jarida na kutoa ushauri kwa vijana, sasa amepata mafanikio hadi kujiona muda wote aliokaa kwenye ajira ilikuwa ni kupoteza muda!. Amewashauri vijana wasomi kuwa siri kubwa mafanikio ni kwanza ni kuwa na na ndoto ya unataka kufanya nini, na pili kujiamini kuwa unaweza, na tatu kukata shauri kuanza utekelezaji wa kutimiza ndoto yako.

Moja ya majukumu ya Tanzania Trade Development Authority (TanTrade) ni kuzibaini fursa mbalimbali za kibiashara na kuwawezesha Watannzania ikiwemo kuwajengea uwezo wa kuzichangamkia fursa hizo kujiletea maendeleo na maendeleo ya Taifa kwa ujumla. Bibi Maleko ameahidi TanTrade itaendelea kutoa fursa kwa watafuta ajira, kupata fursa za kusikiliza shuhuda za waliofaikiwa kwa kujiajiri ili iwe chachu na hamasa kwa wao kujiajiri ili kutengua bomu la ukosefu wa ajira kwa vijana kabla ya bomu hilo halijalipuka.

Source: Mimi mwenyewe nilikuwa eneo la tukio.

Paskali
 

Attachments

  • Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    494.9 KB · Views: 397
  • Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    543.4 KB · Views: 372
  • Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    458.2 KB · Views: 362
  • Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    373.4 KB · Views: 361
  • Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko.JPG
    367.5 KB · Views: 320
  • Mshiriki kutoka MaxCom wanaoendesha Mtandao wa Maxmalipo, akiwahamasisha vijana wasomi kubuni aj.JPG
    Mshiriki kutoka MaxCom wanaoendesha Mtandao wa Maxmalipo, akiwahamasisha vijana wasomi kubuni aj.JPG
    586.2 KB · Views: 313
  • Msomi Mmiliki wa Saloon ya Mharusi ya Maznat, Bibi Maza Sinare, mwenye shahada ya uzamili ya she.JPG
    Msomi Mmiliki wa Saloon ya Mharusi ya Maznat, Bibi Maza Sinare, mwenye shahada ya uzamili ya she.JPG
    363.7 KB · Views: 343
  • Msomi Mmiliki wa Saloon ya Mharusi ya Maznat, Bibi Maza Sinare, mwenye shahada ya uazamili ya sh.JPG
    Msomi Mmiliki wa Saloon ya Mharusi ya Maznat, Bibi Maza Sinare, mwenye shahada ya uazamili ya sh.JPG
    637.2 KB · Views: 206
  • DSC_0770.JPG
    DSC_0770.JPG
    549.5 KB · Views: 153
  • DSC_0787.JPG
    DSC_0787.JPG
    376.1 KB · Views: 142
  • DSC_0797.JPG
    DSC_0797.JPG
    500 KB · Views: 173
  • DSC_0796.JPG
    DSC_0796.JPG
    500 KB · Views: 179
Tatizo mtaji kujiajiri hata sio shida mabenki wanadai riba kubwa, tra usiseme yaani now ni times 2, kama unataka sehemu ya kufanyia biashara ulipe miezi sita na ulikuwa na mtaji wa 1.5 yaani mpaka hapo ushaisha hujafanya chochote bado hujatengeneza hiyi frame yenyewe at the end lazima ushindwe
 
Tatizo mtaji kujiajiri hata sio shida mabenki wanadai riba kubwa, tra usiseme yaani now ni times 2, kama unataka sehemu ya kufanyia biashara ulipe miezi sita na ulikuwa na mtaji wa 1.5 yaani mpaka hapo ushaisha hujafanya chochote bado hujatengeneza hiyi frame yenyewe at the end lazima ushindwe
Kushindwa ni negative mentality inayotegeneza negative energy, inayojenga negativity hivyo kuandaa mazingira ya kushindwa!.

Wahitimu wanapaswa kufunza kitu kinaitwa affirmatives, yaani positivity, kuwa positive, ukiwa positive, una create positive energy inayotoa positive power (the power of positive thinking), itakayofungua milango ya mafanikio!.

Poverty is just the attitude of mind, think small, unakuwa poor, think big, unakuwa rich!.

Paskali
 
Vijana wasomi kote nchini na haswa wahitimu wa vyuo vikuu, wamepewa changamoto ya kuutumia usomi wao kubaini fursa mbalimbali zilizopo kwa kujiajiri, badala ya kubweteka kwa kusubiria kuajiriwa rasmi au kuendelea kusotea kusaka ajira rasmi ambazo ni finyu kulinganisha na idadi ya wasomi.

Changamoto hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Trade Development Authority (TanTrade), Bibi Jacquline Mneney Maleko, wakati wa Semina maalum ya Uhamasishaji vijana wasomi Kujiajiri, iliyofanyika ukumbi wa JK Nyerere, TanTrade, Kilwa RD, jijini Dar es Salaam, hivi karibuni.

Yeye hapo TanTrade amejiajiri au ameajiriwa?

Vipi, watoto wake kuna aliyejiajiri hata mmoja?
 
Yeye hapo TanTrade amejiajiri au ameajiriwa?

Vipi, watoto wake kuna aliyejiajiri hata mmoja?
Yes kwa vile TanTrade ni kampuni ya mtu binafsi, hivyo yeye amejiajiri, na TanTrade ni mali yake!.
Nikienda tena pale next week, nitaulizia kuhusu watoto wake.

Paskali
 
Pasco nakuheahm sana lakn utamshawish VIP kijanq ajiajiri Kwa kamtaji ka laki. wakati messenger TRA anakunja nusu milioni?

Mbunge analambab posho ya hatari
 
Kusema wasomi wajiajiri ni ukwepaji wa majukumu wa serikali tuu. Serikali kazi yake ni kuinua uchumi ambao unaleta ajira kwa wananchi. Kama serikali kazi ya kuinua uchumi na kuleta ajira imewashinda, wawape hayo majukumu wengine.
 
Samahan! Hawa jamaa tan trade walitangaza kazi kitu kama mwezi wa kwanza ivi sasa naona kimya kingi mwenye habari kama waliita interview?
 
Lazima tukubali nafasi za ajira za kuajiriwa ni ndogo sana hasa Kulingana na wahitimu wanaomaliza vyuo mbalimbali ni wengi sana, lazima mkazo uwe kwenye kujiajiri.
 
Yes kwa vile TanTrade ni kampuni ya mtu binafsi, hivyo yeye amejiajiri, na TanTrade ni mali yake!.
Nikienda tena pale next week, nitaulizia kuhusu watoto wake.

Paskali

Paskal hebu weka statement yako sawa.
TanTrade sio kampuni ya mtu binafsi. Ni taasisi ya serikali na ipo chini ya wizara ya viwanda na biashara. Kwa hiyo ameajiriwa na serikali..
 
Mimi sitaki kusikia habari za kujiajiri kwa mtu ambaye ameajiriwa, nataka kusikia habar za kujiajia kwa mtu aliyejiajir siyo hao wati wanachukua mishahara kila mwenzi na posho kibao alafu anakwambia jiajiri,mbona yeye amefanyakazi kwa miaka 20 ameshindwa kujiajir unafikili kujiajir ni rahisi basi kila mtu angeacha kazi na kujiajir coz kazi ni utumwa siku zote,nataka habar za kujiajir kwa mtu aliyejiari na sio hao wanasiasa na maboss wa makampun na serkali
 
Yes kwa vile TanTrade ni kampuni ya mtu binafsi, hivyo yeye amejiajiri, na TanTrade ni mali yake!.
Nikienda tena pale next week, nitaulizia kuhusu watoto wake.

Paskali

Kaka Pascal, TanTrade ni mamlaka iliyo chini ya serikali bila shaka. Nisahihishwe tafadhali.
 
Kushindwa ni negative mentality inayotegeneza negative energy, inayojenga negativity hivyo kuandaa mazingira ya kushindwa!.

Wahitimu wanapaswa kufunza kitu kinaitwa affirmatives, yaani positivity, kuwa positive, ukiwa positive, una create positive energy inayotoa positive power (the power of positive thinking), itakayofungua milango ya mafanikio!.

Poverty is just the attitude of mind, think small, unakuwa poor, think big, unakuwa rich!.

Paskali

Mtaji basi wengine hawana kabisa namna ya kupata mtaji, unashauri nini kifanyike hapo?
 
Mtaji basi wengine hawana kabisa namna ya kupata mtaji, unashauri nini kifanyike hapo?
Mkuu Tamalisa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne!, 1. Watu, 2. Ardhi, 3. Siasa Safi 4. Uongozi Bora!. Fedha sio msingi bali ni matokeo tuu!.

Kitu muhimu cha kwanza ni iwepo nia ya dhati ya kufanya kitu, hiyo nia, itatengeneza nguvu inayoitwa "will", where threr is a will, there is a way!, sasa hiyo will ina powers ya kukupatia kila utakachohitaji ukiwemo mtaji!.

Paskali
 
Mkuu Tamalisa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne!, 1. Watu, 2. Ardhi, 3. Siasa Safi 4. Uongozi Bora!. Fedha sio msingi bali ni matokeo tuu!.

Kitu muhimu cha kwanza ni iwepo nia ya dhati ya kufanya kitu, hiyo nia, itatengeneza nguvu inayoitwa "will", where threr is a will, there is a way!, sasa hiyo will ina powers ya kukupatia kila utakachohitaji ukiwemo mtaji!.

Paskali


Hapana ndugu yangu bado wapo wengi wanashindwa tu, tambua kuna watu wana ndugu, jamaa na marafiki wenye uwezo mkubwa kimaisha lakini ni wabinafsi sana, hata ukiomba 50,000 tu utafute mahala pa kulima walau mchicha uanzie hapo hawakupi. Wengine ndugu, jamaa na marafiki zetu, wana mali kama ardhi zipo tu zinaota nyasi, ukiomba ukapande walau viazi vitamu kwa mwaka mmoja uanzie hapo hakubali, just roho mbaya tu.

Unakuta mzazi au mlezi ndo hivyo tena, unaweza sema nikaanze kubeba zege, bt unapata unsufficient kipato, hapohapo ule, uvae, ujitibu na pengine mzazi hajiwezi anategemea hapo hapo, ni shida.

Hivyo suala la kujiajiri ni zuri, ila wapo ambao wanatamani na hakuna namna ya kupata mtaji, wapo wanapewa mtaji bt ujeuri na kujifanya utozi wanashindwa, wapo wasiotaka kabisa hiyo kitu kwasababu zao binafsi.

Hivyo basi nikuombe wewe kama umejiajiri, au umeajiriwa uwe na support kwa wale wenye moyo wa kujiajiri, mtu akikuomba hata 100,000 aanze kwa kuuza mahindi, matunda, au chochote plz mpe. Kumbuka kwamba suala la kujiajiri ni zuri, lakini hatuwezi wote kuwa tumejiajiri lazima wawepo waajiriwa pia.

Sidhani kama wote tukijiajiri mambo yataenda sawa, huwezi kufungua kampuni wewe huyo huyo ukawa HR, ACCOUNTANT, CONSULT, SECRETARY, MFANYA USAFI, MLINZI. NK.

NB: kubwa zaidi ni support kwa wale wote wenye moyo wa kujiajiri.
 
Mkuu Tamalisa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne!, 1. Watu, 2. Ardhi, 3. Siasa Safi 4. Uongozi Bora!. Fedha sio msingi bali ni matokeo tuu!.

Kitu muhimu cha kwanza ni iwepo nia ya dhati ya kufanya kitu, hiyo nia, itatengeneza nguvu inayoitwa "will", where threr is a will, there is a way!, sasa hiyo will ina powers ya kukupatia kila utakachohitaji ukiwemo mtaji!.

Paskali

Hapana ndugu yangu bado wapo wengi wanashindwa tu, tambua kuna watu wana ndugu, jamaa na marafiki wenye uwezo mkubwa kimaisha lakini ni wabinafsi sana, hata ukiomba 50,000 tu utafute mahala pa kulima walau mchicha uanzie hapo hawakupi. Wengine ndugu, jamaa na marafiki zetu, wana mali kama ardhi zipo tu zinaota nyasi, ukiomba ukapande walau viazi vitamu kwa mwaka mmoja uanzie hapo hakubali, just roho mbaya tu.

Unakuta mzazi au mlezi ndo hivyo tena, unaweza sema nikaanze kubeba zege, bt unapata unsufficient kipato, hapohapo ule, uvae, ujitibu na pengine mzazi hajiwezi anategemea hapo hapo, ni shida.

Hivyo suala la kujiajiri ni zuri, ila wapo ambao wanatamani na hakuna namna ya kupata mtaji, wapo wanapewa mtaji bt ujeuri na kujifanya utozi wanashindwa, wapo wasiotaka kabisa hiyo kitu kwasababu zao binafsi.

Hivyo basi nikuombe wewe kama umejiajiri, au umeajiriwa uwe na support kwa wale wenye moyo wa kujiajiri, mtu akikuomba hata 100,000 aanze kwa kuuza mahindi, matunda, au chochote plz mpe. Kumbuka kwamba suala la kujiajiri ni zuri, lakini hatuwezi wote kuwa tumejiajiri lazima wawepo waajiriwa pia.

Sidhani kama wote tukijiajiri mambo yataenda sawa, huwezi kufungua kampuni wewe huyo huyo ukawa HR, ACCOUNTANT, CONSULT, SECRETARY, MFANYA USAFI, MLINZI. NK.

NB: kubwa zaidi ni support kwa wale wote wenye moyo wa kujiajiri.
 
Back
Top Bottom