Vijana sasa fumbua Macho,Mdomo,Ubongo....ili watoto wako wajivunie Tanzania yao!!

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Vijana wanchi hii yatakiwa sasa kufumbua macho na midomo na akili! ili tuweze kutetea maslahi ya nchi hii...Kutokana na hali tuliyonayo ambayo imesababishwa na Chama kilichopo madarakani CCM.....kwa kukumbatia mtandao wa ufisadi! na kusababisha kushuka kwa uchumi!!na hii ndicho chanzo kikubwa cha nchi hii kuwa nyuma kiuchumi wakati hili ali tuna kila mali asili hapa Tanzania!
Lakini kwa Tanzania imekuwa tofauti uku tukiwa na kila kitu tulichojaliwa na mwenyezi mungu sisi ndo tumewahodhi wala rushwa na sisi vijana tunabaki tukikenua kwa kushangilia CCM!!
Kwa ushabiki wa siasa usiokuwa na tija!
Vijana ingieni katika mapinduzi ya kisiasa tuikomboe nchi hii!!
CCM hakuna mahali itakusaidia hata kama ukiiramba miguu! siku ukiwasema wenye CCM wanakumwaga! kama hawa walivyo mwagwa kwa sababu ya kutaka kuwawajibisha!!nabado kwenye uchaguzi mkuu ndiyo tutaona vituko vingi!!
Vijana ndiyo rasli mali ya taifa hili kuweni wanamageuzi wa kweli tusitake kuwa kwenye vyama kwa ajili ya uroho wa madaraka tunatakiwa kulitumikia taifa hili kwa ajili ya vizazi vijavyo nanilazima uwe nje ya mfumo wa CCM!.
CCM imesha zeeka inataka mabadiliko makubwa ili iendane na wakati na mabadriko hayo nilazima uwasitaafishe watumishi wote wa serikali kitu ambacho si rahisi!!
Hivyo kuitoa CCM madarakani unaweza ukabadilisha mfumo wote maana hata baadhi ya watumishi wa serikali hawataki kukubali kama tupo kwenye mfumo wa vyama vingi mifano ni Idara ya Polisi,Mahakama,wakuu wa mikoa,wakuu wa wilaya!!hii nikutokana na mfumo uliopo!
Kijana badirika sasa hakuna jipya CCM!!!
 
Back
Top Bottom