Vijana Njooni CCM, ndoto zenu zitatimia

...mnataka kutufunza ujangili,ufisadi,kuuza unga na kupeana vibali sebuleni, chama chakavu kweli nyie....
 
Paul Makonda hivi ndoto gani tena au sikuelewi? Tangu tupate uhuru CCM ndio inatawala, ni juzi tu vimekuja hivi vyama vingine na kimsingi ni baada ya uhitaji kuwepo uhitaji utokanao na CCM kutotimiza ndoto. Asilimia kubwa ya maeneo yapo chini ya Ccm ajabu ndio yanatisha kwa ufukara, ccm wameua elimu yetu tutegemeayo vijana ambao ndio ndoto zetu zingetimia. Sisi hatuna wazazi viongozi kuturithisha uongozi ndoto zitimieje?? Sisi wengine dadazetu wana sura mbaya hawawezi kupendwa na viongozi japo watupe nafasi za upendeleo kama wakuu wa mikoa na wilaya, hizo ndoto zitatimiaje Makonda?? Acha dharau bwana wewe. Tumekusikia ukidai 300,000 hazikutoshi wakati sisi huku mtaani hiyo hata kwa mwaka ni ngumu na tunakadi zachama au unadhani ndoto zetu ni kuwauzia kadi za Ccm kipindi cha uchaguzi? Au unadhani ndoto zetu ni kuvaa tishet na kofia mnazotupa wakati wa uchaguzi??
 
Last edited by a moderator:
Wewe Paul Makonda Wewe hujui kitu, ni mzoa maganda tu. Umoja wa vijana wa ccm ni kwa ajili ya watoto wa vigogo wa chama na mafisadi. Mfano wewe mwenyewe ulivyoyumbishwa just because ya tofauti zako na mtoto wa kigogo!! Usivyokuwa na akili hao wote uliowataja hapo juu hakuna mtoto wa mlala hoi!

Hujazungumzia uchaguzi wa chipukizi jinsi vigogo wanavyotembeza rushwa ili watoto wao wachaguliwe kny uongozi! Kwa hiyo rushwa kny uchaguzi ccm ipo damuni kabisa. Watoto wao wanafundishwa rushwa tangu wakiwa kindergarten, unategemea utapata viongozi waadilifu ndani hicho chama.

Kuwaalika vijana kujiunga na ccm ni sawa na kuwaita kny njia ya jahanamu. Kwani mla rushwa/fisadi hana tofauti muuaji aliyekusudia zawadi yake ni kwenda motoni, na viongozi wote wa ccm pamoja na familia zao kwao ni motoni tu, kwani ni wafuasi wa SHETANI MWENYEWE KABISAA!! Hell!! Paul Makonda ningekuwa wewe nisingediriki kutetea upuuzi ambao upo bayana, kumbe na wewe upo kny payroll ya book 7 eh! Ndiyo maana umewehuka.

Pole mwaya!
 
Last edited by a moderator:
Kwa bahati mbaya wengi ya Vijana hawajui historia yangu na hivyo hujikuta katika mkanganyiko mkubwa wakiwa wanajaribu kujadiliana na mimi. Hoja yako ndugu yangu haiko sahihi, mimi si miongoni mwa "HIGH CLASS" au "PRIVELEDGED FEW" mimi ni mtoto wa masikini, niliyekulia kijijini kabisa Usukumani kwetu. Ila nataka ufahamu kuwa mafanikio yangu ya kimaisha, kiuchumi na kisiasa kunatokana na Chama Cha Mapinduzi..,malezi ya Mzee wangu Makamba, Jakaya, Kinana na wengineo yamenifikisha hapa nilipo.

Kuniambia kuwa sijawafikiria Vijana wa Vijijini katika post hii, nasema ni uelewa wa taratibu sana wa kile nilichokiandika, nikitaja Vijana waje kwenye CCM kwani ndiko kwenye fursa namaanisha Vijana wote na namaanisha fursa za aina zote, wala sibagui kuwa ni graduates tu ama vijana wa mjini pekee...jaribu kusoma na kuelewa kabla haujachangia.

Nitoe wito kwa Vijana wenzangu kuuona ukweli huu na kuufuata, ufike wakati Vijana wajiandae na waandaliwe kuwa Viongozi Bora wa Kizazi Chao.
Mtoa mada nakuelewa sana ila andiko lako lina upotoshaji mkubwa, sidhani ni ndoto zipi ambazo unataka zitimie kwa vijana waliokwisha KUKATA TAMAA na maisha yao. Sio kweli kuwa kila kijana anataka kuwa kiongozi ndani ya ccm, vijana wana mahitaji mengine zaidi ya uongozi, ndio maana najaribu kukueleza wewe unazungumzia THE PRIVILEGED FEW, tazama vijana WANAOCHUKUA MADARAKA ndani ya ccm ni wale wale WABARIKIWA WACHACHE huku wengine wakiwa wapambe na wabeba mikoba. Kwako ni katika wale wachache wenye hulka ya kujikomba kwa watawala wa sasa na kutimiza malengo yao na nyie kutokea kwenye njia hizo. Sio sawa vijana KUJIBANZA-BANZA kwa wakubwa na watoto wao ili watoke kama wewe. Nashukuru kwa kuwa mwungwana kwa kujibu "comments" kiungwana
 
Ukiamua kuwa mwanachama wa hiki chama, basi ni vyema uwe tayari kwa lolote wakati wowote na mahali popote.
 
Makonda hivi ndoto gani tena au sikuelewi? Tangu tupate uhuru CCM ndio inatawala, ni juzi tu vimekuja hivi vyama vingine na kimsingi ni baada ya uhitaji kuwepo uhitaji utokanao na CCM kutotimiza ndoto. Asilimia kubwa ya maeneo yapo chini ya Ccm ajabu ndio yanatisha kwa ufukara, ccm wameua elimu yetu tutegemeayo vijana ambao ndio ndoto zetu zingetimia. Sisi hatuna wazazi viongozi kuturithisha uongozi ndoto zitimieje?? Sisi wengine dadazetu wana sura mbaya hawawezi kupendwa na viongozi japo watupe nafasi za upendeleo kama wakuu wa mikoa na wilaya, hizo ndoto zitatimiaje Makonda?? Acha dharau bwana wewe. Tumekusikia ukidai 300,000 hazikutoshi wakati sisi huku mtaani hiyo hata kwa mwaka ni ngumu na tunakadi zachama au unadhani ndoto zetu ni kuwauzia kadi za Ccm kipindi cha uchaguzi? Au unadhani ndoto zetu ni kuvaa tishet na kofia mnazotupa wakati wa uchaguzi??
Nafikiri huyu Mhe. Mjumbe wa Bunge Maalum ana tatizo kwenye kuelezea na kufafanua NDOTO ZA VIJANA WA KITANZANIA. Vijana wa kitanzania wana ndoto nyingi zaidi ya uongozi lakini ZIMESHAZIKWA NA MIFUMO mibaya iliyoasisiwa na ccm. Tukatae tukubali tukiendelea na ccm basi TUKUBALI KUTAWALIWA NA WATOTO KUTOKA FAMILIA CHACHE BARIKIWA NCHI HII na hata kama tutaongozwa na vijana kutoka familia maskini kama ya huyu mtoa mada lakini bado tutakuwa tunatimiza mahitaji na matakwa ya WABARIKIWA WACHACHE ambao wamejibariki kwa rasilimali za UMMA. Lazima mtoa mada afanye utafiti kwanza kabla ya kuja kuwaambia vijana wahamie ccm, wakafanye nini au WAKAKUTE LIPI JIPYA?
 
Paul Makonda Haya tuambieni mlichotufanyia waTZ at least kupunguza umasikini?? hizi sera za bila vitendo mnawafanya vijana wazidi kuwachukia
 
Last edited by a moderator:
unateswa na makundi ya ccm ndo sababu ccm hao hao walisema umemwibia mjumbe mwenzio sim bungeni alafu ulivyo kajinga unatanguliza vyama na sera zenu hizo za viraka nawakati hili taifa chini ya uongozi huu wa ccm halina sera ya vijana na vijana nawe hili walitambua hata mbungeni huwezi lijengea hoja na kulisimamia wee kalia kupewa darasa tu na hirizi ukawange
 
Vijana wana kila sababu ya kukimblia CCM kwani:
- Vijana waoajiriwa ni 9,056,217 sawa na %80.6 ya vijana nguvu kazi yote ya vijana waliostahili kuajiriwa kwenye sekta rasmi na
isiyo rasmi.
- Katika 2011/2012 jumla ya ajira 250,678 zilipatikana
 
Mkuu kabla sijaja CCM, naomba unijibu maswali matatu tu
1. Ndoto hizo zitatimia lini?
2. CCM ina muda gani tangu iingie madarakani na kuongoza serikali?
3. Wazee wangapi (kwa asilimia) ndoto zao zimetimia tangu walipojiunga CCM wakati wakiwa vijana enzi hizo?

Nimeshaandaa picha ya passport size, ukinipa hayo majibu tu narudisha kadi ya ACT na naenda kukata kadi ya CCM katika ofisi utakayonielekeza
 
Ingefaa sana iwapo ungeainisha mafanikio ya hao "vijana" uliowatolea mfano kuwa "ndoto zao zimetimia" ili tufahamu walikuwa na ndoto gani (zaidi ya kupata vyeo / tu).

Kwa mafanikio, ninamaaisha kwa jamii nzima ya waTanzania kuwaletea maisha bora.

Iwapo unachokisema kwenye bandiko lako ni kuwavutia tu vijana waje "kupiga hela" etc., kwangu mimi ninaona ni propaganda "hasi" kwa chama chenu.

Ninashauri ungehamasisha vijana wa Tanzania (ukiwa mwenzao) wafanye kazi popote walipo kwa juhudi na maarifa ili kujiletea maendeleo yao na jamii zao, mwishowe nchi nzima.

Ni bahati mbaya sana kwamba vijana wengi siku hizi mnadhani vyama vitaleta maendeleo yoyote kwa taifa. Ni bahati mbaya zaidi kuwa vijana wenyewe ndiyo mnaojipambanua kuwa na elimu. Sasa wasio na elimu sijui ndiyo wakoje. Loh!

Tafadhali ainisha "ndoto zilizotimia" sambamba na majina ili vijana wenzio wafahamu ulichoandika badala ya hii "who's who", waambie "who done what".

Ni ushauri wangu kwako na vijana wengine. Jaribuni kufikiria zaidi ya vyama.

Kama mpaka leo haujajua mafanikio ambayo tayari vijana hao niliowataja wameyafikia katika umri wao kisiasa basi naomba ukubali kuwa uko mbali sana na habari za kisiasa na matukio yake, na sidhani kama hata uwepo wako hapa kwenye jukwaa la siasa la jamiiforums kuna maana yeyote.

Miongoni mwa vijana waliopokea tuzo ya wanasiasa bora barani Afrika ni pamoja na January Makamba, lakin pia ni miongoni mwa manaibu waziri vijana ambao wameendelea kufanya vizuri katika Wizara zao lakini pia alikuwa ni Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi, katibu wa Idara ya SUKI ya CCM, na bado ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama..,hizo nafasi zote ni za juu mno kimaamuzi ndani ya Chama na Nchi. Lakini hilo la tuzo linampa sifa ya Kimataifa kuwa miongoni wa Vijana watatu wanaofanya siasa bora barani Africa January ni wa Kwanza wao. Katika Chadema sio tu vijana bali hata wazee wao hakuna hata aliyepewa tuzo ya kuwa kiongozi bora wa Mtaa achilia mbali tuzo za Kitaifa ama za kitaifa.

Ama Nape na Jerry inafahamika wazi kuwa ukitaja majina hayo hasa NAPE kila kona ya Tanzania watakuambia ni nani, ni hiyo kisiasa ina maana kubwa ikiwa unafahamu. Wote ni wajumbe wa kamati kuu ya Chama, wajumbe wa halmashauri kuu ya Taifa na kwa Nape ni Katibu wa Idara ya Itikadi na uenezi na alishawahi kuwa DC wa masasi, hali ya kuwa Jerry ni Mjumbe wa Baraza kuu la UVCCM Taifa pia ni meya wa Manispaa ya Ilala.

Niambie kuwa hayo sio mafanikio wakiwa na umri huo. Wote niliowataja hakuna aliyetimiza miaka 40, January 39 Nape 37 na Jerry 29. Nitajie mafanikio ya hata mwanasiasa mmoja wa Chadema ama chama kingine cha upinzani hapa nchini ambae hata anakaribia robo ya mafanikio hayo..?

Karibu CCM na kazi inaendelea....!!!
 
CCM ndio jibu. Tumuombee uzima Mheshimiwa Lowassa aweze kugombea na kushinda mbio za urais ili kumkomboa mtanzania kutoka katika umasikini.Kidumu!
 
Makonda hakika leo umeniharibia siku humu JF!kuitetea CCM kwa sasa yabidi uwe na akili za ukichaa!kuwataja akina jerry,nape,january n.k hujakosea ila ulichosahau ni kudhania vijana wote wa kitanzania tuna majina ya ukoo yaani kawawa,msekwa,msuya,malechela,makamba,nnauye n.k.Pole sana kwa hilo ila tambua wengine tumezaliwa na wakulima wa jembe la mkono ambao tumejitutumua kila namna lakini wapi.Nimeambiwa siku hizi chama ni cha wanasiasa na wafanyabiashara(mafisadi) na si cha wakulima na wafanyakazi tena.No problem endeleeni kula maisha huku mkila mafungu manono kwenye bunge la katiba na kuishia kuzomea huku walimu wanapiga miayo na danadana za madeni yao eti serikali haina pesa!Mwisho hongera kwa kuzaliwa kwenye ukoo wa makonda.
 
Daaa ni heri NIFE NIZIKWE KABISA, kuliko nijiunge na hiki chama{CCM} ambacho kwa takribani miaka 52 ya uhuru, lakn shangaz yangu bado anajifungulia njia, wtt wetu bdo wanakaa chn huko mashuleni, alaf nikupe somo la bure kuwa si kila anayejiunga na siasa anataka uongozi wengne tuko chadema tukiamin ndio chama kitakachotukomboa vijana kutoka kwenye lindi la ukosefu wa ajira na hatuwez kuja ccm kwani ndio chanzo cha tatizo letu kwa mfano hebu tazama jinsi walivyoua viwanda vyetu vya ndani heb tazama wanavyogawa ardhi yetu kwa wageni.? NAICHUKIA CCM KULIKO SHETANI.
 
Jamani ni kweli... vijana njooni mtimize ndoto zenu za kuwa na fani mbali mbali:
1. Ukitaka kuwa mwanajeshi binafsi
2. Ukitaka uendeleze kipaji cha matanuzi mijini...
 

Attachments

  • CCM-Kapuya na Dokii.jpg
    CCM-Kapuya na Dokii.jpg
    12.9 KB · Views: 148
mjinga mjibu kwa kiasi cha ujinga wake....kwani mtoto wa mwanasiasa anakuwa mwansiasa kwa hiyari au analazimika tu.?

Kwa hiyo godfrey mgimwa kagombea kalenga kwa hiyari yake?unaweza kwenda kuchukua fomu huku una majonzi ya msiba wa baba?2015 asingegombea huku hata machungu ya msiba yameisha?ONLY IN CCM KWENYE MAMBO YA KIJINGA YASIYO NA KIKOMO.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom