Vigogo watatu NEMC kuburuzwa Takukuru

singidadodoma

JF-Expert Member
Nov 11, 2013
4,394
1,531
SAKATA la maofisa watatu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), waliosimamishwa kazi kwa tuhuma ya kukiuka miiko yao ya kazi, limechukua sura mpya, baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba, kuagiza wafikishwe mbele ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Pamoja na hayo, Waziri huyo amemsimamisha kazi aliyekuwa mwanasheria wa baraza hilo, John Mnyele kwa matumizi mabaya ya ofisi.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, alisema tayari amemwagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, kuwasilisha mashtaka yanayowakabili maofisa hao watatu Takukuru kwa ajili ya uchunguzi na hatua zaidi, ikiwemo kufikishwa mahakamani.

Maofisa waliosimamishwa kazi kutokana na udhaifu huo ni pamoja na Ofisa Mazingira Mwandamizi Dk Eladius Makene, Mwanasheria Daraja la II Wakili Heche Suguta Manchare ; na Ofisa Mazingira Boniface Benedict Kyaruzi. Wanatuhumiwa kukiuka miiko ya kazi yao katika kusimamia kiwanda cha kusindika minofu ya punda kilichopo mkoani Dodoma.

Pamoja na maofisa hao, pia Mwanasheria Mnyele, anayetuhumiwa kuingia mkataba na Mchungaji Getrude Rwakatare wa kuondoa kesi mahakamani kwa niaba ya NEMC bila kuijulisha ofisi, naye anachunguzwa na taasisi hiyo ya rushwa.Mama Rwakatare kwa sasa ana kesi mahakamani dhidi ya baraza hilo ya kupinga kubomolewa kwa nyumba yake, inayodaiwa kujengwa mahali pasiporuhusiwa.

Kiwanda hicho cha minofu ya Punda cha China, kilianza kazi hiyo rasmi mwaka 2012 huko Dodoma ambapo pamoja na kuchinja, pia huuza nyama hiyo nje ya nchi, hususan China.
Kiwanda hicho kilipatiwa vibali vyote, ikiwemo cha Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA) na cha Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi cha kuchinjia.

Pia, kilikuwa na vibali vingine vya Manispaa. Hata hivyo, hakikuwa na kibali cha masuala ya mazingira kutoka NEMC.Katika ukaguzi uliofanywa siku za nyuma na Baraza hilo, ilibainika kuwa kiwanda hicho hakina kibali hicho cha mazingira, lakini pia kilikuwa kikilalamikiwa na wananchi wanaokizunguka kutokana na kutofuata taratibu za utunzaji wa mazingira.NEMC ilibaini kuwa kiwanda hicho, hakikuwa na mfumo wa majitaka, lakini pia kilikuwa kikichoma mabaki yanayotumika kuchinjia ndani ya kiwanda hicho na moshi wake kusambaa maeneo yanayokizunguka.

Kutokana na makosa hayo, baraza hilo lilikifungia kiwanda hicho kama adhabu na kukilipisha faini ya Sh milioni 240.Juzi Waziri January pamoja na kuwasimamisha maofisa hao watatu kwa kukiuka miiko yao ya kazi, pia aliagiza Mkurugenzi Mkuu wa baraza hilo, Mhandisi Bonaventura Baya, apewe barua ya onyo kali na la mwisho kwa tuhuma za udhaifu katika usimamizi wa watumishi wa baraza hilo, hivyo kusababisha malalamiko mengi kuhusu utendaji wa baraza hilo
 
Hivi serikali inata hawa wachina waendelee kuchinja punda? Maana punda ni wanyama walio wachache sana iko hatari wakapotea wote? Lakini si hivyo hawa wachina wamekuwa hawajari uharibifu wa mazingira wanaoufanya,wananchi wengi tunaamini mh Heche alifanya kazi nzuri sana. Kinachofanya asimamishwe ni nini? Tunapata hofu kwa hawa watetezi wa wanyonge kunyamazishwa sauti zao
 
Kwa hili serikali yote ya jpm imejitia doa lisilofutika yaani mtu anafanya kazi kuweka maslahi ya nchi mbele lakini anatokea tuu mototo mmoja na kusema vyote ni kazi bure inasikitisha inauma sana
 
We unajua NEMC walifanya misconduct ipi baada ya kufunga machinjio ya punda. Unajua HECHE anahusika vipi na hili swala? Unajua kama Hawa NEMC walikuwa wanatumia media mchana wakati Wa kufunga viwanda ili waonekane majembe? Unajua usiku kamera zikizimwa walikuwa wanafanya nini? Mbona walikuwa hawaiti media wakati wanafungulia viwanda walivyovifungia? Unajua mirungura wewe? Unajua waziri kapitia ushahidi UPI mpaka kufanya maamuzi haya?
扫描_20150814 (2).png
扫描_20150814 (3).png
扫描_20150814 (4).png
Humu nimeattach barua ya NEMC kwenda HUACHENG INTERNATIONAL LTD ya kufunga kiwanda( emergency stop order) Naomba tuisome wote.
1.kosa namba moja huwacheng hawakuwa wamefanya environmental impact audit/assessment so hawakuwa na cheti cha NEMC cha mazingira. Kiuhalisia hili ni kosa lakini mbigu ilikuwa haijaangushwa linarekebishika kwani mwekezaji hakupata mwongozo mzuri awali.
2.makosa yanayofatia yote yanahusiana na kuchafua mazingira kama kutokuwa na waste water plant, improper management of of solid wastes na kuchoma taka kiholela.
Haya yote ni makosa na mwekezaji alalamiki Kwa nini alifungiwa. Ishu hapo ni fine ya millioni 240 kushuka mpaka millioni 20. Unajua nini kilifanyika gizani?
Kumbukeni haya yalitokea tarehe 14 Augustus 2014. Leo ni lini? Unajua mwekezaji amedevelop vipi kiwanda mpaka leo but akawa anapigwa danadana kupewa certificate to date? Mnajua kama mwekezaji hajafanya shortcut katika kupata vibari kutoka mamlaka yoyote? Mnajua wizara ya Mifugo na ofisi ya mkuu Wa mkoa Wa Dodoma waliwaandikia NEMC barua Mara ngapi Kwa niaba ya mwekezaji?
IJUE HUWACHENG INTERNATIONAL KWA UFUPI
Hii kampuni ilikuwa incorporated mwaka 2014 na msajiri Wa makampuni. Mwaka huohuo wakapata kwanza leseni ya constructing, Insuring, financing and own premices kutoka EPZA. Baadae tena mwaka huohuo wakapewa licence ya kufungua kiwanda cha kuchakata Ngozi na kuanzisha machinjio kutoka haohao EPZA. Wakati huohuo Huwacheng waliandika barua wizara ya Mifugo kuomba kibali cha kuchinja Punda na barua ilijibiwa mwezi Wa tano 2015 kuwa wamepewa kibari cha muda Wa mwaka mmoja(provisional) huku wakijaribu kufatilia how sustainable will the project be kwani Kwa Tanzania ilikuwa ni jambo jipya ingawa Kenya Nigeria nk wanafanya hii biashara.
 
Hebu hili la nyama ya punda serekali ione aibu basi.. Kwa hiyo wanataka punda waendelee kuchinjwa dodoma..
 
Punda ni kama nguruwe tu. Unataka leo nikitaka kuchinja Punda niexport nitakuwa nakosea. We hujui kuna watanzania wana bucha ya Punda mvumi Dodoma na wanajia vyao saafi na bwana Afya anaenda kukagua nyama.
Hizo bucha mvumi hakuna tengua kauli yako tafadhali.
 
Back
Top Bottom