Sio habari tena kwamba mbio zauraisi 2015 zilianza 2004 na labda nyuma ya hapo. Kwa tuliopiga kura yakumchagua rais wa 2005/10/2010/15 huenda pia tuliamua juu ya rais wa2015/2020.
Leo hii vigezo vitakavyoamua rais ajaye huenda vimeimarika zaidi na kutoa changamoto kubwa zaidi kwa nchi, wagombea, wapiga kura na majirani zetu. Sehemu hii ya kwanza nitajadili machache.
Sehemu ya pili, tatu na nne nitakamilisha.
Dini
Pamoja na kuwa Katiba yetuinatupa uhuru wa kuabudu na kuamini mungu umtakaye maadamu haiingilii uhuru wa mtu mwingine lakini nguvu ya dini hizi mbili, yaani Uislamu na Ukristu si ya kubeza. Leo hii ni dhahiri kwamba kuna udini Tanzania (dini kama mojawapo yavigezo vinavyompa sifa mtu na haki ya kupata vile ambayo asiye wa dini husika hapati, iwe kwa uwazi au kwa kificho).
Hali hii imejitokeza na inaimarika katika mfumo rasmi (wa kisheria na kitaratibu kama katika elimu, biashara na ajira) na katika mfumo usio rasmi (mashindano ya kidini, katika michezo, vijiwe na maongezi ya mtu na mtu). Katika mfumo usio rasmi ni sifa kwa muislamu na jambo la kujivunia kuwa na kiongozi au mkuu wa kitengo Fulani muislamu, halikadharika kwa mkristo ni sifa na jambo la kujivunia kuwa na mkristo kiongozi au mkuu wa kitengo Fulani mkristu.
Na kinyume chake ni jambo baya kuongozwa na mtu wa dini isiyo yako. Wasomi na viongozi kadhaa wa umma kwa unafiki wamelibeza hili mbele ya umma kwa muda mrefu sasa. Ni Mh. Rais Kikwete tu aliyelieleza hili kwa ujasiri mbele ya umma katika hotuba yake kwa wabunge wa bunge la JMT, lakini pia alibezwa na wengi, hata viongozi wa dini ambao kwa siri wanaliona lakini kwa unafiki wao wanashindwa kulisemea. Raisi wa kwanza wa nchi yetu alilaumiwa, na anaendelea kulaumiwa sana na jamii ya kiislamu kwa kuukandamiza uislamu Tanzania na kuujenga na kuuimarisha ukristu (ukatoliki?). Waislamu wana sababu wanazozitoa.
Nitatoa mifano michache katika hili, tumeshuhudia sana wakati wa mazimisho ya miaka 50 ya uhuru kuwa wapigania uhuru wengi na hasa waislamu hawakuenziwa na utawala wa mwalimu Nyerere (je tatizo ni dini yao?), pia kuundwa kwa BAKWATA kuwa haikuwa ridhaa ya waislamu bali malengo ya Mwalimu kuunda chombo cha kugandamiza uislamu na harakati za uislamu kujitanua, nafasi za ajira na uongozi. Katika elimu pia, fuatilia madajiliano baada ya matakeo ya kidato cha nne yaliyopita na sakata la Ndanda Sekondari kwa uchache kwa siku za jirani.
Rais Mwinyi naye katika utawala wake alilaumiwa sana na wakristu kwa kujenga uislamu Tanzania. Maaskofu na hasa wakatoliki (TEC) walijitokeza wazi kuvutana na serikali katika mambo kadhaa. Wakristo waliona kuna kitu kinapungua kwa kuwa na Rais muislamu, na hasa wavaa kanzu wengi kuonekana wakitembelea Ikulu na shamrashamra za kiislamu kuwa na mh. Rais mara nyingi. Hamu ikawa ni kuwa na mabadiliko katika uchaguzi wa mwaka 1995.
Tunatambua kwa hakika harakati kadhaa za mihadhara ya uislamu na ukristu ilivyoshamiri katika awamu hii. Kelele za lawama kutoka kwa maaskofu zilipungua sana katika wakati wa Mkapa na nyingi zikitokea katika uislamu. Lakini bado alihusishwa sana na ukristu, katika teuzi zake kwa wakuu wa idara nyeti za umma kama Mahakama, TISS, na Jeshi. Wakristo waliona ile kuwa na rais asiye muislamu ni jambo jema kwao bila ya hasa nini anakifanya.
Baada ya enzi ya Mkapa, kaingia Kikwete, kwa mbwembwe na sifa nyingi kutoka pande zote za dini hizi. Waislamu wakiona ni wakati sasa wakukamilisha ajenda zao nyingi kama kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi na kuongeza idadi ya wateule waislam. Mambo ambayo waislamu wengi wanaona leo bado hayajatimia na wangependa yasimamiwe na awamu ijayo ya 2015/20.
Na wakristu nao wakaona Kikwete aliyesoma shule za kikristu na mwenye msimamo usiojulikana juu ya u-islamu atafaa kwa sasa kwani ndio chaguo lilokuwepo na namna pekee ilikuwani kumuunganisha na Mungu wa wakristu kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.
Katika miakahii 7 tumeshuhudia na tunaendelea kushuhudia mivutano na minyukano mikali ya u-dini. Ndani ya mfumo wa elimu na hasa makao makuu, ofisi ya utumishi, TISS, wizara ya fedha, mashirika ya umma, wakala za serikali, mifuko ya hifadhi yajamii, uafisa katika idara nyingi za halmashauri.
Ni vigumu kuamini mambo haya, lakini pia panahitajika vigezo gani ili kuyaamini haya?Sasa tunapoelekea uchaguzi wa 2015 kigezo (variable) cha dini kitakuwa na nguvu kubwa. Wakristo watapenda rais ajaye awe mkristo kama sifa kuu ya kumuunga mkono (tunatambua nguvu ya maaskofu wa makanisa mbalimbali ndani ya Tanzania).
Huyu mkristo atakabidhiwa (ameshakabidhiwa) jukumu la kusimamia nchi isiyo na mahangaiko ya udini (kuachana na mahakama ya kadhi), kurudisha taasisi za kikristu mikononi mwa wenyewe, kuteua wakristu katika taasi muhimu za umma na kurekebisha na ama kuzima kabisa hisia za udini katika makao makuu ya Wizara nyingi hasa Elimu, fedha na ofisi ya Makamu wa Rais na Utumishi Makao Makuu. Rais mkristo atatakiwa kusukuma mbele ajenda ya kufadhili taasisi za kikristu kwa mlango wa ruzuku.
Mfumo huu ni vigumu kwa waislamu kupambana nao kwani taasisi nyingi za afya na elimu ni za kikristu. Mgombea u-Rais mkristu ndio litakuwa pia chaguo la nchi za magharibi ambazo harakati dhidi ya u-islam ni kati ya ajenda kuu ya kiuchumi na kijamii. Hili litaongezwa nguvu na mapambano ya ugaidi kwa sasa, mambo ambayo Mkapa aliyasimamia kwa nguvu na misingi yake kushindwa kuvunjwa na Kikwete.
Ufadhili wa nchi za magharibi kwa TISS ulijikita zaidi katika mapambano dhidi ya ugaidi. Pamoja na kutokuwa na uhakika wa takwimu zetu lakini ukiachia ukanda wa pwani (Dar, Lindi, Mtwara, Tanga) nabaadhia maeneo machache ya bara (kama Tabora, Kigoma na sehemu chache za mkoa wa Kagera na Iringa) sehemu zinazosalia kwa Tanzania Bara ni ama Wakristu, kwa uchache sana waislamu na/au wenye dini nyingine (lakini si uislamu).
Pia ndani ya ukanda wa Pwani ukristu umeenea sana na idadi ya wakristu kuongezeka. Pia wana ushawishi mkubwa wa kitamaduni (umagharibi) kuliko uarabu (tazama miji ya dar, tanga),. Wakristu hawa ni wapinzani wa uislamu kwani kwa mtazamo wao u-islamu ni si dini sahihina (wenye mtazamo mkali uislamu=ushetani). Kundi hili la wakristu watakuwatayari kumpigia kura rais yeyote asiye mu-islamu kwani kufanya hivyo ni sehemuya kuimarisha uinjilishaji.
Hapa kigezo cha usafi kitashindwa dhidi ya umoja. Ajenda ya ufisadi haitakuwa na nguvu tena. Mgombea u-Rais muislamu asiye na msimamo mkali na ambaye hajulikani vizuri huku bara anaweza kupewa nafasi kiasi ndani ya jumuia ya kikristu lakini ni wakristu wachache wataziba masikio yao wakati wa kampeni kama kauli hii itatumika waislamu kuongoza nchi kwa awamu mbili, yaani miaka 20 . kwa hakika ataungwa mkono kwa nguvu zote na waislamu hata kama hana sifa, sifa kuu ya kuwa mu-islamu itakuwa kigezo kikuu. Huyu ndiye atakayebeba jukumu la kukamilisha uwepo wa mahakama ya kadhi na vipaumbele kadhaa kwa waislamu.
Waislamu watapata nafasi ya kutafakari upya ndoto ya kuanzisha mahakama ya kadhi. Karata ya waislamu wa Tanzania kumpata raisi muislamu awamu ya tano itawabidi kuungana na wazanzibari kupigana kupata Rais wa Muungano mzanzibari. Kwani hilo litawahakikishia rais muislamu (hata kama ni mzanzibari).
Kama hili likifanyika (limeanza kufanyika?) changamoto kuu ni namna ya kumuuza kwa wabara, ambao ni wapiga kura wengi na ambao kwa hakika bado hawaoni mzanzibari anayefaa kwa sasa kuwaongoza. Hili la changamoto za kumnadi mgombea uraisi mzanzibari nitalieleza vizuri katika sehemu zijazo.
Hivyo basi vyama vya siasa, wagombea urais na wapambe wao wanalazimika kukiangalia vizuri kigezo hiki chadini na kuchagua maneno mazuri sana ya kutumia kuwauza watu wao. Ni wakati muafaka wa think tanks za watu hawa kufanya kazi hasa juu ya hili ikiwemo kupata ushauri wa wataalmu (Consultants) wenye weledi.
Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx tuonane maranyingine xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Leo hii vigezo vitakavyoamua rais ajaye huenda vimeimarika zaidi na kutoa changamoto kubwa zaidi kwa nchi, wagombea, wapiga kura na majirani zetu. Sehemu hii ya kwanza nitajadili machache.
Sehemu ya pili, tatu na nne nitakamilisha.
Dini
Pamoja na kuwa Katiba yetuinatupa uhuru wa kuabudu na kuamini mungu umtakaye maadamu haiingilii uhuru wa mtu mwingine lakini nguvu ya dini hizi mbili, yaani Uislamu na Ukristu si ya kubeza. Leo hii ni dhahiri kwamba kuna udini Tanzania (dini kama mojawapo yavigezo vinavyompa sifa mtu na haki ya kupata vile ambayo asiye wa dini husika hapati, iwe kwa uwazi au kwa kificho).
Hali hii imejitokeza na inaimarika katika mfumo rasmi (wa kisheria na kitaratibu kama katika elimu, biashara na ajira) na katika mfumo usio rasmi (mashindano ya kidini, katika michezo, vijiwe na maongezi ya mtu na mtu). Katika mfumo usio rasmi ni sifa kwa muislamu na jambo la kujivunia kuwa na kiongozi au mkuu wa kitengo Fulani muislamu, halikadharika kwa mkristo ni sifa na jambo la kujivunia kuwa na mkristo kiongozi au mkuu wa kitengo Fulani mkristu.
Na kinyume chake ni jambo baya kuongozwa na mtu wa dini isiyo yako. Wasomi na viongozi kadhaa wa umma kwa unafiki wamelibeza hili mbele ya umma kwa muda mrefu sasa. Ni Mh. Rais Kikwete tu aliyelieleza hili kwa ujasiri mbele ya umma katika hotuba yake kwa wabunge wa bunge la JMT, lakini pia alibezwa na wengi, hata viongozi wa dini ambao kwa siri wanaliona lakini kwa unafiki wao wanashindwa kulisemea. Raisi wa kwanza wa nchi yetu alilaumiwa, na anaendelea kulaumiwa sana na jamii ya kiislamu kwa kuukandamiza uislamu Tanzania na kuujenga na kuuimarisha ukristu (ukatoliki?). Waislamu wana sababu wanazozitoa.
Nitatoa mifano michache katika hili, tumeshuhudia sana wakati wa mazimisho ya miaka 50 ya uhuru kuwa wapigania uhuru wengi na hasa waislamu hawakuenziwa na utawala wa mwalimu Nyerere (je tatizo ni dini yao?), pia kuundwa kwa BAKWATA kuwa haikuwa ridhaa ya waislamu bali malengo ya Mwalimu kuunda chombo cha kugandamiza uislamu na harakati za uislamu kujitanua, nafasi za ajira na uongozi. Katika elimu pia, fuatilia madajiliano baada ya matakeo ya kidato cha nne yaliyopita na sakata la Ndanda Sekondari kwa uchache kwa siku za jirani.
Rais Mwinyi naye katika utawala wake alilaumiwa sana na wakristu kwa kujenga uislamu Tanzania. Maaskofu na hasa wakatoliki (TEC) walijitokeza wazi kuvutana na serikali katika mambo kadhaa. Wakristo waliona kuna kitu kinapungua kwa kuwa na Rais muislamu, na hasa wavaa kanzu wengi kuonekana wakitembelea Ikulu na shamrashamra za kiislamu kuwa na mh. Rais mara nyingi. Hamu ikawa ni kuwa na mabadiliko katika uchaguzi wa mwaka 1995.
Tunatambua kwa hakika harakati kadhaa za mihadhara ya uislamu na ukristu ilivyoshamiri katika awamu hii. Kelele za lawama kutoka kwa maaskofu zilipungua sana katika wakati wa Mkapa na nyingi zikitokea katika uislamu. Lakini bado alihusishwa sana na ukristu, katika teuzi zake kwa wakuu wa idara nyeti za umma kama Mahakama, TISS, na Jeshi. Wakristo waliona ile kuwa na rais asiye muislamu ni jambo jema kwao bila ya hasa nini anakifanya.
Baada ya enzi ya Mkapa, kaingia Kikwete, kwa mbwembwe na sifa nyingi kutoka pande zote za dini hizi. Waislamu wakiona ni wakati sasa wakukamilisha ajenda zao nyingi kama kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi na kuongeza idadi ya wateule waislam. Mambo ambayo waislamu wengi wanaona leo bado hayajatimia na wangependa yasimamiwe na awamu ijayo ya 2015/20.
Na wakristu nao wakaona Kikwete aliyesoma shule za kikristu na mwenye msimamo usiojulikana juu ya u-islamu atafaa kwa sasa kwani ndio chaguo lilokuwepo na namna pekee ilikuwani kumuunganisha na Mungu wa wakristu kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.
Katika miakahii 7 tumeshuhudia na tunaendelea kushuhudia mivutano na minyukano mikali ya u-dini. Ndani ya mfumo wa elimu na hasa makao makuu, ofisi ya utumishi, TISS, wizara ya fedha, mashirika ya umma, wakala za serikali, mifuko ya hifadhi yajamii, uafisa katika idara nyingi za halmashauri.
Ni vigumu kuamini mambo haya, lakini pia panahitajika vigezo gani ili kuyaamini haya?Sasa tunapoelekea uchaguzi wa 2015 kigezo (variable) cha dini kitakuwa na nguvu kubwa. Wakristo watapenda rais ajaye awe mkristo kama sifa kuu ya kumuunga mkono (tunatambua nguvu ya maaskofu wa makanisa mbalimbali ndani ya Tanzania).
Huyu mkristo atakabidhiwa (ameshakabidhiwa) jukumu la kusimamia nchi isiyo na mahangaiko ya udini (kuachana na mahakama ya kadhi), kurudisha taasisi za kikristu mikononi mwa wenyewe, kuteua wakristu katika taasi muhimu za umma na kurekebisha na ama kuzima kabisa hisia za udini katika makao makuu ya Wizara nyingi hasa Elimu, fedha na ofisi ya Makamu wa Rais na Utumishi Makao Makuu. Rais mkristo atatakiwa kusukuma mbele ajenda ya kufadhili taasisi za kikristu kwa mlango wa ruzuku.
Mfumo huu ni vigumu kwa waislamu kupambana nao kwani taasisi nyingi za afya na elimu ni za kikristu. Mgombea u-Rais mkristu ndio litakuwa pia chaguo la nchi za magharibi ambazo harakati dhidi ya u-islam ni kati ya ajenda kuu ya kiuchumi na kijamii. Hili litaongezwa nguvu na mapambano ya ugaidi kwa sasa, mambo ambayo Mkapa aliyasimamia kwa nguvu na misingi yake kushindwa kuvunjwa na Kikwete.
Ufadhili wa nchi za magharibi kwa TISS ulijikita zaidi katika mapambano dhidi ya ugaidi. Pamoja na kutokuwa na uhakika wa takwimu zetu lakini ukiachia ukanda wa pwani (Dar, Lindi, Mtwara, Tanga) nabaadhia maeneo machache ya bara (kama Tabora, Kigoma na sehemu chache za mkoa wa Kagera na Iringa) sehemu zinazosalia kwa Tanzania Bara ni ama Wakristu, kwa uchache sana waislamu na/au wenye dini nyingine (lakini si uislamu).
Pia ndani ya ukanda wa Pwani ukristu umeenea sana na idadi ya wakristu kuongezeka. Pia wana ushawishi mkubwa wa kitamaduni (umagharibi) kuliko uarabu (tazama miji ya dar, tanga),. Wakristu hawa ni wapinzani wa uislamu kwani kwa mtazamo wao u-islamu ni si dini sahihina (wenye mtazamo mkali uislamu=ushetani). Kundi hili la wakristu watakuwatayari kumpigia kura rais yeyote asiye mu-islamu kwani kufanya hivyo ni sehemuya kuimarisha uinjilishaji.
Hapa kigezo cha usafi kitashindwa dhidi ya umoja. Ajenda ya ufisadi haitakuwa na nguvu tena. Mgombea u-Rais muislamu asiye na msimamo mkali na ambaye hajulikani vizuri huku bara anaweza kupewa nafasi kiasi ndani ya jumuia ya kikristu lakini ni wakristu wachache wataziba masikio yao wakati wa kampeni kama kauli hii itatumika waislamu kuongoza nchi kwa awamu mbili, yaani miaka 20 . kwa hakika ataungwa mkono kwa nguvu zote na waislamu hata kama hana sifa, sifa kuu ya kuwa mu-islamu itakuwa kigezo kikuu. Huyu ndiye atakayebeba jukumu la kukamilisha uwepo wa mahakama ya kadhi na vipaumbele kadhaa kwa waislamu.
Waislamu watapata nafasi ya kutafakari upya ndoto ya kuanzisha mahakama ya kadhi. Karata ya waislamu wa Tanzania kumpata raisi muislamu awamu ya tano itawabidi kuungana na wazanzibari kupigana kupata Rais wa Muungano mzanzibari. Kwani hilo litawahakikishia rais muislamu (hata kama ni mzanzibari).
Kama hili likifanyika (limeanza kufanyika?) changamoto kuu ni namna ya kumuuza kwa wabara, ambao ni wapiga kura wengi na ambao kwa hakika bado hawaoni mzanzibari anayefaa kwa sasa kuwaongoza. Hili la changamoto za kumnadi mgombea uraisi mzanzibari nitalieleza vizuri katika sehemu zijazo.
Hivyo basi vyama vya siasa, wagombea urais na wapambe wao wanalazimika kukiangalia vizuri kigezo hiki chadini na kuchagua maneno mazuri sana ya kutumia kuwauza watu wao. Ni wakati muafaka wa think tanks za watu hawa kufanya kazi hasa juu ya hili ikiwemo kupata ushauri wa wataalmu (Consultants) wenye weledi.
Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx tuonane maranyingine xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx