Vifo Katesh; Je, Tanzania kuna milima mingine kama mlima Hanang?. Serikali imechukua hadhari gani?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,319
12,622
Tunasubiri vifo ili turushe helkopta kuangalia kiwango cha uharibifu na idadi ya waliokufa badala ya kunusa mapema hatari na dalili vifo.

Kwa kilichotokea Hanang ni matokeo ya mipango mibaya ya watanzania wenzetu tunaowalipa kwa kazi ya kutulinda na majanga. Kuna idadi kubwa ya watanzania ambao wameruhusiwa kujenga chini na juu ya milima, mabondeni, kwenye njia za maji na wanyama.

Watu hawa wamepewa vibali vyote ama vya kujenga, au kuingiza umeme na maji kwenye nyumba zao bila kupewa onyo la aina yoyote wala elimu ya namna ya kuishi kwenye maeneo hayo.

Maswali:,
1. Je, baada ya maafa ya Katesh, watu waendelee kujenga na kuishi kwenye maeneo yao yaleyale yaliyokubwa na janga au wahamie kwingine?
2. Je, Tanzania hakuna watanzania wanaoishi kwenye maeneo yanayofanana na maeneo ya Katesh?
3. Je, kuna mifumo gani ya kutaarifiana kama ving'ora kama likitokea janga?

Kinga ni bora kuliko kiba hii tunayoiona.
 
Uzuri wa viongozi wetu ni wazuri sana kuhudhuria maeneo ya matukio kwa wingi na kupiga picha za kutosha pamoja na ahadi/kauli za haja.

Huwa wanaenda mbali zaidi na kuchukulia kila janga kuwa ni jipya kabisa na linatokea kwa mara ya kwanza. Maana huundwa tume za uchunguzi na jopo la wakaguzi.

Tanzania tuna laana kubwa sana ya kuaminishwa kuwa tuna amani na tuitunze. Hii laana imekuja na uoga mkubwa wa kudai hata kilicho stahiki yetu.
 
Pia kwa kasi yetu ya kuzaana, wakati nchi haiongezeki, huko mbele watu watazidi kubanana tu.

Hivyo tunahitaji kupangilia vizuri sana both land use na family planning.

Enzi za kuzaana zaana ovyo tu na kuishi kwa kujua nchi kubwa tu hii zinaisha.
 
Uzuri wa viongozi wetu ni wazuri sana kuhudhuria maeneo ya matukio kwa wingi na kupiga picha za kutosha pamoja na ahadi/kauli za haja.

Huwa wanaenda mbali zaidi na kuchukulia kila janga kuwa ni jipya kabisa na linatokea kwa mara ya kwanza. Maana huundwa tume za uchunguzi na jopo la wakaguzi.

Tanzania tuna laana kubwa sana ya kuaminishwa kuwa tuna imani na tuitunze. Hii laana imekuja na uoga mkubwa wa kudai hata kilicho stahiki yetu.
majanga haya ni mitaji
 
Pia kwa kasi yetu ya kuzaana, wakati nchi haiongezeki, huko mbele watu watazidi kubanana tu.

Hivyo tunahitaji kupangilia vizuri sana both land use na family planning.

Enzi za kuzaana zaana ovyo tu na kuishi kwa kujua nchi kubwa tu hii zinaisha.
Mipango miji yetu ni hovyo sana. Kwenye mipango miji safi Watu wooote wa Dar, bagamoyo na kibaha wangeenea kwenye wilaya moja tu ya Kinondoni.
 
Mipango miji yetu ni hovyo sana. Kwenye mipango miji safi Watu wooote wa Dar, bagamoyo na kibaha wangeenea kwenye wilaya moja tu ya Kinondoni.
Huko mijini ukijenga kwa kwenda juu, unabaki na nafasi kubwa sana. Tatizo nyumba nyingi za chini. Yani sehemu ya kukaa famikia 10, kwa kujenga ghorofa kumi, inakaa familia moja tu.

Matokeo yake, mji unakuwa mkubwa mara 10 kuliko inavyotakiwa juwa kama tungejenga kwenda juu.
 
Pia kwa kasi yetu ya kuzaana, wakati nchi haiongezeki, huko mbele watu watazidi kubanana tu.

Hivyo tunahitaji kupangilia vizuri sana both land use na family planning.

Enzi za kuzaana zaana ovyo tu na kuishi kwa kujua nchi kubwa tu hii zinaisha.
Mkuu,
Nakupinga
Tanzania ipo UNDER POPULATION ukiangalia ENEO na Population yetu huwezi sema tunazaliana Kwa Kasi wakati population imejikusanya mahali pamoja na sehemu kubwa ya ardhi ipo under populated......
 
Nafikiri ile ilo poromoshwa na maji ni volcanic ashes..

Milima mingi TZ ipo kwenye miamba migumu... La, Mwanza kungekua hakuna mtu anaishi. Wote wako milimani...au Mbeya.
 
Mkuu,
Nakupinga
Tanzania ipo UNDER POPULATION ukiangalia ENEO na Population yetu huwezi sema tunazaliana Kwa Kasi wakati population imejikusanya mahali pamoja na sehemu kubwa ya ardhi ipo under populated......
Tatizo unaangalia eneo tu.

Hujaangalia arable land. Hujaangalia irrigation. Hujaangalia technology.

Unaweza kuwa na eneo kubwa, huna uwezo wa kulitumia vizuri, huna technology,ukawa na tatizo kwamba kwa level yako ya maendeleo, uko overpopulated.

Halafu akaja mtu ana population kama wewe eneo dogo, anajua kulitumia, ana technology kubwa, akawa underpopulated.

Japan wana watu zaidi ya milioni 125, karibu mara mbili ya population ya Tanzania.

Tanzania ina 365,756 sq mi Japan ina 145,937.06 sq mi, lakini Japan ina tatizo la kuongeza watu, Tanzania ina watu wengi sana wasio na kazi na haitakiwi kuongeza watu zaidi kwa kasi wakati hawa waliopo tu hatujui tufanye nini.

Katika dunia ambayo watu wanaweza kujenga miji kwenda juu kama Tokyo, suala la overpopulation si la ukubwa wa nchi tu, ni suala la teknolojia na uwezo wa kukabiliana na mazingira.

Kwa teknolojia yetu ambayo hata kilimo cha umwagiliaji kinatushinda, bado tunakata miti kupata kuni kamansource of energy, we are overpopulated.
 
Tunasubiri vifo ili turushe helkopta kuangalia kiwango cha uharibifu na idadi ya waliokufa badala ya kunusa mapema hatari na dalili vifo.

Kwa kilichotokea Hanang ni matokeo ya mipango mibaya ya watanzania wenzetu tunaowalipa kwa kazi ya kutulinda na majanga. Kuna idadi kubwa ya watanzania ambao wameruhusiwa kujenga chini na juu ya milima, mabondeni, kwenye njia za maji na wanyama. Watu hawa wamepewa vibali vyote ama vya kujenga, au kuingiza umeme na maji kwenye nyumba zao bila kupewa onyo la aina yoyote wala elimu ya namna ya kuishi kwenye maeneo hayo.

Maswali:,
1. Je, baada ya maafa ya Katesh, watu waendelee kujenga na kuishi kwenye maeneo yao yaleyale yaliyokubwa na janga au wahamie kwingine?
2. Je, Tanzania hakuna watanzania wanaoishi kwenye maeneo yanayofanana na maeneo ya Katesh?
3. Je, kuna mifumo gani ya kutaarifiana kama ving'ora kama likitokea janga?

Kinga ni bora kuliko kiba hii tunayoiona.
Inaelekea wewe bado kijana mdogo! Landslide iliyotokea Makonde plateau huko Mtwara ilikuwa kubwa sana na iliangamiza vijiji na watu wengi sana. Majanga kama haya kuyazuia ni vigumu sana kwa sababu mbalimbali.

Kwa mfano ili kuzuia maporomoko ya mlima Hanang ilitakiwa kupunguza uwingi wa maji kwa kuzibua chem chem (springs) ili zitiririshe maji mengi. Kitendo cha kutiririsha maji mengi baada ya muda mrefu kungesababisha vijito kutoka mlimani kupungua maji. Kwa hiyo watu wangelalamika na kupelekea kumtuhumu huyo aliyetoa wazo hilo kama mhujumu uchumi!

Kitaalamu inawezekana kujenga vipima maji (piezometers) ili kupima uwingi wa maji kila wakati lakini inahitajika utashi wa kisiasa kuidhinisha matumizi ya fedha zinazotakiwa.
 
Tatizo unaangalia eneo tu.

Hujaangalia arable land. Hujaangalia irrigation. Hujaangalia technology.

Unaweza kuwa na eneo kubwa, huna uwezo wa kulitumia vizuri, huna technology,ukawa na tatizo kwamba kwa level yako ya maendeleo, uko overpopulated.

Halafu akaja mtu ana population kama wewe eneo dogo, anajua kulitumia, ana technology kubwa, akawa underpopulated.

Japan wana watu zaidi ya milioni 125, karibu mara mbili ya population ya Tanzania.

Tanzania ina 365,756 sq mi Japan ina 145,937.06 sq mi, lakini Japan ina tatizo la kuongeza watu, Tanzania ina watu wengi sana wasio na kazi na haitakiwi kuongeza watu zaidi kwa kasi wakati hawa waliopo tu hatujui tufanye nini.

Katika dunia ambayo watu wanaweza kujenga miji kwenda juu kama Tokyo, suala la overpopulation si la ukubwa wa nchi tu, ni suala la teknolojia na uwezo wa kukabiliana na mazingira.

Kwa teknolojia yetu ambayo hata kilimo cha umwagiliaji kinatushinda, bado tunakata miti kupata kuni kamansource of energy, we are overpopulated.
Nitakuwa kinyume na wewe.Mimi naona nchi zenye idadi kubwa ya watu ndiyo zenye maendeleo (kiuchumi) makubwa hapa duniani.
 
Nitakuwa kinyume na wewe.Mimi naona nchi zenye idadi kubwa ya watu ndiyo zenye maendeleo makubwa hapa duniani.
Maendeleo hayaji kwa idadi kubwa ya watu, maendeleo yanakuja kutokana na kujua kutumia watu na kupanga uchumi vizuri kulingana na idadi ya watu.

Unaweza kuwa na watu wengi, lakini hujajipanga, unaongeza njaa tu.

Ingekuwa maendeleo yanatokana na wingi wa watu, India ingekuwa imeendelea kuliko Marekani na Nigeria ingekuwa imeendelea kuliko Italy.
 
Back
Top Bottom