Ablessed
JF-Expert Member
- Mar 19, 2013
- 4,616
- 3,499
Yaani hadi inaudhi kuwa na kiongozi kama huyu hajui hata anachokifanya, yaani hajitambui hata alifanyalo sasa kusema kua hakuna kipaza sauti hawezi kuongea na wanafunzi kwani mbunge alikua anatumia nini. Hii ndio type ya watu waliokariri namna ya utendaji kazi hawajui hata kutumia mbinu mbadala. Sijui kwanini yupo madarakani hadi sasa, mtu akisema anaambiwa ni mpinzani jamani hata mambo yaliyo bayana tusihoji kisa tutaambiwa wapinzani. Nanyi maaskari kwanini mnafanya hivi hebu waoneeni huruma binadamu wenzenu msitumie jazba kumbukeni mambo haya yanamwisho. Muda ukifika haki itakaposimama mtaona mnaonewa pale mtakapokua mnapelekwa mbele ya sheria ndugu zangu. Mbona mnaweza tu kutuliza fujo kistaarabu sio lazima kutumia mabavu acheni hizo bwana.Duh Mkuu wa Mkoa Kiburi! Hizi semina elekezi vipi kuna watu walienda haneymoon badala ya kufuata maelekezo ya Uongozi Bora? Swala kama hili huwezi kulichukulia personal hata siku moja! Jamaa kakwazwa live alitaka kusujudiwa na mtu kama huyu ni hatari kwelikweli akiwa Raisi hafai popote. Mkuu wa mkoa ni nafasi inayohitaji busara na hekima za hali ya juu, pamoja na kupata somo kwa h Lema, bado hakulisoma kasimamia ushabiki na jazba! Hebu ngoja nione kama atabaki muda gani katika nafasi na mkoa huo. Ninavyoamini mkoa sensitive kama Arusha hauhitaji mtu asiyekuwa sensitive kama huyu, kama hao wangekuwa ni wananchi na wanataka kuongea nae, Arusha si ndo pasingekalika, yangerudia mautumbo yaleyale.
Poleni wanafunzi kwa msiba na shuluba hii!
Poleni ambao hamkuona, nunueni moderm zenye speed sio bei rahisi.