MAMLAKA ya Mafunzo na Ufundi Stadi Tanzania (VETA) imesema kuwa wameunda gari linalotumia mfumo wa sola.
Mtafiti wa Soko la Ajira wa VETA, Abdallah Mhagama, alisema gari hilo walilolibuni halina moshi wala kelele lakini likiwa mahali ambapo hakuna jua kwa saa tano haliwezi kufanya kazi.
Alisema utafiti wa gari hilo ulichukua mwaka mmoja ambapo lina uwezo wa kubeba watu wanane. Gari hilo la sola lina spidi 100 kwa saa. Veta tuna uwezo wa kubadilisha gari lolote kulipeleka kwenye sola, alisema na kuongeza kuwa magari yanayotumia sola hayana gharama.
Kwa mujibu wa mtafiti huyo, alisema gari hilo limegharimu shilingi mil. saba. Alisema ubunifu huo utasaidia kupunguza gharama za mafuta.
Sorce Tanzania Daima
Mtafiti wa Soko la Ajira wa VETA, Abdallah Mhagama, alisema gari hilo walilolibuni halina moshi wala kelele lakini likiwa mahali ambapo hakuna jua kwa saa tano haliwezi kufanya kazi.
Alisema utafiti wa gari hilo ulichukua mwaka mmoja ambapo lina uwezo wa kubeba watu wanane. Gari hilo la sola lina spidi 100 kwa saa. Veta tuna uwezo wa kubadilisha gari lolote kulipeleka kwenye sola, alisema na kuongeza kuwa magari yanayotumia sola hayana gharama.
Kwa mujibu wa mtafiti huyo, alisema gari hilo limegharimu shilingi mil. saba. Alisema ubunifu huo utasaidia kupunguza gharama za mafuta.
Sorce Tanzania Daima