Uzito kupitiliza watajwa kuwa changamoto, wahusika hatarini kupata magonjwa ya Moyo

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Picha 5.JPG
"Sehemu kubwa ya jamii yetu tuliyoipata idadi kubwa ni uzito uliopitiliza ukilinganisha na wale ambao uzito upo chini, na sababu kubwa ya wale ambao uzito upo chini wengi ni kwa sababu ya upatikanaji wa vyakula vya makundi yote lakini wengine ni kuchagua kuacha kula baadhi ya vyakula vya makundi muhimu ya chakula uenda ni kwa sababu ya elimu ambazo wanazipata kuna vyakula wameviacha kabisa."

Hayo yameelezwa na Mtaalamu wa Masuala ya Lishe, Maria Samlongo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kufuatia kambi ya siku mbili ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Dar Group iliyopo TAZARA, inanayotoa Huduma za Tiba Mkoba (Outreach Service) kwa kufanya kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa jirani.
Snapinsta.app_431263622_3817137471847528_2616976886609961790_n_1080.jpg

Snapinsta.app_431194402_1452121175726396_488286043586833007_n_1080.jpg
Kambi hiyo imewajumuisha na wataalamu wa lishe ambao wanatoa elimu ya lishe bora ambayo inalenga kuwapa wananchi uelewa wa kufuata mtindo bora wa maisha na kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo ambayo yanaweza kuepukika kwa kufuata ushauri wa kitaalumu.

Ambapo mtaalamu huyo wa masuala ya lishe ameeleza kuwa yapo madhara ambayo watu wenye uzito wa kupitiliza yanaweza kuwakumba, ambapo ametaja baadhi kuwa ni pamoja na magonjwa ya kisukari, presha na mogonjwa ya moyo.

Aidha kwa upande wa Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto, ambaye ni Kaimu Mkuu wa Huduma za Tiba za Hospitali ya Dar Group, Dr. Eva Wakuganda ameeleza mwitikio wa watu katika kunufaika na huduma hiyo ambapo amesema wananchi wamejitokeza na baadhi yao wanaogundulika na matatizo ya moyo wanawahudumia kulinga na majibu ya vipimo.

Pia Kaimu Mkurugenzi wa JKCI- Dar Group Hospital, Iddi Lemmah ameendelea kutoa wito kwa wananchi kujitokeza kunufaika na huduma hiyo inayotolewa bure. Ambapo huduma hiyo inatarajiwa kuhitimishwa kesho March 3, 2024 ikiwa ni siku ya pili.

Itakumbukuwa Dr. Eva alitaja dalili mbalimbali za magonjwa ya moyo kwa watoto wadogo kuwa ni pamoja na mtoto kuanza kuwa na mwonekano wa rangi ya bluu kwenye sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo kwenye midomo na kucha, changamoto ya upumuaji, kushindwa kuongezeka uzito, mapigo ya moyo kwenda mbio, mtoto kushindwa kula au akila anachoka na kutoka sana jasho.
 
Kuna program nilikua naangalia jana kupitia chaneli ya Davinci (star tmes), nilichokiona nadhani kitabadilisha mtazamo wangu kuhusu matumizi ya sukari. Vinywaji na vyakula vilivyo sindikwa vinasukari ambayo ukiona kwa macho kiwango cha sukari kinachowekwa, pengine unaweza usivitumie tena.. matokeo ya sukari kwa asilimia kubwa ni chanzo cha magonjwa mengi yasiyo ya kuambukiza. Nilifikiria mengi, hata vinywaji vyenye ziro sugar sijui sugar free hakuna tofauti hata kidogo.
 
Back
Top Bottom