Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
MCHUNGAJI wa Kanisa Anglikana Parishi ya Pandambili Jimbo Kuu la Mpwapwa-Kongwa mkoani hapa, Petro Namga, amesimamishwa kazi kutokana na kashfa ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na muumini wake.
Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Dk. Jacob Chimeledya, alilithibitishia gazeti hili jana kutokea kwa tukio hilo na kuwa tayari hatua za awali zimechukuliwa dhidi ya mchungaji huyo.
Alisema kutokana na kashfa hiyo, mchungaji Namga amesimamishwa kutoa huduma katika Kanisa la Parishi hiyo, kwa muda wa miezi mitatu kama hatua ya awali huku uchunguzi ukiendelea.
Askofu huyo alifafanua kuwa uamuzi huo ulitokana na uchunguzi wa awali uliofanywa na viongozi wa Kanisa ngazi ya jimbo na kubaini ukweli wa mchungaji huyo kufanya hivyo kinyume cha taratibu na Sheria za Kanisa.
Hatua zaidi zitachukuliwa kwa kuwa kitendo kilichotokea ni utovu wa nidhamu na ukiukwaji mkubwa wa maadili ya huduma za kiroho, alisema Askofu Chimeledya.
Aidha Askofu huyo alibainisha kuwa kitendo hicho kimeliaibisha Kanisa na hawezi kuendelea na kazi ya kumtumikia Mungu.
Mchungaji Namga anatuhumiwa kwa kashfa hiyo, baada ya simu ya mwanamke huyo kukutwa na ujumbe wa mapenzi kutoka kwa mchungaji huyo. Mmoja wa waumini wa Kanisa hilo, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alidai kuwa baada ya mwanamke huyo kubanwa, alimtaja mchungaji huyo kuwa ndiye humtumia ujumbe huo wa mapenzi.
Alifafanua kuwa mume wa muumini huyo, alikuta ujumbe wa mapenzi katika simu ya mkewe na alipombana zaidi kuwa ujumbe huo ulitumwa na mchungaji huyo ambaye alikuwa akimtaka kimapenzi kwa muda mrefu.
Mume aliwaagiza baadhi ya watu kwenda kumweleza mchungaji huyo juu ya tabia yake lakini hakuna kilichobadilika, kwani aliendelea kumfuatilia mkewe.
Aliongeza kuwa kutokana na mchungaji kuendelea na tabia yake alimwekea mtego na kumkamata akiwa na mkewe na kuifikisha kesi hiyo katika uongozi wa juu wa Kanisa hilo.
Muumini huyo alifafanua kuwa baada ya vikao kadhaa vya usuluhishi kati ya mume, mchungaji na uongozi wa Kanisa, tangu Januari mwaka huu, hatimaye walifikia muafaka, ambapo Februari 25 mchungaji aliamriwa kulipa faini ya Sh 100,000.
Pamoja na faini hiyo pia viongozi wa juu ngazi ya jimbo akiwamo Askofu Mkuu, walikubaliana kutoa adhabu ya kumsimamisha mchungaji huyo mpaka uchunguzi wa kina utakapofanyika.
HabariLeo ilimtafuta Mchungaji huyo lakini alipopigiwa simu na kujulishwa juu ya suala hilo, alikata, na baadaye alipopigiwa tena simu iliita kwa muda mrefu bila majibu na hatimaye kuzimwa.
Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Dk. Jacob Chimeledya, alilithibitishia gazeti hili jana kutokea kwa tukio hilo na kuwa tayari hatua za awali zimechukuliwa dhidi ya mchungaji huyo.
Alisema kutokana na kashfa hiyo, mchungaji Namga amesimamishwa kutoa huduma katika Kanisa la Parishi hiyo, kwa muda wa miezi mitatu kama hatua ya awali huku uchunguzi ukiendelea.
Askofu huyo alifafanua kuwa uamuzi huo ulitokana na uchunguzi wa awali uliofanywa na viongozi wa Kanisa ngazi ya jimbo na kubaini ukweli wa mchungaji huyo kufanya hivyo kinyume cha taratibu na Sheria za Kanisa.
Hatua zaidi zitachukuliwa kwa kuwa kitendo kilichotokea ni utovu wa nidhamu na ukiukwaji mkubwa wa maadili ya huduma za kiroho, alisema Askofu Chimeledya.
Aidha Askofu huyo alibainisha kuwa kitendo hicho kimeliaibisha Kanisa na hawezi kuendelea na kazi ya kumtumikia Mungu.
Mchungaji Namga anatuhumiwa kwa kashfa hiyo, baada ya simu ya mwanamke huyo kukutwa na ujumbe wa mapenzi kutoka kwa mchungaji huyo. Mmoja wa waumini wa Kanisa hilo, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alidai kuwa baada ya mwanamke huyo kubanwa, alimtaja mchungaji huyo kuwa ndiye humtumia ujumbe huo wa mapenzi.
Alifafanua kuwa mume wa muumini huyo, alikuta ujumbe wa mapenzi katika simu ya mkewe na alipombana zaidi kuwa ujumbe huo ulitumwa na mchungaji huyo ambaye alikuwa akimtaka kimapenzi kwa muda mrefu.
Mume aliwaagiza baadhi ya watu kwenda kumweleza mchungaji huyo juu ya tabia yake lakini hakuna kilichobadilika, kwani aliendelea kumfuatilia mkewe.
Aliongeza kuwa kutokana na mchungaji kuendelea na tabia yake alimwekea mtego na kumkamata akiwa na mkewe na kuifikisha kesi hiyo katika uongozi wa juu wa Kanisa hilo.
Muumini huyo alifafanua kuwa baada ya vikao kadhaa vya usuluhishi kati ya mume, mchungaji na uongozi wa Kanisa, tangu Januari mwaka huu, hatimaye walifikia muafaka, ambapo Februari 25 mchungaji aliamriwa kulipa faini ya Sh 100,000.
Pamoja na faini hiyo pia viongozi wa juu ngazi ya jimbo akiwamo Askofu Mkuu, walikubaliana kutoa adhabu ya kumsimamisha mchungaji huyo mpaka uchunguzi wa kina utakapofanyika.
HabariLeo ilimtafuta Mchungaji huyo lakini alipopigiwa simu na kujulishwa juu ya suala hilo, alikata, na baadaye alipopigiwa tena simu iliita kwa muda mrefu bila majibu na hatimaye kuzimwa.