Trubetzkoy
JF-Expert Member
- Oct 31, 2018
- 298
- 542
Habari!
Picha linaanza kwa kumuangazia bwana X ambaye kutokana na tabia yake ya uzinzi imekuwa ni kawaida kwake kutamani kila mwanake anayekatiza mbele ya macho yake. Hali hii imemfanya awe na orodha ndefu ya wanawake alioshiriki nao tendo la ndoa na mara nyingi akishamnyandua mwanamke huwa hamrudii tena mwanamke huyo.
Ilitokea siku moja jamaa alimnyandua binti fulani na kama ilivyo kawaida yake baada ya mnyanduo jamaa akakata mawasiliano na huyo binti japo walikuwa wakionana mara kadhaa ila hakukuwa na stori zaidi ya salamu.
Miezi takribani kumi baada ya kukutana kimwili jamaa anapigiwa simu na yule dada, dada anadai amejifungua na mtoto ana umri wa wiki moja kwahiyo binti anachohitaji ni jamaa apendekeze mtoto apewe jina gani.
Taarifa hii si tu ilimshitua jamaa bali ilimkasirisha pia. Alipouliza hili linawezekanaje na kwanini binti hakutoa taarifa ya ujauzito wake badala yake amekaa kimya kipindi chote cha ujauzito na amekuja kutoa taarifa mtoto kashazaliwa, binti anadai ooh! niliogopa kukwambia nilihisi pengine ungeniambia nitoe na mimi kutoa mimba siwezi naogopa. Jamaa akachanganyikiwa akamwambia binti kwa sasa siwezi kukujibu chochote kwa sababu taarifa imekuwa ya ghafla sana.
Baada ya hapo jamaa akaamua kufanya ujasusi na hatimaye aligundua kuwa miezi michache baada ya kukutana kimwili na yule binti, binti aliolewa na mshkaji mwingine na kipindi chote hicho muoaji hakujua kuwa mkewe ni mjamzito. Muoaji amekuja kushtuka tumbo limeshakuwa kubwa na hapo hapo wakaongozana kwenda hospitali ambapo ilibainika mimba imeshakuwa kubwa na kwamba muda wowote binti angeweza kujifungua.
Jamaa(mume) baada ya kupata maelezo hayo ya kitabibu ilibidi aitishe wana ukoo kwa ushauri zaidi. Haikupita wiki moja binti akajifungua. Mume wa binti hakuweza kumsaidia binti kwa chochote badala yake alimfungashia kila kilicho chake na kumtimua.
Ndugu yangu (mzinzi) baada ya kupata taarifa hizo za kijasusi aliweka msimano kwamba huyu mtoto sitahusika naye kwa lolote, lakini ulipopita mwezi mmoja tangu kuzaliwa mtoto, mzinzi alitumiwa picha ya mtoto ambaye mama yake na ndugu wengine walidai kuwa mtoto kafanana naye(kafanana na mzinzi). Mzinzi alipotazama picha, kwa kiasi fulani mtoto kafanana naye. Sasa kaja kuniomba ushauri kwamba je, katika mazingira kama hayo amkubali mtoto au abaki na msimano wake wa awali?
Naomba mnishauri ili nikamshari mwana.
Picha linaanza kwa kumuangazia bwana X ambaye kutokana na tabia yake ya uzinzi imekuwa ni kawaida kwake kutamani kila mwanake anayekatiza mbele ya macho yake. Hali hii imemfanya awe na orodha ndefu ya wanawake alioshiriki nao tendo la ndoa na mara nyingi akishamnyandua mwanamke huwa hamrudii tena mwanamke huyo.
Ilitokea siku moja jamaa alimnyandua binti fulani na kama ilivyo kawaida yake baada ya mnyanduo jamaa akakata mawasiliano na huyo binti japo walikuwa wakionana mara kadhaa ila hakukuwa na stori zaidi ya salamu.
Miezi takribani kumi baada ya kukutana kimwili jamaa anapigiwa simu na yule dada, dada anadai amejifungua na mtoto ana umri wa wiki moja kwahiyo binti anachohitaji ni jamaa apendekeze mtoto apewe jina gani.
Taarifa hii si tu ilimshitua jamaa bali ilimkasirisha pia. Alipouliza hili linawezekanaje na kwanini binti hakutoa taarifa ya ujauzito wake badala yake amekaa kimya kipindi chote cha ujauzito na amekuja kutoa taarifa mtoto kashazaliwa, binti anadai ooh! niliogopa kukwambia nilihisi pengine ungeniambia nitoe na mimi kutoa mimba siwezi naogopa. Jamaa akachanganyikiwa akamwambia binti kwa sasa siwezi kukujibu chochote kwa sababu taarifa imekuwa ya ghafla sana.
Baada ya hapo jamaa akaamua kufanya ujasusi na hatimaye aligundua kuwa miezi michache baada ya kukutana kimwili na yule binti, binti aliolewa na mshkaji mwingine na kipindi chote hicho muoaji hakujua kuwa mkewe ni mjamzito. Muoaji amekuja kushtuka tumbo limeshakuwa kubwa na hapo hapo wakaongozana kwenda hospitali ambapo ilibainika mimba imeshakuwa kubwa na kwamba muda wowote binti angeweza kujifungua.
Jamaa(mume) baada ya kupata maelezo hayo ya kitabibu ilibidi aitishe wana ukoo kwa ushauri zaidi. Haikupita wiki moja binti akajifungua. Mume wa binti hakuweza kumsaidia binti kwa chochote badala yake alimfungashia kila kilicho chake na kumtimua.
Ndugu yangu (mzinzi) baada ya kupata taarifa hizo za kijasusi aliweka msimano kwamba huyu mtoto sitahusika naye kwa lolote, lakini ulipopita mwezi mmoja tangu kuzaliwa mtoto, mzinzi alitumiwa picha ya mtoto ambaye mama yake na ndugu wengine walidai kuwa mtoto kafanana naye(kafanana na mzinzi). Mzinzi alipotazama picha, kwa kiasi fulani mtoto kafanana naye. Sasa kaja kuniomba ushauri kwamba je, katika mazingira kama hayo amkubali mtoto au abaki na msimano wake wa awali?
Naomba mnishauri ili nikamshari mwana.