Annina
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 437
- 57
Inawezekana suala hili limesha ongelewa humu jamvini, mniwie radhi kama ninalirudia katika namna ya kuwarudisha nyuma. Siku zote nimekuwa na wazo la kuunganisha nguvu za kuweza kusaidia kutatua matatizo katika jamii yetu japo kwa kiasi kidogo.
Kupitia mijadala mbalimbali hapa JF nimeona wengi wanaguswa na hali mbaya ya maisha inayotukabili wananchi wa kawaida. Ni wazi serikali yetu kwa sababu mbalimbali ambazo zimejadiliwa pia humu inashindwa kutimiza majukumu yake ikiwa ni pamoja na huduma za kijamii kama vile afya (mfano wa post ya Mwanakijiji kuhusu ward ya akina mama katika hospitali ya temeke), maji, usafi wa miji yetu nk nk.
Wazo langu ni kuwa, badala ya kuishia kujadili tu na kuacha hali iendelee kama ilivyo, tunaweza kujipanga tukabadili hali kwa kiasi fulani pamoja na uwezo mdogo tulionao. Tunaweza kupitia mkuu wa kaya, tukajipanga na kuchangia vitanda katika baadhi ya hospitali, au madawati, vitabu katika shule au kufanya usafi katika baadhi ya maeneo, au chochote chenye kugusa maslahi ya umma kadri tutakavyoona inafaa kwa wakati huo. Pia tunaweza kuandaa vijarida (popular version) vya elimu ya uraia katika minajili ya kuelimisha umma.
Annina
Kupitia mijadala mbalimbali hapa JF nimeona wengi wanaguswa na hali mbaya ya maisha inayotukabili wananchi wa kawaida. Ni wazi serikali yetu kwa sababu mbalimbali ambazo zimejadiliwa pia humu inashindwa kutimiza majukumu yake ikiwa ni pamoja na huduma za kijamii kama vile afya (mfano wa post ya Mwanakijiji kuhusu ward ya akina mama katika hospitali ya temeke), maji, usafi wa miji yetu nk nk.
Wazo langu ni kuwa, badala ya kuishia kujadili tu na kuacha hali iendelee kama ilivyo, tunaweza kujipanga tukabadili hali kwa kiasi fulani pamoja na uwezo mdogo tulionao. Tunaweza kupitia mkuu wa kaya, tukajipanga na kuchangia vitanda katika baadhi ya hospitali, au madawati, vitabu katika shule au kufanya usafi katika baadhi ya maeneo, au chochote chenye kugusa maslahi ya umma kadri tutakavyoona inafaa kwa wakati huo. Pia tunaweza kuandaa vijarida (popular version) vya elimu ya uraia katika minajili ya kuelimisha umma.
Annina