Utitiri wa shule za "English Medium"

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
Nukuu hii hapa chini ni malengo makuu ya kuanzishwa kwa shule ya Southern Highlands School inayotoa elimu kwa kufuata mtaala wa lugha ya Kiingereza (English Medium School).Shule hii inamilikiwa na familia ya Mhe. Mungai ambae alipata kuwa Waziri wa Elimu wa nchi hii.
OBJECTIVES OF THE SCHOOL

Educational for children, with a strong English base, has become a topical issue among parents and educators in Tanzania. There is a community-felt need for an English-medium primary education curriculum.


The main objectives include:

· To equip children with sound knowledge of English for effective communication as citizens of a world that has become a single global village resulting from advances in information technology.

· To prepare children more effectively for English medium secondary school education in Tanzania.

· To provide boarding and day school experience for effective learning and social interaction among pupils themselves.

· To provide a learning school that is affordable, accessible, and cost effective to families who need English medium primary education for their children.

· To motivate pupils to become passionate in learning in order to become self-reliant, disciplined and well-behaved young people.

· To provide children with early exposure to information technology.



Southern Highlands School:
* Executive Director Mrs. Mary A. Mungai
*School’s Head Teacher Njoroge Francis
*School’s Deputy Head Teacher James Kelela​




Ki mtazamo, inaonekana kana kwamba shule nyingi za "English Medium" zimekuwa zikianzishwa kwa madhumuni makubwa ya kuwajenga vijana wetu kufahamu kiingereza zaidi lakini wakati huo huo tunahimiza matumuzi ya kiswahili chetu.

Uzoefu pia unaonyesha kuwa kwa sasa shule nyingi zimekuwa zikitumia hilo neno "English Medium" kuvuta wazazi wengi kupeleka watoto wao huo.. Laikini binafisi sina uthibitisho wa kutosha kuhusu viwango vya taaluma inayotolewa kupitia lugha hiyo ya Kiingereza ambacho kwa shule nyingi imekuwa ikifundishwa na wageni kutoka Kenya au Uganda na si Watazania japo kuwa wpo wale ambao wamemaliza katika shule hizi hizi za Kiingereza!.

Kwa wale wenye uzoefu na shule hizo labda watusaidie kiwango cha taaluma kinachotolewa na shule hizo mbali na suala la watoto kujua lugha ya Kiingereza!!.


 
kwani tatizo liko wapi, nawee ukitaka si ujenga yako? kama huna pesa za kujengea waache wenye nazo wajenge ili watoto wa kitz wafaidi. wivu tuuu wivu tuuu kila mkiona mtu anafanya kitu cha maana.
 
Kiwango cha taaluma kinategemea ni shule ipi unayoiongelea, hauwezi ukatoa comment kuhusu shule zote za English medium kwa pamoja.
 
Ukweli ni kuwa utitiri wa shule za English medium ni ushamba wa waswahili tu.Hata sisi tunaoanzisha wengine wala hatukithamini kiiengereza lakini tunafanya hivyo kuwavutia wazazi wa watoto wanaofikiri mtoto wao akizungumza kiiengereza kama mkoloni ndio mwisho wa matatizo.
Mimi nina shakaa na watendaji wa wizara ya elimu tangu zamani kwamba huwa wanahongwa na waiengereza na wafaransa ili lugha zao zifundishwe mashuleni.
Fitina ya umuhimu wa kiteknolojia juzi imezimwa baada ya mitandao ya intaneti kuanza kutumia hata herufi za lugha nyengine kama kiarabu bila hata herufi moja ya kiiengereza.Sasa watoto walioko arabuni au China wana ulazima gani kusoma kiiengereza?.
 
huu ni ujinga uliyokomaa TZ. kuna jirani yangu aliwapeleka watoto wake kusoma Nairobi miaka ya 90, ni tajiri sana an mihela kibao, watoto waliporudi likizo kiswahili washasahau na wazazi wao hawajui hata kuongea kithungu, ehh mbona aliwarudisha TZ kwani ilikuwa taabu sana! fuata mkumbo!
 
Back
Top Bottom