Uteuzi wa JK wa Mwandosya ni wa busara na hekima sana

Ndio maana tunasema serikali hii ya magamba ya kishikaji tu,rais anatoa vyeo kwa huruma? None sense!
 
Wengi wanamlaumu JK juu ya kumteua Prof. Mwandosya kuwa Waziri asiye na Wizara maalum. Nadhani upembuzi huo si sahihi. Mie nadhani JK amemheshimu sana Mwandosya. Kumbukeni Mwandosya bado hajarejesha afya yake vema, na hivyo JK hajampa Wizara kamili ambayo ingehitaji nguvu nyingi. Wengi tungeishia kusema Mwandosya bado mgonjwa kwa nini apewe Wizara kubwa wakati Watanzania wengine wapo.

Alichofanya JK ni sawa na kuamua kumpumzisha Mwandosya huku bado akimweka karibu ili asiwe mbali na yanayojiri katika Baraza la Mawaziri, ikimaanisha bado anahitaji busara za Mwandosya na anaamini atapona kabisa na kuendelea na kazi. Kumbukeni kuna wakati Nyerere alimpumzisha Sokoine akiwa mgonjwa kwa karibu kipindi cha miaka miwili. Sokoine alipopona kabisa ndipo Nyerere akamrudishia Uwaziri Mkuu. JK angempumzisha Mwandosya kwa namna hiyo watu ndio mngesema hata zaidi!

In fact JK kumfanya Mwandosya Waziri asiye na Wizara maalum Mwandosya atakuwa katika ofisi ya Raisi, ikimaanisha atakuwa karibu zaidi na JK kushauriana mambo yanayohusu Wizara yeyote ile. Mie binafsi ninaheshimu sana utendaji wa Mwandosya, na kwa hili alilofanya JK kwa Mwandosya nimeona JK katumia busara sana. Fikirieni kwa makini.

Labda cha kumsihi JK ni kwamba sasa atumie busara na umakini wa Mwandosya kwa namna kubwa hata zaidi kwa kuwa wako ofisi moja; Ofisi ya Raisi.


Inawezekana kuna busara katika kufanya hivyo, ila usitumie mifano ambayo siyo sahihi. Nyerere hakumpuzisha Sokoine kwa ajili ya Ugonjwa bali Sokoine alikuwa akienda kusoma elimu ya juu ya utawala huko Bulgaria.
 
Ndio maana tunasema serikali hii ya magamba ya kishikaji tu,rais anatoa vyeo kwa huruma? None sense!

Kwa hiyo kosa la Mwandosya ni kwamba aliumwa, ugonjwa ambao hata utata wake hakutaka kuingia kiundani akihofia kutovuruga watu? Haya bwana, ibilisi anakusikia, labda na wewe utaumwa!
 
Wengi wanamlaumu JK juu ya kumteua Prof. Mwandosya kuwa Waziri asiye na Wizara maalum. Nadhani upembuzi huo si sahihi. Mie nadhani JK amemheshimu sana Mwandosya. Kumbukeni Mwandosya bado hajarejesha afya yake vema, na hivyo JK hajampa Wizara kamili ambayo ingehitaji nguvu nyingi. Wengi tungeishia kusema Mwandosya bado mgonjwa kwa nini apewe Wizara kubwa wakati Watanzania wengine wapo.

Alichofanya JK ni sawa na kuamua kumpumzisha Mwandosya huku bado akimweka karibu ili asiwe mbali na yanayojiri katika Baraza la Mawaziri, ikimaanisha bado anahitaji busara za Mwandosya na anaamini atapona kabisa na kuendelea na kazi. Kumbukeni kuna wakati Nyerere alimpumzisha Sokoine akiwa mgonjwa kwa karibu kipindi cha miaka miwili. Sokoine alipopona kabisa ndipo Nyerere akamrudishia Uwaziri Mkuu. JK angempumzisha Mwandosya kwa namna hiyo watu ndio mngesema hata zaidi!

In fact JK kumfanya Mwandosya Waziri asiye na Wizara maalum Mwandosya atakuwa katika ofisi ya Raisi, ikimaanisha atakuwa karibu zaidi na JK kushauriana mambo yanayohusu Wizara yeyote ile. Mie binafsi ninaheshimu sana utendaji wa Mwandosya, na kwa hili alilofanya JK kwa Mwandosya nimeona JK katumia busara sana. Fikirieni kwa makini.

Labda cha kumsihi JK ni kwamba sasa atumie busara na umakini wa Mwandosya kwa namna kubwa hata zaidi kwa kuwa wako ofisi moja; Ofisi ya Raisi.

sidhan kama unafikiri vizuri..unadhani kupewa uwaziri usio na wizara maalumu ndo kuhitaji busara za muhusika?hapa hatuhitaj afya ya mtu ,2nahitaji maslahi ya taifa..je unadhan mwandosya atatumia pesa ngapi za watanzania?kwa kazi isiyoonekana?jiulize wakati nyerere anampumzisha sokoine kwa ugonjwa alimuundia wizara gani ili nyerere apate support ya watu wa monduli?kikwete ni msanii aliyebobea..watu wa mbeya msidanganyike..2nahitaji baraza dogo la mawaziri lenye ufanisi na sio mzigo kwa watanzania..achen kufikiri kwa makalio
 
Unajuaje kwamba hakomba apumzishwe akaambiwa bado unaweza kuwa na manufaa kwa nchi? Labda uwaulize wale ambao wamekuwa mawaziri, kwamba je, Mwandosya amekuwa na mchango wowote wa busara katika vikao vya Baraza la Mawaziri? Na wakikuambia ndio, jiulize ni jinsi gani JK angeweza kuendelea kutumia busara za Mwandosya katika vikao vya Baraza la Mawaziri katika mazingira kama haya. Kumbuka hata manaibu waziri hawaingii kwenye vikao vya Baraza la Mawaziri.

Mie binafsi nimewahi kushiriki vikao ambavyo Mwandosya amekuwapo, hapa nchini na nje ya nchi. Na nakuhakikishia kwamba that man bwana ana uwezo wa kupembenua pumba akatoa mbegu kwa namna ya pekee kabisa.

Kuna waziri mmoja aliwahi kusema kuna baadhi ya mawaziri hawampendi Mwandosya kwa kuwa akitoa point zake kwenye vikao vya Baraza la mawaziri anafanya waonekane ni watupu mno!
....hahah naamini kweli umetumwa
 
Nashangaa Mwandosya hajachukua maamuzi magumu mpaka sasa.
 
Huyu kama anaumwa ya nini kuongeza idadi ya mawaziri?

Halafu Mwandosya ana busara gani za ajabu kihivyo? Kuna speech moja katoa kwao huko utumbo mtupu, anahimiza watu wale rushwa bila aibu. Mie hata sioni tofauti.
 
Huyo bwana kichwa, cv yake inasoma bsc eng harafu phd, alifanya thesis ya msc wakampa phd, o lev A zote, A lev A zote!
 
....hahah naamini kweli umetumwa
wabongo bwana..!
So so mediatico..!
Eti vua gamba,,vaaa gwanda
sasa gwanda nalo likichakaa na kuchanika tutahamasishana kuvua na kuvaa nin??
Tunataka katiba mpya tuh hapa
politicians wote wanafiki tuh wanatucheza shere..!
 
Mwandosya bado ni mhimili wa Magamba Mbeya. JK hana option yoyote ya kukihalalisha CCM na wana Mbeya isipokuwa kwa kumheshimu Mwandosya. Kwa kasi ya CDM ilivyo Mbeya Mwandosya anatakiwa aendelee kuwepo barazani
 
Upepo wa kisiasa umeishia kuwa dhoruba ama kimbunga kama alivyodai suguu!
 
mi naona busara kwako ni kugawana madaraka. hivi huyo mwandosya ana katibu kweli wizarani kwake? je atakuwa katibu asiyekuwa na taaluma maalum nae? du natamani bunge lianze nione atakuwa anajibu maswali gani?
 
Kaongeza nini katika sayansi?

Are you serious? Naona uko ulimwengu mbali na huu. Kwa taarifa yako tu, katika mambo electrical engineering, kuna kitu inaitwa Mwandosya's formula au Mwandosya's principle, kutokana na umahili wake katika mifumo ya umeme. Na pia jamaa alikuwa na mchango katika kitu inaitwa Kyoto Protocol, akiwa msemaji wa G77 and China. Pia aliasisi energy policy ya nchini baada ya Tanzania kuingia mfumo wa biashara huria. Nk, nk, nk.




 
Kuna speech moja katoa kwao huko utumbo mtupu.

Mie kama sidhani kiongozi bora ni yule anayejua kutoa speech za kuvutia - labda huyo ni mwanasiasa bora. Sasa sijui kama Tanzania tunahitaji wanasiasa bora au viongozi bora. In fact hili ni tatizo kwa CCM na CDM, kwamba focus iko kwa wanasiasa bora na si viongozi bora. Katika mawaziri waliofukuzwa, wapo wanasiasa bora, lakini hawakuwa viongozi bora.

Nitakuwa wa kwanza kukiri kwamba Mwandosya si mtoa hotuba mzuri, japo ni kiongozi mzuri. Wakazi wa Mbeya wanawapenda sana Sugu na Mwandosya; sababu za kumpenda Sugu ni tofauti sana na sababu za kumpenda Mwandosya. Mwandosya hapendwi kwa ajili ya uwezo wake wa kuimba jukwaani, "kudua" au ku-resonate na washikaji wa mtaani. Sasa niambie, nani kati ya Mwandosya na Sugu ni mwanasiasa bora na nani ni kiongozi bora? Wewe ungechagua yupi ikiwa maendeleo ya Tanzania ndio jambo la msingi kwako?

Usizingatie sana suala la uwezo wa kutoa hotuba. Sokoine, kiongozi bora, hakuwa mtoaji hotuba.

Kumbuka kwamba ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi.
 
kati ya vitu alivyofanya rais ni kumrejesha Mwandosya kwenye baraza la mawaziri wakati ni mgonjwa na mwandosya pia ameonyesha udhaifu wa kuendelea na kazi wakati mgonjwa hii inaonyesha hata kama angekuwa rais likatokea jambo ambalo lingempasa kuwajibika asingefanya hivyo kwa kweli hazitendei haki kodi zetu tunazolipa vijana wengi wa sasa hivi hawajui kwanini bado tunamzungumzia Marehemu Sokoine kama mfano wa viongozi bora kabisa kuwahi kutokea kwani alipoona ni mgonjwa alijiuzulu na wakati akitibiwa alitumia muda huo kujiendeleza kielimu na alipopona aliweza kulitumikia taifa kwa ufanisi mkubwa lakini Mwandosya akiwemo na mwakyembe walipoumwa hawakumpa fursa rais kuteua watu wa kuziba nafasi zao ili wao wapate muda wa kushugurikia matibabu vizuri hebu tujiulize wizara muhimu kama ya maji inakosa huduma ya waziri mhusika kwa muda karibia miaka miwili inamaanisha nini hii inaonyesha mchango wa mawaziri katika nchi yetu ni wa kisiasa zaidi naomba ieleweke sipingi uwezo wa mwandosya ila tu apumzike ili akipona aweze kutumikia taifa kwa ufanisi
 
Waziri asiye na Wizara Maalum dunia ya leo? Chukulia hata anapotoka nyumban kwake anaagaje; Jaman nakwenda ofcni. Ofic ipi hata yeye hajui

Unajua nina kauli moja kwako, kwamba uko "so naive" kiasi kwamba unasahau hata kutumia common sense. Mwandosya anakuwa Waziri asiye na Wizara maalum katika Ofisi ya Raisi. Hivi unajua katika Ofisi ya Raisi kuna majukumu ya aina ngapi? Hebu sema, kazi za raisi wa nchi ni nini? Sintashangaa ukisema kuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za kitaifa na kukaribisha mabalozi wa nje wapya!
 
Huu ni uzandiki, kama mtu ni mgonjwa si akae pembeni kwani kuna ulazima gani wa kuendelea kuwa waziri... au alivyotoka tumboni kwa mama yake aliahidiwa uwaziri mpaka kifo chake.. huku ni kubebeshana mizigo tu kwa walipa kodi... Mwandosya inampasa akapumzike...
 
Inawezekana kuna busara katika kufanya hivyo, ila usitumie mifano ambayo siyo sahihi. Nyerere hakumpuzisha Sokoine kwa ajili ya Ugonjwa bali Sokoine alikuwa akienda kusoma elimu ya juu ya utawala huko Bulgaria.

Sokoine alikuwa mgonjwa na hili la kusoma lilikuwa la ziada tu. Alipopona hata alitangaza rasmi kwamba sasa yuko fit kwa ajili ya kazi.

Jambo moja ninaloona hapa, ni kwamba kuna watu JF wanaongea kwa kutumia ushabiki badala ya logic. Huko nyuma nimemkosoa sana JK. In fact kwa hili la Baraza la mawaziri namkosoa bado kuondoa mawaziri 6 badala ya 8 kama yalivyokuwa maelewano, ikimaanisha ame-undermine vikao vyote vilivyosema wale 8 waondoke. La Mwandosya simlaumu.

Sasa tukitaka kuendeleza nchi yetu tuache ushabiki. Haya ni mambo ni serious sio kama suala la Simba na Yanga. Kuna watu walioko CCM watabisha tu chochote kinachotoka CDM, na vice versa. Pia wapo watu humu JF kweli wanalalamikia viongozi kwa kuwa wana uchungu na Tanzania. Lakini pia wapo wengine wengi tu wanalalamika tu kwa ajili ya "frustrations" za maisha yao; hata umweke nani kuwa kiongozi, watapata sababu ya kulalamika.

Hata kama CDM wakichukua madaraka - hawa watu watabadilika na kuanza kulalamikia CDM, kwa kuwa wana matatizo katika maisha yao na kulalamika na kulaumu ndio njia pekee ya kutoa hizo "frustration" zao. Hawataki kufanya kazi za kujiendeleza bali wapo kukosoa wengine pasipo sababu za msingi, na wala haimaanishi wao wakipewa hizo nafasi watakuwa waaminifu kuliko hao wanaowalalamikia.

Frustrated minds will complain about everything, whether it makes sense to complain or not. Sasa unfortunately, JF haiwezi kutofautisha watu wa namna hiyo, wawe CCM or CDM au whatever. Wote wana nafasi sawa ya kutoa maoni humu jamvini, na too bad, inabidi tusome maneno yao.
 
Katika watu wanaofahamiana vizuri na JMK ukimwondoa EL nadhani ni huyu Mwandosya. Mwandosya mwenyewe nilimsikia akimsifia JMK kuwa ni mtu sana. Amemsaidia sana kwenye kuugua huku. Tungeambiwa tu kwamba sasa UWAZIRI ni AJIRA.
 
Back
Top Bottom