Kusema ukweli!
Nimefuatilia nimegundua tuko nyuma sana kiakili pamoja na teknolojia! Kwa karne hii sikutegemea uhakiki wa vyeti vya masomo kwa watu (Vetting) uwe kizamani namna hii! Popote ukiomba ajira au panapohitaji uhakiki wa vyeti Tanzania bado tunatumia mbinu ya kizamani sana!
Mfano! Umeomba ajira Dodoma! Utapeleka CV yako wataipitia, then watatuma vyeti vyako chuoni kwa uhakiki kwa sanduku la posta! Mchakato wa kuvituma vyeti chuoni unachukua mwezi, hapo hujazungumzia endapo muombaji kasoma chuo zaidi ya kimoja!
Hapo kunakupotea bahasha au kufika, na endapo ikifika hadi ifunguliwe hapo chuoni kwa Uhakiki wa chuo inaweza fikisha miezi mitatu! Hapo hadi mkuu wa chuo faili limfikie mezani kwake asaini, waandae barua ya kujibu kwenda idara au kampuni husika miezi 6 inapotea!
Na majibu yake hutumwa kwa barua ambapo yanweza kufika au kupotelea njiani! Huu ndiyo utaratibu wa kuhakiki vyeti vya masomo unaotumika hadi Leo Tanzania!
Kwa wenzetu Huko duniani VETTING YA CHETI wanaichukulia serious sana, Wanaamini hayo ni maisha ya mtu, wanaipokea taarifa haraka kama vile taarifa ya msiba, kwamba haiwezi kuzidi masaa 12 kwa wenzetu email zote za VETTING Zinakuwa zimejibiwa
Hapa kwetu bongo sijui nani katuroga wallah! VETTING ya saa 12 inachukua miezi 12 kama vile mtu karudi kusoma tena!
Waziri wa ajira na kazi yupo kimya, kamishina utumishi wala hajigusi, waziri wa elimu na wasaidizi wake wala hawamwambii hilo ni tatizo!
Nimefuatilia nimegundua tuko nyuma sana kiakili pamoja na teknolojia! Kwa karne hii sikutegemea uhakiki wa vyeti vya masomo kwa watu (Vetting) uwe kizamani namna hii! Popote ukiomba ajira au panapohitaji uhakiki wa vyeti Tanzania bado tunatumia mbinu ya kizamani sana!
Mfano! Umeomba ajira Dodoma! Utapeleka CV yako wataipitia, then watatuma vyeti vyako chuoni kwa uhakiki kwa sanduku la posta! Mchakato wa kuvituma vyeti chuoni unachukua mwezi, hapo hujazungumzia endapo muombaji kasoma chuo zaidi ya kimoja!
Hapo kunakupotea bahasha au kufika, na endapo ikifika hadi ifunguliwe hapo chuoni kwa Uhakiki wa chuo inaweza fikisha miezi mitatu! Hapo hadi mkuu wa chuo faili limfikie mezani kwake asaini, waandae barua ya kujibu kwenda idara au kampuni husika miezi 6 inapotea!
Na majibu yake hutumwa kwa barua ambapo yanweza kufika au kupotelea njiani! Huu ndiyo utaratibu wa kuhakiki vyeti vya masomo unaotumika hadi Leo Tanzania!
Kwa wenzetu Huko duniani VETTING YA CHETI wanaichukulia serious sana, Wanaamini hayo ni maisha ya mtu, wanaipokea taarifa haraka kama vile taarifa ya msiba, kwamba haiwezi kuzidi masaa 12 kwa wenzetu email zote za VETTING Zinakuwa zimejibiwa
Hapa kwetu bongo sijui nani katuroga wallah! VETTING ya saa 12 inachukua miezi 12 kama vile mtu karudi kusoma tena!
Waziri wa ajira na kazi yupo kimya, kamishina utumishi wala hajigusi, waziri wa elimu na wasaidizi wake wala hawamwambii hilo ni tatizo!