ndandawamalenja
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 472
- 347
UTAPELI UNAOFANYWA NA HESLB KWA UZEMBE NA UOGA WA WAAJIRI WETU
1. Mtu ulimaliza kulipa mkopo wa elimu ya juu miaka kumi iliyopita (2012)
2. Mwaka 2023 unapata barua kutoka kwa mwajiri wako kuwa unadaiwa na HESLB utaanza kukatwa mshahara kulipa deni hilo.
3. Ukiwa bado unajadili na mwajiri wako pesa walizokukata kwa ajili ya deni la HESLB, mwezi unaofuata unakatwa asilimia 15 ya mshahara ghafi (mwajiri anapeleka tena makato kwa sababu HESLB wamemwagiza kufanya hivo). Na ni mwajiri huyo huyo alikukata pesa za deni la HESLB mpaka likaisha na salary slip zote alizokupa zinaonyesha hivyo. Pesa hiyo, mfano, laki mbili na elfu ishirini na tano (225,000) ambayo ni 15% ya 1,500,000 inakatwa bila kujali makato mengine yoyote yanayoendelea, mfano mikopo uliyochukua baada ya kumaliza deni la HESLB.
4. Unaenda HESLB kuuliza kulikoni mbona haudaiwi imekuwaje wameagiza ukatwe mshahara na mwajiri amekukata, wanakwambia ni kweli deni lako ulimaliza kulipa miaka 10 iliyopita ila makato hayo hayakuingia kwenye system ya HESLB, yaani umekatwa kimakosa. (Umeadhibiwa kwa kosa sio lako).
5. Wanakushauri uombe kurejeshewa pesa zako kupitia mtandao wa HESLB.
6. Unaingia kuomba. Unafikia hatua fulani ambayo hauwezi kuvuka (wanajua kabisa hautavuka) kwa sababu kuna kikwazo. Kwa makusudi wamefanya taarifa fulani ya hatua hiyo isikubali kuingia kwenye mfumo, mfano jina la mwajiri wako halipo kwenye menu, hivyo huwezi kuvuka kwenda hatua inayofuata kwa sababu button ya NEXT itakuwa inactive. Na wamemtoa mwajiri wako makusudi kwa sababu mwezi huo wanakuwa wamekata watu wengi pesa “KIMAKOSA” (Ambayo ni makusudi). Kwa hiyo wanazuia hao waliokatwa wasiombe refund. (KWA MAKUSUDI)
Pesa yako inakuwa imeenda mpaka wakati watakaoamua wao kuingiza jina la mwajiri wako kwenye list (Au kuondoa kikwazo walichoweka makusudi ili ukwame) ili uweze kuvuka hiyo hatua mpaka ufike hatua ya kusubmit madai yako ya refund.
Utasubiri siku 90 kurejeshewa pesa zako baada ya kuwa system ilikukubalia kusubmit maombi yako ya refund.
Najiuliza maswali mengi. Hizi pesa zinaendaga wapi? Kuna watu wengi wanakata tamaa ya kuatilia hizi pesa, hasa kama kiasi kilichokatwa hakiathiri sana bajeti zao, pesa zao zinaendaga wapi na zinaripotiwa vipi? Yaani serikali yetu haioni inatuumiza wafanyakazi wake kwa makusudi kabisa?
Halafuuu, kwanini waajiri hawatujali kiasi hiki? Deni nilimaliza kulipa na wewe ndio ulinikata hizo pesa ukapeleka ninakodaiwa mpaka deni likaisha. Mdai wangu anarudi tena kusema ananidai, naleta mpaka uthibitisho wa salary slip kwako kuonyesha kuwa huyo mtu hanidai, wewe unanikata tu pesa unampa tena! Halafu unasema nikalete barua kutoka kwa mdai wangu inayosema nisikatwe mshahara kwa sababu deni nilimaliza kulipa!! This strange country.
Yeyote anaye-engineer huu uovu alaaniwe mpaka kizazi chake cha kumi. Na kuna siku tutapata wa kututetea tu. Kila jambo lina mwisho wake.
1. Mtu ulimaliza kulipa mkopo wa elimu ya juu miaka kumi iliyopita (2012)
2. Mwaka 2023 unapata barua kutoka kwa mwajiri wako kuwa unadaiwa na HESLB utaanza kukatwa mshahara kulipa deni hilo.
3. Ukiwa bado unajadili na mwajiri wako pesa walizokukata kwa ajili ya deni la HESLB, mwezi unaofuata unakatwa asilimia 15 ya mshahara ghafi (mwajiri anapeleka tena makato kwa sababu HESLB wamemwagiza kufanya hivo). Na ni mwajiri huyo huyo alikukata pesa za deni la HESLB mpaka likaisha na salary slip zote alizokupa zinaonyesha hivyo. Pesa hiyo, mfano, laki mbili na elfu ishirini na tano (225,000) ambayo ni 15% ya 1,500,000 inakatwa bila kujali makato mengine yoyote yanayoendelea, mfano mikopo uliyochukua baada ya kumaliza deni la HESLB.
4. Unaenda HESLB kuuliza kulikoni mbona haudaiwi imekuwaje wameagiza ukatwe mshahara na mwajiri amekukata, wanakwambia ni kweli deni lako ulimaliza kulipa miaka 10 iliyopita ila makato hayo hayakuingia kwenye system ya HESLB, yaani umekatwa kimakosa. (Umeadhibiwa kwa kosa sio lako).
5. Wanakushauri uombe kurejeshewa pesa zako kupitia mtandao wa HESLB.
6. Unaingia kuomba. Unafikia hatua fulani ambayo hauwezi kuvuka (wanajua kabisa hautavuka) kwa sababu kuna kikwazo. Kwa makusudi wamefanya taarifa fulani ya hatua hiyo isikubali kuingia kwenye mfumo, mfano jina la mwajiri wako halipo kwenye menu, hivyo huwezi kuvuka kwenda hatua inayofuata kwa sababu button ya NEXT itakuwa inactive. Na wamemtoa mwajiri wako makusudi kwa sababu mwezi huo wanakuwa wamekata watu wengi pesa “KIMAKOSA” (Ambayo ni makusudi). Kwa hiyo wanazuia hao waliokatwa wasiombe refund. (KWA MAKUSUDI)
Pesa yako inakuwa imeenda mpaka wakati watakaoamua wao kuingiza jina la mwajiri wako kwenye list (Au kuondoa kikwazo walichoweka makusudi ili ukwame) ili uweze kuvuka hiyo hatua mpaka ufike hatua ya kusubmit madai yako ya refund.
Utasubiri siku 90 kurejeshewa pesa zako baada ya kuwa system ilikukubalia kusubmit maombi yako ya refund.
Najiuliza maswali mengi. Hizi pesa zinaendaga wapi? Kuna watu wengi wanakata tamaa ya kuatilia hizi pesa, hasa kama kiasi kilichokatwa hakiathiri sana bajeti zao, pesa zao zinaendaga wapi na zinaripotiwa vipi? Yaani serikali yetu haioni inatuumiza wafanyakazi wake kwa makusudi kabisa?
Halafuuu, kwanini waajiri hawatujali kiasi hiki? Deni nilimaliza kulipa na wewe ndio ulinikata hizo pesa ukapeleka ninakodaiwa mpaka deni likaisha. Mdai wangu anarudi tena kusema ananidai, naleta mpaka uthibitisho wa salary slip kwako kuonyesha kuwa huyo mtu hanidai, wewe unanikata tu pesa unampa tena! Halafu unasema nikalete barua kutoka kwa mdai wangu inayosema nisikatwe mshahara kwa sababu deni nilimaliza kulipa!! This strange country.
Yeyote anaye-engineer huu uovu alaaniwe mpaka kizazi chake cha kumi. Na kuna siku tutapata wa kututetea tu. Kila jambo lina mwisho wake.