Utani na Msichana ninaye fanya naye kazi unataka kunivunjia ndoa yangu

ukome!
Yaani nimepata hasira mpaka na-vibrate!
Utani gani huo, je ingekua ni mkeo anataniwa hvyo na kidume cha ofsn kwake ungejisikiaje?
Kila uhusiano una mipaka ww na huyo mate wako hamna mipaka? Hv ingekua wife hajaiona msg ungemjibu vp mate wako?
 
ingekuwa ni mm, kwanza kama kweli huyo rafiki wa ofisi hatuna mahusiano na ni rafiki kweli nitamuomba tuongozane nyumbani, aongee na mamsap wangu ili ukweli ujulikane....
si ana simu alyotumia kunitext? tutaona sent items au namba zake zitaprove. ila kama atakataa kwenda, nitajua hakuwa rafiki ila alkuwa na nia nyingine kwangu. Ila pole sana..
 
sasa meku...shimbonyi shafoo...sasa aisee kwanini aisee unaleta utani kwenye ndoa aisee mekuuu....halafu inaonekana wife ni mkali sana aisee mana unaogopa kabi kabisa kumsogelea na kumueleza ukweli....sasa aisee umeshalala gesti utamueleza vipi hukulala kwa huyo malaya wako aisee...rudi ho home mueleze banaaa kwa utaratibu atakuelewa.....acha kuwa lege lege mekuu. pole sana aisee
 
rudi nyumbani mkayazungumze...... utaishi hotel mpaka lini.....unavyozidi kuwa nje ya nyumbani unazidi kuharibu
 
Hata mimi nawaambiaga rafiki zangu hakuna utani kati ya mtoto wa kike na wa kiume wananiona mnoko. Mimi ukimtania mume wangu sikukopeshi. Wanaanzaga hivo hivo! Singles wameisha mpaka ukatanie mume/mke wa mtu. Eti umwite mume wangu honey! We! SItakuelewa kabisa nakuweka kwenye wanted list yangu!

Ni obvious hizo ni dalili za kunyemeleana. Utani my foot. Utakuta mijitu inaongea mambo ya chumbani kabisa tena wanaongelea wake na waume zao kwa hao the so called watani. Mimi uwa nawacheki, kimoyo moyo nasema ole wenu mumtanie mume wangu. NAWATOA NISHAI LIVE. Tunaona watu wa hivo makazini na in most cases ni wale maharage ya mbeya ndio wanapenda mambo ya utani. Ikitokea ukabug step tu unalo. UKIMWI UTATUMALIZA.

Pole sana mkuu,
Ulipokosea wewe ni kuondoka nyumbani. Rudi nyumbani haraka na umuombe msamaha maana hilo ni kosa. Hata mimi mkuu yamesha nikumba hayo hayo na imenifanya sasa niache kabisa mizaha na watoto wa kike. hawa viumbe siku hizi hawataniwi wamekuwa kama maharage ya mbeya maji mara moja.
Pole sana mkuu,
 
Kuna mdada mmoja ofisini ni dirvocee huwa namsikia anaongea na waume za watu kwenye phone, yaani napata hasira on behalf. Anaongelea mambo ya faragha kabisa so tempting. Afu akimaliza anasema huyu kijana tunatanianaga. Ni full matusi. Ni sawa na kuangalia movie za X na mume/mke wa mtu. Maanake asojua kuwa matani yanaamasisha nani?
 
Kuna msichana nafanya naye kazi katika kampuni moja. Sasa tumezoea kweli kutaniana na kuitana majina ya Kimahaba huku kukiwa hakuna uhusiano wowote wa Kimapenzi. Jana saa nne usiku nikiwa nafanya kazi zangu kwenye kompyuta sebuleni na simu ikiwa chumbani akanitumia ujumbe unaosomeka "Honey, its too cold today, I wish you could be beside me now, I cant Imagine how the situation could be". Aisee, mama watoto alikuwa kajipumzikia kitandani huyoo akaamka na kwenda mezani, akachukua simu na kusoma meseji. Kilichojiri hapo nilisikia mlango wa chumbani umefunguliwa, baadaye nikasikia paa, nimepigwa kofi zito la shavuni. Nilipozinduka nikamkuta analia, akaniambia haya twende chumbani ukavae uende ukampe joto huyo malaya wako. Nikasita, nikapigwa tena kofi la begani na kuambiwa nyanyukaaaa, malaya mkubwa wewe. Unataka kuniuwa niache watoto wanakula shida na malaya zako. Kwa kweli ilikuwa ni zengwe sana. na leo nimemkia hotel, baada ya kuona vurugu inataka kuanza kushirikisha majirani. Wife amekataa kabisa kunielewa, leo nimempigia simu hapokei, meseji hajibu binti nimemueleza yaliyonikuta kwa sababu ya ushenzi wake anachekacheka tu, natamani nimmeze kwa kweli. Natafakari nielekee wapi nkitoka hapa kazini.Nawasilisha kwa ushauri.

damn!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!stpid husband
 
Kuna msichana nafanya naye kazi katika kampuni moja. Sasa tumezoea kweli kutaniana na kuitana majina ya Kimahaba huku kukiwa hakuna uhusiano wowote wa Kimapenzi. Jana saa nne usiku nikiwa nafanya kazi zangu kwenye kompyuta sebuleni na simu ikiwa chumbani akanitumia ujumbe unaosomeka "Honey, its too cold today, I wish you could be beside me now, I cant Imagine how the situation could be". Aisee, mama watoto alikuwa kajipumzikia kitandani huyoo akaamka na kwenda mezani, akachukua simu na kusoma meseji. Kilichojiri hapo nilisikia mlango wa chumbani umefunguliwa, baadaye nikasikia paa, nimepigwa kofi zito la shavuni. Nilipozinduka nikamkuta analia, akaniambia haya twende chumbani ukavae uende ukampe joto huyo malaya wako. Nikasita, nikapigwa tena kofi la begani na kuambiwa nyanyukaaaa, malaya mkubwa wewe. Unataka kuniuwa niache watoto wanakula shida na malaya zako. Kwa kweli ilikuwa ni zengwe sana. na leo nimemkia hotel, baada ya kuona vurugu inataka kuanza kushirikisha majirani. Wife amekataa kabisa kunielewa, leo nimempigia simu hapokei, meseji hajibu binti nimemueleza yaliyonikuta kwa sababu ya ushenzi wake anachekacheka tu, natamani nimmeze kwa kweli. Natafakari nielekee wapi nkitoka hapa kazini.Nawasilisha kwa ushauri.
Wahi Loliondo tu mkuu
 
Kuna mdada mmoja ofisini ni dirvocee huwa namsikia anaongea na waume za watu kwenye phone, yaani napata hasira on behalf. Anaongelea mambo ya faragha kabisa so tempting. Afu akimaliza anasema huyu kijana tunatanianaga. Ni full matusi. Ni sawa na kuangalia movie za X na mume/mke wa mtu. Maanake asojua kuwa matani yanaamasisha nani?
Tena kama wewe nyumba kubwa, mumeo ndiyo rahisi kwelikweli! basi tu hujui
 
mrs mkali hivyo.huyo dada wa ofisini ulimzoesha vibaya,matokeo yake umelikoroga.mpe muda mke wako,muelezee hali halisi,ingawa itachukuwa muda sana kukuamini.maana msg ni ushahidi tosha,haijalishi kama mnataniana au hamtaniani,maana kwa hayo maneno,hata mimi ningehisi huyo ni mpenzi wako tu.na huyo dada muambie kuanzia leo,wewe na yeye matani basi,hata ofisini msitaniane,sio kwa huyo tu,hata kwa wasichana wowote wale,wewe sasa umeoa, jaribu kujiwekea mipaka unapozungumza na wasichana wengine.maana wadada wengine ukimregezea kidogo,kosa kama hilo linaweza kutokea au zaidi ya hilo
 
huyo binti anakutaka ila wewe unaona ni kama mzaha, fanya uamuzi haraka wa kutojibu au kupokea simu zake na pia mwambie masihara yenu yafike kikomo au yaishie huko huko ofisini, itafika wakati mke wako anaweza choka na hayo anayoyaona na akaamua nae kufanya yale anayodhani wewe unayafanya. KUWA MAKINI ...UIKIMWI UNAUA!

Sio aishie ofisini tu! Yaani aache kabisa utani na huyo binti. Watu wengine hawataniwi ati! Kwa mtu anayejua kuwa huyu ni mmilikiwa wa mtu utani huishia mkitoka mjengoni mnakopiga mzigo. Kaa naye mbali ana dhamira ya kuwa mama mwenye nyumba babu!
 
Mimi nimeshtuka kusikia hivyo ila kwa sababu sina facts nimebaki kuguna tu!!!
Asavali umesema...one of my investments ni mmachame sasa nlishaanza kuogopa.

mmeambiwa mtalijua Lima kilimanjaro nyie sio Jiji tena....Huyo kaoa Bondia acha akome...umeoa Bondia unataka kuchakachua?
 
mrs mkali hivyo.huyo dada wa ofisini ulimzoesha vibaya,matokeo yake umelikoroga.mpe muda mke wako,muelezee hali halisi,ingawa itachukuwa muda sana kukuamini.maana msg ni ushahidi tosha,haijalishi kama mnataniana au hamtaniani,maana kwa hayo maneno,hata mimi ningehisi huyo ni mpenzi wako tu.na huyo dada muambie kuanzia leo,wewe na yeye matani basi,hata ofisini msitaniane,sio kwa huyo tu,hata kwa wasichana wowote wale,wewe sasa umeoa, jaribu kujiwekea mipaka unapozungumza na wasichana wengine.maana wadada wengine ukimregezea kidogo,kosa kama hilo linaweza kutokea au zaidi ya hilo

huyu jamaa anaye Chele...wewe umeoa unataniana na mtu kweli kihivyo? mie mfanyakazi mwenzangu tu kuniita kimahabahaba mwiko...sijui honey sijui switie helll NOOOOOOOO....halafu anajua kabisa niko home, mbele ya my wife wangu anatuma MSG kama hiyo? Walah ndoa yangu inatetemeka yeye sijui itakuwaje? Walah atakuja niombea msamaha...
 
Kuna mdada mmoja ofisini ni dirvocee huwa namsikia anaongea na waume za watu kwenye phone, yaani napata hasira on behalf. Anaongelea mambo ya faragha kabisa so tempting. Afu akimaliza anasema huyu kijana tunatanianaga. Ni full matusi. Ni sawa na kuangalia movie za X na mume/mke wa mtu. Maanake asojua kuwa matani yanaamasisha nani?

Contact zake mie sitamtania...nitamwambia ukweli....
 
Sio aishie ofisini tu! Yaani aache kabisa utani na huyo binti. Watu wengine hawataniwi ati! Kwa mtu anayejua kuwa huyu ni mmilikiwa wa mtu utani huishia mkitoka mjengoni mnakopiga mzigo. Kaa naye mbali ana dhamira ya kuwa mama mwenye nyumba babu!

Utani ni live tu sio kwa msg tena....Niite majina yote lkn sio uniandikie maana written ni ushahidi tosha...mama kaisave text msg akibisha tu, linawekwa live...
 
Kwanza pole,pili mwache kwa muda hasira zikipungua umwambie,jaribu kuwashirikisha watu anaowaheshimu,akishindwa kukuelewa hayo yatakuwa nje ya uwezo wako!Huwezi kubadili hali halisi mzee!
 
Utani gani saa nne ucku? Au hajui kuwa una mke? Lakini mangi mkeo ndio angetumiwa hiyo msg akakwambia utani ungeelewa? Hukupaswa kuondoka home hata kama moto ungewaka vp,rudi home muombe radhi mkeo,siku ukiona hasira zake zimepungua mweleze hali halisi ilivyokuwa. Huyo bint mkumbushe jina lako la kwenye passport na formality ihusike from 2day on wards.
 
Situation kama hizi inabidi huwe mwepesi wa kufikiri....,
ungecheka saaana alafu ukasema kumbe kweli unanipenda.., yaani umeshinda mtego, tulipanga na rafiki yangu tukupime.., hivi kweli wife ningekuwa nategemea sms kama hiyo unadhani ningeacha simu chumbani.., dah kumbe mshikaji alisema kweli mi nilisema wife hawezi kukubali mtego mdogo hivi..., dah wife embu twende tukalale......
 
Back
Top Bottom