Mangi Moshi
Member
- Jun 21, 2011
- 22
- 11
Kuna msichana nafanya naye kazi katika kampuni moja. Sasa tumezoea kweli kutaniana na kuitana majina ya Kimahaba huku kukiwa hakuna uhusiano wowote wa Kimapenzi. Jana saa nne usiku nikiwa nafanya kazi zangu kwenye kompyuta sebuleni na simu ikiwa chumbani akanitumia ujumbe unaosomeka "Honey, its too cold today, I wish you could be beside me now, I cant Imagine how the situation could be". Aisee, mama watoto alikuwa kajipumzikia kitandani huyoo akaamka na kwenda mezani, akachukua simu na kusoma meseji. Kilichojiri hapo nilisikia mlango wa chumbani umefunguliwa, baadaye nikasikia paa, nimepigwa kofi zito la shavuni. Nilipozinduka nikamkuta analia, akaniambia haya twende chumbani ukavae uende ukampe joto huyo malaya wako. Nikasita, nikapigwa tena kofi la begani na kuambiwa nyanyukaaaa, malaya mkubwa wewe. Unataka kuniuwa niache watoto wanakula shida na malaya zako. Kwa kweli ilikuwa ni zengwe sana. na leo nimemkia hotel, baada ya kuona vurugu inataka kuanza kushirikisha majirani. Wife amekataa kabisa kunielewa, leo nimempigia simu hapokei, meseji hajibu binti nimemueleza yaliyonikuta kwa sababu ya ushenzi wake anachekacheka tu, natamani nimmeze kwa kweli. Natafakari nielekee wapi nkitoka hapa kazini.Nawasilisha kwa ushauri.