Sinkala
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 1,773
- 684
Nimekuwa nikiona baadhi ya watuhumiwa wakiwa wameshikiliwa au kusindikizwa chini ya ulinzi wa wa askari wanaoitwa "Askari Kanzu". Juzi juzi mitaa ya barabara ya Nyerere maeneo ya njia panda Segerea nimeshashuhudia defender ikiwa inapita mitaani huku ikibeba watu waliovalia kiraia wakiwa nyuma ya gari huku wakishikilia silaha na kuyaamuru magari mengine yawapishe kwani gari lao lilikuwa katika mwendo wa kasi kama vile wanawahi tukio fulani. Nilipouliza watu pale nikaambiwa hao ni askari kanzu.
Nilipoangalia namba za usajili za gari lile niliona ni za kawaida tu (T nnn XXX), sio za magari ya Police (PT XXX). Sasa nilijiuliza maswali, hawa jamaa wamevalia kiraia, na gari lao lina namba za kiraia, lakini wameshika bunduki wakiwa katika mwendo wa kasi. Je, majambazi hawawezi kuwa katika hali waliyokuwa nayo wale askari kanzu?
Kauli mbiu ya jeshi la Polisi inayoitwa Polisi jamii itatekelezwaje iwapo mimi sijui nani ni askari na nani ni jambazi? Naombeni mnisaidie ninyi mnatumia njia gani kuwatambua askari kanzu.
Nilipoangalia namba za usajili za gari lile niliona ni za kawaida tu (T nnn XXX), sio za magari ya Police (PT XXX). Sasa nilijiuliza maswali, hawa jamaa wamevalia kiraia, na gari lao lina namba za kiraia, lakini wameshika bunduki wakiwa katika mwendo wa kasi. Je, majambazi hawawezi kuwa katika hali waliyokuwa nayo wale askari kanzu?
Kauli mbiu ya jeshi la Polisi inayoitwa Polisi jamii itatekelezwaje iwapo mimi sijui nani ni askari na nani ni jambazi? Naombeni mnisaidie ninyi mnatumia njia gani kuwatambua askari kanzu.