Usipite bila kusema shukurani hizi kwa Mungu / Allah kwa mwaka 2020

PMWAKA

Senior Member
Aug 29, 2019
191
206
Should we thank GOD/ ALLAH

prayer2.jpg
?!

Mungu vinywa vyetu vimejawa na maneno ya Shukrani.

Tunashukuru kwa ajili ya 2020, umekua nasi January mpaka December.

Asante kwa yale ambayo umekwisha kuyafanya, asante kwa yale ambayo bado hujayafanya, asante kwa yale ambayo umefanya kwa sehemu tuu, Tunaomba tunda la uvumilivu likajae kwa wingi ndani yetu na kutuandaa kupokea yale uliyokusudia kwa mwaka ujao.,

Nyakati za usiku tukiwa hatujitambui, hukulala wala kusinzia, ulitulinda na ulitupa nafasi nyingine ya kuona siku mpya.

Tukiwa barabarani, ulituepusha na ajali, katika biashara zetu hatukupungukiwa bali Bwana ulitusaidia tukapata kwa sehemu.

Katika huduma zenu, tumeona Neema yako ikituongoza na kutusaidia kujua tunachopaswa kufanya kwa wakati na majira fulani.

Mbingu hazijawahi kunyamaza na kuacha kutusikia, tumeshuhudia ukitushika mkono na kutuvusha, tumeshuhudia ukituganga mioyo kwenye nyakati ngumu, tumeshuhudia ukituzungushia watu wanaotusababisha tuone bado ipo sababu ya kukuamini.

Katika utafutaji wetu, kuna nyakati tulikosa kabisa lakini wewe Baba hukutuacha tulale njaa, bado ulionyesha vile ulivyo mwaminifu na wa haki.

Tukiwa masomoni, kuna nyakati ada zilisumbua, tukahisi hatutamaliza masomo, lkn Bwana uaminifu wako hatuwezi kuelezea, hata sasa umetusaidia, tumeuona mkono wako.

Kuna nyakati upatikanaji wa kodi ulikua mgumu, lakini tunakushukuru hatukuwahi kulala nje, tukapigwa na jua wala mvua.

Kuna nyakati tulipoteza nuru katika nyuso zetu, lakini hukuacha kututia moyo na kutushika mkono, kuna nyakati hatukuona sabb za kuishi kwasbb ya yale tunayoyapitia lakini wewe Mungu hukuacha kusema nasi kwa namna fulani.

Yapo tuliyoyaomba, tunaona yamechelewa kibinadamu, lkn tunajua ipo siku yatatimia na tutajawa na kelele za shangwe.

Tuliomba mtaji, ukatupatia, tuliomba afya njema, ukatupatia, umetuhurumia, umetutetea, umetupenda kwa uvumilivu.

TUSEME NINI Mungu, zaidi ya KUKUSHUKURU..
Pokea sifa hizi Mfalme wa wafalme..
Tunakurudishia sifa, heshima, utukufu na adhama, UNASTAHILI MFALME...!
 

Attachments

  • bhuh.jpg
    bhuh.jpg
    8.3 KB · Views: 1
Should we thank GOD/ ALLAH?

Mungu vinywa vyetu vimejawa na maneno ya Shukrani.

Tunashukuru kwa ajili ya 2020, umekua nasi January mpaka December.

Asante kwa yale ambayo umekwisha kuyafanya, asante kwa yale ambayo bado hujayafanya, asante kwa yale ambayo umefanya kwa sehemu tuu, Tunaomba tunda la uvumilivu likajae kwa wingi ndani yetu na kutuandaa kupokea yale uliyokusudia kwa mwaka ujao.,

Nyakati za usiku tukiwa hatujitambui, hukulala wala kusinzia, ulitulinda na ulitupa nafasi nyingine ya kuona siku mpya.

Tukiwa barabarani, ulituepusha na ajali, katika biashara zetu hatukupungukiwa bali Bwana ulitusaidia tukapata kwa sehemu.

Katika huduma zenu, tumeona Neema yako ikituongoza na kutusaidia kujua tunachopaswa kufanya kwa wakati na majira fulani.

Mbingu hazijawahi kunyamaza na kuacha kutusikia, tumeshuhudia ukitushika mkono na kutuvusha, tumeshuhudia ukituganga mioyo kwenye nyakati ngumu, tumeshuhudia ukituzungushia watu wanaotusababisha tuone bado ipo sababu ya kukuamini.

Katika utafutaji wetu, kuna nyakati tulikosa kabisa lakini wewe Baba hukutuacha tulale njaa, bado ulionyesha vile ulivyo mwaminifu na wa haki.

Tukiwa masomoni, kuna nyakati ada zilisumbua, tukahisi hatutamaliza masomo, lkn Bwana uaminifu wako hatuwezi kuelezea, hata sasa umetusaidia, tumeuona mkono wako.

Kuna nyakati upatikanaji wa kodi ulikua mgumu, lakini tunakushukuru hatukuwahi kulala nje, tukapigwa na jua wala mvua.

Kuna nyakati tulipoteza nuru katika nyuso zetu, lakini hukuacha kututia moyo na kutushika mkono, kuna nyakati hatukuona sabb za kuishi kwasbb ya yale tunayoyapitia lakini wewe Mungu hukuacha kusema nasi kwa namna fulani.

Yapo tuliyoyaomba, tunaona yamechelewa kibinadamu, lkn tunajua ipo siku yatatimia na tutajawa na kelele za shangwe.

Tuliomba mtaji, ukatupatia, tuliomba afya njema, ukatupatia, umetuhurumia, umetutetea, umetupenda kwa uvumilivu.

TUSEME NINI Mungu, zaidi ya KUKUSHUKURU..
Pokea sifa hizi Mfalme wa wafalme..
Tunakurudishia sifa, heshima, utukufu na adhama, UNASTAHILI MFALME...!
 
Licha ya maswahibu na hasara toka January ,stress za ndoa,familia,ukooo n.k....... NAKUSHUKURU YESU WANGU KWA AFYA YA ROHO,MWILI NA AKILI ULIONIPATIA,MAANA NAAMINI NTAONGEZEWA MARA ELFU ZISIPOZIMIA ROHO
 
Asante sana Mungu wewe ndio muweza wa yote nakushukuru sana kwa kila jambo "Ameeen"
 
Najiunganisha na Maombi Haya ya Shukrani,Simba Wa Kabila ya Yuda,Yehova,Elshadai Onekana Kwetu Kama Ulivyoonekana Bahari ya Shamu Ukiwavusha Wana Wa Israel,Tuvushe Eeh Baba 2021,Onyesha Ukuu Wako Yehova,Pigana na Hila Zote Za mwovu ibilisi na mipango yake miovu kwetu,Simama Nami Eeh Bwana,Simama na Asomae Sasa,Pigania Familia Yangu,Koo,Kabila,Taifa na Dunia Nzima Eeh Bwana,Wape Viongozi Wetu Hekima Kama Ya Suleiman.

Unayeishi na Kutawala,Tusamehe Makosa Yetu,Pigana na Afya Zetu,Biashara,Kazi,Masomo,Safari Zetu,Na Kila Nukta ya Pumzi Tuivutayo Yenye Kibali Mbele Zako.

Onekana Tena Eeh Baba,Wale Waliokata Tamaa Wainue Tena Yehova,Tuonyeshe Njia Baba,Na Roho Wako Atuongoze Kutenda Ya Kukupendeza Mungu Wangu.

Katika Haya Machache Ninaomba Na Kukushukuru,Amen.........!!
 
Back
Top Bottom