ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Hata kama huko ibadani wenzio wanakushangaa kwa nini unaenda kusali peke yako, fahamu kuwa suala la imani ni la kibinafsi zaidi na kwenda kwako mbinguni kutategemea na matendo yako.
Kuna mdada amekuwa akimshinikiza mumewe aokoke kama yeye, lakini mume amekuwa hataki kufanya hivyo na kuamua aendelee kuwa ktk imani yake ya awali waliyokuwanayo awali kabla ya mke kuokoka. Sasa mke anajisikia vibaya kuona anaishi na mume ambaye sio mlokole na inaonekana kuna shinikizo toka kwa waumini wenzake kuhusu hilo.
Hali hiyo imeanza kupelekea mume kuona nyumba yake kuwa kama 'jela' kwani mke anaona kama anaishi na shetani, na mume anaona kero muda wote kuimbiwa wimbo wa kuokoka na mkewe.
Hali hiii imemfanya mume kuachelewa kurudi nyumbani ili muda uende akirudi akute usiku umeenda na mke kalala walau amani iwepo na makelele yapungue. Ukiangalia hapo ni kama ndoa inaelekea kuanza kuharibika maana 'akili' za wanaume huwa hazichelewi.
Angalizo: Kina mama ni kweli nyinyi ni wepesi kujifunza na kutenda yale yanayowapa furaha moyoni. Kuweni makini na ndoa zenu, msisumbue waume zenu kisa eti hawajaokoka. "Mwanamke mpumbavu huivunja 'nyumba' yake kwa mikonoye".
Kuna mdada amekuwa akimshinikiza mumewe aokoke kama yeye, lakini mume amekuwa hataki kufanya hivyo na kuamua aendelee kuwa ktk imani yake ya awali waliyokuwanayo awali kabla ya mke kuokoka. Sasa mke anajisikia vibaya kuona anaishi na mume ambaye sio mlokole na inaonekana kuna shinikizo toka kwa waumini wenzake kuhusu hilo.
Hali hiyo imeanza kupelekea mume kuona nyumba yake kuwa kama 'jela' kwani mke anaona kama anaishi na shetani, na mume anaona kero muda wote kuimbiwa wimbo wa kuokoka na mkewe.
Hali hiii imemfanya mume kuachelewa kurudi nyumbani ili muda uende akirudi akute usiku umeenda na mke kalala walau amani iwepo na makelele yapungue. Ukiangalia hapo ni kama ndoa inaelekea kuanza kuharibika maana 'akili' za wanaume huwa hazichelewi.
Angalizo: Kina mama ni kweli nyinyi ni wepesi kujifunza na kutenda yale yanayowapa furaha moyoni. Kuweni makini na ndoa zenu, msisumbue waume zenu kisa eti hawajaokoka. "Mwanamke mpumbavu huivunja 'nyumba' yake kwa mikonoye".