Usiende Kwenye Usaili (Job Interview) Kabla ya Kusoma Kitabu Hiki (na Vinginevyo)

Shimba ya Buyenze

JF-Expert Member
Dec 22, 2014
178,275
1,077,680
Kitabu hiki ni kizuri. Mimi binafsi kilinisaidia katika interview yangu ya tatu baada ya kuwa nimeboronga katika interview zangu mbili za kwanza. Ndiyo nilikuwa nimemaliza chuo na kazi ya kwanza ndiyo hasa niliitaka lakini nilikutana na vijana wenzangu kutoka Kenya na Nigeria nikajua tu waziwazi kuwa hapa sitoboi maana wenzangu walikuwa wamejiandaa kweli kweli. Baada ya kusoma kitabu hiki nilipata picha halisi ya ninachotakiwa kufanya katika interview yangu ya tatu na nilikwenda kwa kujiamini sana maana nilikuwa nimejua mambo ya msingi. Mifano ya majibu ya maswali ya kawaida yanayoulizwa katika interview nyingi yaliyomo kwenye kitabu hiki pia yalinisaidia sana. Na nilipata hiyo kazi!

Najua ukiritimba uliopo katika ajira hapa kwetu. Kuna mambo ya kujuana (nepotism), rushwa (za kila aina) na connection. Pamoja na yote haya naamini utafaidika na yaliyomo katika kitabu hiki katika ujumla wake. Na watakaofaidika zaidi ni wale watakaoomba kazi katika mashirika ya kimataifa ambako pengine mambo ya kujuana, rushwa na connection hayana nafasi kubwa sana kama huku kwingine. Usiende huko tu kichwa kichwa. Soma kitabu hiki kwa uangalifu. Zingatia yale mambo ya msingi. Jiamini na mengine mwachie Mungu!

Nitaongezea na vingine viwili au vitatu hivi vyenye mitazamo tofauti tofauti huko mbele ya safari. Kila la heri kwa vijana mnaotafuta kazi. Kama kitabu hiki kitamsaidia japo kijana mmoja kwa namna moja au nyingine kupata kazi basi, lengo langu litakuwa limekamilika. Endeleeni kupambana kwa kadri inavyowekana na kamwe msikate tamaa. Ndivyo maisha yalivyo!​
Everything Job Interview Book.jpg
 

Attachments

  • The Everything Job Interview Question Book The Best Answers to the Toughest Interview Questions.pdf
    1.5 MB · Views: 90
Naona nikiongezee na hiki hapa moja kwa moja. Hiki kina mifano ya majibu 301 ya maswali yanayopenda kuulizwa sana katika usaili. Siyo ukariri majibu haya lakini ni mwongozo tu wa kuona jinsi maswali mbalimbali (yakiwemo yale ya msingi "Mf. Tell me a little bit about yourself" yanavyopaswa kujibiwa.
 

Attachments

  • 301 Smart Answers to Tough Interview Questions.pdf
    1.4 MB · Views: 62
Kitabu hiki ni kizuri. Mimi binafsi kilinisaidia katika interview yangu ya tatu baada ya kuwa nimeboronga katika interview zangu mbili za kwanza. Ndiyo nilikuwa nimemaliza chuo na kazi ya kwanza ndiyo hasa niliitaka lakini nilikutana na vijana wenzangu kutoka Kenya na Nigeria nikajua tu waziwazi kuwa hapa sitoboi maana wenzangu walikuwa wamejiandaa kweli kweli. Baada ya kusoma kitabu hiki nilipata picha halisi ya ninachotakiwa kufanya katika interview yangu ya tatu na nilikwenda kwa kujiamini sana maana nilikuwa nimejua mambo ya msingi. Mifano ya majibu ya maswali ya kawaida yanayoulizwa katika interview nyingi yaliyomo kwenye kitabu hiki pia yalinisaidia sana. Na nilipata hiyo kazi!

Najua ukiritimba uliopo katika ajira hapa kwetu. Kuna mambo ya kujuana (nepotism), rushwa (za kila aina) na connection. Pamoja na yote haya naamini utafaidika na yaliyomo katika kitabu hiki katika ujumla wake. Na watakaofaidika zaidi ni wale watakaoomba kazi katika mashirika ya kimataifa ambako pengine mambo ya kujuana, rushwa na connection hayana nafasi kubwa sana kama huku kwingine. Usiende huko tu kichwa kichwa. Soma kitabu hiki kwa uangalifu. Zingatia yale mambo ya msingi. Jiamini na mengine mwachie Mungu!

Nitaongezea na vingine viwili au vitatu hivi vyenye mitazamo tofauti tofauti huko mbele ya safari. Kila la heri kwa vijana mnaotafuta kazi. Kama kitabu hiki kitamsaidia japo kijana mmoja kwa namna moja au nyingine kupata kazi basi, lengo langu litakuwa limekamilika. Endeleeni kupambana kwa kadri inavyowekana na kamwe msikate tamaa. Ndivyo maisha yalivyo!​
Shukran tutapitia kuongeza maujuz
 
Shukran tutapitia kuongeza maujuz
Ndiyo mkuu. Tukichoka kujadili mambo ya akina Dayamondi na akina Mgaya kuchapiwa, tukumbuke pia na kujiongezea maarifa tofauti tofauti. Ni muhimu sana hasa katika dunia ya sasa.
 
Ila ume leta Public. Ungekaa nayo ndani kama hutaki mawazo kinzani
Kukaa nayo ndani haingenisaidia ndiyo maana nimeamua kushea na wadogo zangu hapa. Angalau wajue misingi ya interview.

Na umetoa mawazo gani kinzani kamanda? Au unatafuta shari tu bila sababu? Acha ambao wataweza kusoma wasome hata kama ni page elfu moja. Sioni tatizo kabisa!
 
Kitabu hiki ni kizuri. Mimi binafsi kilinisaidia katika interview yangu ya tatu baada ya kuwa nimeboronga katika interview zangu mbili za kwanza. Ndiyo nilikuwa nimemaliza chuo na kazi ya kwanza ndiyo hasa niliitaka lakini nilikutana na vijana wenzangu kutoka Kenya na Nigeria nikajua tu waziwazi kuwa hapa sitoboi maana wenzangu walikuwa wamejiandaa kweli kweli. Baada ya kusoma kitabu hiki nilipata picha halisi ya ninachotakiwa kufanya katika interview yangu ya tatu na nilikwenda kwa kujiamini sana maana nilikuwa nimejua mambo ya msingi. Mifano ya majibu ya maswali ya kawaida yanayoulizwa katika interview nyingi yaliyomo kwenye kitabu hiki pia yalinisaidia sana. Na nilipata hiyo kazi!

Najua ukiritimba uliopo katika ajira hapa kwetu. Kuna mambo ya kujuana (nepotism), rushwa (za kila aina) na connection. Pamoja na yote haya naamini utafaidika na yaliyomo katika kitabu hiki katika ujumla wake. Na watakaofaidika zaidi ni wale watakaoomba kazi katika mashirika ya kimataifa ambako pengine mambo ya kujuana, rushwa na connection hayana nafasi kubwa sana kama huku kwingine. Usiende huko tu kichwa kichwa. Soma kitabu hiki kwa uangalifu. Zingatia yale mambo ya msingi. Jiamini na mengine mwachie Mungu!

Nitaongezea na vingine viwili au vitatu hivi vyenye mitazamo tofauti tofauti huko mbele ya safari. Kila la heri kwa vijana mnaotafuta kazi. Kama kitabu hiki kitamsaidia japo kijana mmoja kwa namna moja au nyingine kupata kazi basi, lengo langu litakuwa limekamilika. Endeleeni kupambana kwa kadri inavyowekana na kamwe msikate tamaa. Ndivyo maisha yalivyo!​

Mkuu hebu ni PM najaribu kuku PM inanigomea..
 
Back
Top Bottom