Ndugu zangu,
Inakaribia saa sita za usiku hapa Iringa. Kabla sijafunga kazi zangu za usiku huu nimeona niseme japo neno fupi la usiku huu.
Ndio, nimelipitia jarida la kila wiki ( Pichani) . Limesheheni vichwa vya watarajiwa Urais 2015. Inahusu Urais 2015. Si mnajua, Watanzania hatuna ndoto ya taifa, nyingi ni za vyeo tu, ikiwamo Urais.
Na Urais Bongo ni vita, tena si ya mchezo. Na kwenye vita kuna ya muhimu haya; Uwanja wa vita kwa maana ya uwanja wa kupigania. Kuna mikakati, kuna makamanda wa vita na wapiganaji. Lakini, vita pia ni sharti iwe na malengo.
Ndio, babu yangu alipata kuniambia; porini usidanganywe na miguu ya tembo. Tembo ni mnyama makini sana. Unaweza kuifuata miguu ya tembo ardhini ukadhani unayemfuatilia ni tembo mmoja. Hapana, tembo hukanyaga nyayo za tembo aliyemtangulia. Nyuma ya tembo mmoja yumkini kuna tembo mia moja.
Inahusu Uongozi pia, leadership. Nyuma ya kiongozi mmoja yaweza kukawa na kumi wanaomfuatia nyuma yako. Mzee Kenyatta alitamka; " Fuata Nyayo!"- Na kwa tembo ni " Kanyaga Unyayo!"
Naam, usidanganywe na miguu ya tembo, ukadhani ni mmoja, kumbe wako mia moja.
Na hilo ni Neno Fupi La Usiku Huu.
Alamsiki.
Maggid,
Iringa.
Inakaribia saa sita za usiku hapa Iringa. Kabla sijafunga kazi zangu za usiku huu nimeona niseme japo neno fupi la usiku huu.
Ndio, nimelipitia jarida la kila wiki ( Pichani) . Limesheheni vichwa vya watarajiwa Urais 2015. Inahusu Urais 2015. Si mnajua, Watanzania hatuna ndoto ya taifa, nyingi ni za vyeo tu, ikiwamo Urais.
Na Urais Bongo ni vita, tena si ya mchezo. Na kwenye vita kuna ya muhimu haya; Uwanja wa vita kwa maana ya uwanja wa kupigania. Kuna mikakati, kuna makamanda wa vita na wapiganaji. Lakini, vita pia ni sharti iwe na malengo.
Ndio, babu yangu alipata kuniambia; porini usidanganywe na miguu ya tembo. Tembo ni mnyama makini sana. Unaweza kuifuata miguu ya tembo ardhini ukadhani unayemfuatilia ni tembo mmoja. Hapana, tembo hukanyaga nyayo za tembo aliyemtangulia. Nyuma ya tembo mmoja yumkini kuna tembo mia moja.
Inahusu Uongozi pia, leadership. Nyuma ya kiongozi mmoja yaweza kukawa na kumi wanaomfuatia nyuma yako. Mzee Kenyatta alitamka; " Fuata Nyayo!"- Na kwa tembo ni " Kanyaga Unyayo!"
Naam, usidanganywe na miguu ya tembo, ukadhani ni mmoja, kumbe wako mia moja.
Na hilo ni Neno Fupi La Usiku Huu.
Alamsiki.
Maggid,
Iringa.