OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,245
- 103,948
Hodi huku
Kumekuwa na nyuzi humu zikijadili uimara wa trekhlta zinazouzwa mitandaoni South Afrika. Uimara huo umekuwa ukitiliwa mashaka kulinganisha na bei ya trekta hizo. Ukiingia kwenye mitandao mingi utagundua bei ya trekta zilizotumika muda mfupi zikiuzwa mpaka milioni 15.
Achana na stori za mitandao na simulizi. Mwanenu huwa sikubali kushindwa nilifunga safari mwenyewe mpaka South. Twende taratibu nikupe udondozi wa shuhuda.
TRA na TBS
Kabla ya chochote nikaingia TBS kujua taratibu na gharama za ukaguzi.Nikamuonyesa msela picha kadha wa kadha ili anipe ABC. Kwanza akanipa hongera kichizi,akanitakia kila la kheri niingize chombo nizalishe chakula watu wale washibe. Akaniambia gharama ni laki 3 mpaka laki 4 na kazi inafanywa na NIT. Taratibu ni kwamba kama kutakuwa na hitilafu wataandika ripoti nirekebishe.
Baada ya hapo nikaendesha ndinga mpaka TRA waniambie ushuru ukoje, sio nilete chombo halafu kipigwe mnada. Jamaa akaniambia hakuna kodi kwenye trekta ila kuna ushuru kidogo tu nitalipa kama 0.6% na 1.6% ya bei. Nikampa invoice mbili tatu za wauzaji wa South zenye around 15m mpaka 20m tukaona haizidi laki 5.
Nikaona usinichezee,moja kwa moja nikaenda kupima Covid 19 tayari kwa kusafiri.
South Africa
Kabla sijaondoka nilikuwa na sample ya sellers kama 5 hivi ikiwemo niliopewa link na wadau humu. Watatu nikiwa na invoice zao tayari. Muda mwingi walikuwa wananipiga sound nilipe tu wanitumie mzigo. Sikuwa napepesa macho niliwaambia siwezi kuwa fala,nakuja mwenyewe kuangalia chombo nitafute fundi akague ndio nilipe. Mara oooh invoice ita expiry,nawaambia utaandika nyingine kwani shida iko wapi.
Moja kwa moja nikadondoka Cape Town ambapo ilionekana wauzaji wengi wapo kule. Nikaanza na wa kwanza ambaye mzigo wake ulinivutia sana. Nikampigia simu ku book appointment kesho asubuhi namtimbia. Akaniambia wamefunga wamehamia Pritoria. 🤣🤣 nikamwambia kwa kizungu we ni tapeli? Tumewasiliana kila siku unasema upo Cape Town,adress yenu inasoma Cape Town. Hakujibu.
Nikamcheki wa pili. Huyu adress ilikuwa na geogle location. Nikachukua uber kufika hapo hola kuna malls tu wala hawatambuliki. Kuulizia naambia wewe ni mtu wa 3 leo anaulizia hao jamaa.
Siku ikakata ikabidi nijisalimishe kwa mwanangu mmoja huku bongo aliwahi kuishi South miaka ya 2000s. Akaniunganisha na muhuni mmoja hivi mbongo. Sasa yule ndio akanipeleka kwa wenyewe kabisa.
Uhalisia
Hatimaye nikafika kwa wauzaji halisi wa trekta mpya na used. Kiukweli bei tunazodanganyana humu ni bei za matapeli tu. Lakini uhalisia ni tofauti na hakuna tofauti kuuubwa na bei za kina Chriss Lukosi na wauzaji wengine. Japo kwa mtu mwenye muda wa kutosha anaweza kupata trekta lililotumika mwaka hadi miwili kwa bei ya 30m.
Nikafanikiwa kupata trekta New Holland kali sana TT75 kwa 29m. Ngoma ikiwa kwenye muda wa kusafirisha ungepishana na msimu wa mvua. Kusafirisha kwa meli ambayo ni nafuu inachukua 14 mpaka 21days. Nikaona isiwe tabu hii milioni 2 ikipotea sio issue sana ngoja nikakomae tu huko huko. By the way nimekula bata na pisi mbili huko sio haba
Baada ya kurudi Tz nikapambana tena nikapata Case HP 75 4WD kwa 39.5m kwa mwarabu mmoja hivi.
Nitakuja kuhitimisha baadae,ngoja nitafute vibarua huku Iramba.
Kumekuwa na nyuzi humu zikijadili uimara wa trekhlta zinazouzwa mitandaoni South Afrika. Uimara huo umekuwa ukitiliwa mashaka kulinganisha na bei ya trekta hizo. Ukiingia kwenye mitandao mingi utagundua bei ya trekta zilizotumika muda mfupi zikiuzwa mpaka milioni 15.
Achana na stori za mitandao na simulizi. Mwanenu huwa sikubali kushindwa nilifunga safari mwenyewe mpaka South. Twende taratibu nikupe udondozi wa shuhuda.
TRA na TBS
Kabla ya chochote nikaingia TBS kujua taratibu na gharama za ukaguzi.Nikamuonyesa msela picha kadha wa kadha ili anipe ABC. Kwanza akanipa hongera kichizi,akanitakia kila la kheri niingize chombo nizalishe chakula watu wale washibe. Akaniambia gharama ni laki 3 mpaka laki 4 na kazi inafanywa na NIT. Taratibu ni kwamba kama kutakuwa na hitilafu wataandika ripoti nirekebishe.
Baada ya hapo nikaendesha ndinga mpaka TRA waniambie ushuru ukoje, sio nilete chombo halafu kipigwe mnada. Jamaa akaniambia hakuna kodi kwenye trekta ila kuna ushuru kidogo tu nitalipa kama 0.6% na 1.6% ya bei. Nikampa invoice mbili tatu za wauzaji wa South zenye around 15m mpaka 20m tukaona haizidi laki 5.
Nikaona usinichezee,moja kwa moja nikaenda kupima Covid 19 tayari kwa kusafiri.
South Africa
Kabla sijaondoka nilikuwa na sample ya sellers kama 5 hivi ikiwemo niliopewa link na wadau humu. Watatu nikiwa na invoice zao tayari. Muda mwingi walikuwa wananipiga sound nilipe tu wanitumie mzigo. Sikuwa napepesa macho niliwaambia siwezi kuwa fala,nakuja mwenyewe kuangalia chombo nitafute fundi akague ndio nilipe. Mara oooh invoice ita expiry,nawaambia utaandika nyingine kwani shida iko wapi.
Moja kwa moja nikadondoka Cape Town ambapo ilionekana wauzaji wengi wapo kule. Nikaanza na wa kwanza ambaye mzigo wake ulinivutia sana. Nikampigia simu ku book appointment kesho asubuhi namtimbia. Akaniambia wamefunga wamehamia Pritoria. 🤣🤣 nikamwambia kwa kizungu we ni tapeli? Tumewasiliana kila siku unasema upo Cape Town,adress yenu inasoma Cape Town. Hakujibu.
Nikamcheki wa pili. Huyu adress ilikuwa na geogle location. Nikachukua uber kufika hapo hola kuna malls tu wala hawatambuliki. Kuulizia naambia wewe ni mtu wa 3 leo anaulizia hao jamaa.
Siku ikakata ikabidi nijisalimishe kwa mwanangu mmoja huku bongo aliwahi kuishi South miaka ya 2000s. Akaniunganisha na muhuni mmoja hivi mbongo. Sasa yule ndio akanipeleka kwa wenyewe kabisa.
Uhalisia
Hatimaye nikafika kwa wauzaji halisi wa trekta mpya na used. Kiukweli bei tunazodanganyana humu ni bei za matapeli tu. Lakini uhalisia ni tofauti na hakuna tofauti kuuubwa na bei za kina Chriss Lukosi na wauzaji wengine. Japo kwa mtu mwenye muda wa kutosha anaweza kupata trekta lililotumika mwaka hadi miwili kwa bei ya 30m.
Nikafanikiwa kupata trekta New Holland kali sana TT75 kwa 29m. Ngoma ikiwa kwenye muda wa kusafirisha ungepishana na msimu wa mvua. Kusafirisha kwa meli ambayo ni nafuu inachukua 14 mpaka 21days. Nikaona isiwe tabu hii milioni 2 ikipotea sio issue sana ngoja nikakomae tu huko huko. By the way nimekula bata na pisi mbili huko sio haba
Baada ya kurudi Tz nikapambana tena nikapata Case HP 75 4WD kwa 39.5m kwa mwarabu mmoja hivi.
Nitakuja kuhitimisha baadae,ngoja nitafute vibarua huku Iramba.
Msaada: Umadhubuti wa tractor za Afrika kusini
Wakuu naomba msaada. Kuna tractor nimeziona kwenye mtandao za Afrika kusini aina ya massey furgerson series mbalimbali. Zinaonekana ziko refurbished, na ni kama mpya. MfanoF 290 inaenda bei ya Rand 150,000. Naomba msaada kwa mwenye uzoefu, uimara na umadhubuti wa hizi tractor kwani za...
www.jamiiforums.com