Ushuhuda wangu kuhusu RADI (my own testimonial)Nimeshuhudia RADI! Mara mbili, Ni kweli RADI ni kuku kabisa! Tena jogoo anaevutia haswa!

Kama sio kigoma huko basi rukwa au katavi

Huko Kuna radi hadi za jero za kununua.

Kuna kipindi cha mambo mseto radio one enzi zile Charles Hilary akikiendesha aliwa tupa stori ya mwewe kubebwa ngombe wa kilo 300 huko kati
Ilikua 2004 kipindi hicho niko nasoma Kantalamba Sec. School
 
Mkuu kuna radi mbili ile ya asili ambayo shughuri yake tunaijua na hii ya wanchi kutengeneza ambayo mtengenezaji anaweza kuipa muonekano wowote anaotaka ata akitaka iwe na muonee wa binadamu anaweza tu sasa wewe umeona hii ya binadamu
 
Vitu vya asili vinasiri sana. Jogoo au ndege kutoa umeme mkubwa na ngurumo kubwa. Inashangaza sana.
Wacha niendelee kujifunza
 
Sayansi inaamini ni umeme wa asili,. na wewe unaamimi ni kuku mwekundu tena jogoo anayevutia.??
 
Duh "LY" yaani Last Year umetisha!!!
Nilitaka nimuulize,,,YAANI last year alikuwa darasa la Saba....?so Yuko form one kwa Sasa...ok ngoja nijadili mada....RADI HATA KULE KWETU SUMBAWANGA INAKUJA KWA MTINDO WA MANYUNYU MEPESI MEPESI IKIAMBATANA NA NGURUMO RASHARASHA..ILA KAMA HAIKUHUSU HAINAGA SHOBO NAWE
 
Naam,

Kumekuweko na speculation nyingi kuhusu RADI. Nyingi zikihusisha radi katika makundi mawili, ambayo ni radi kisayansi,kama umeme asilia na Radi kiimani. Wengi wakiihusisha na ushirikina.

Binafsi ziko katika upande wowote Kati ya hizo pande mbili hapo juu, bali naeleza kile nilichopata kukishuhudia mara mbili kwa macho yangu mawili, utotoni( adolescent age) na ukubwani kidogo nikiwa najitambua.

Nikiwa na yapata miaka kadhaa, tukiwa porini tunachunga ng'ombe tukiwa rika vijana wadogo watatu tuliona jogoo mzuri pembezoni na maeneo tuliyopo, alikuwa anaevutia tulimnyatia na tukamkamata jogoo alikuwa na kila kitu chekundu kuanzia mdomo,manyoya hadi miguu tukamfikisha nyumbani huku manyunyu ya mvua yakiendelea kuongezeka, tukamfungia jogoo jikoni na wengine wakiirudisha mifugo zizini.

Tukiwa tumefurahi na tukiendelea na michezo kwani kitoweo kimepatikana, tukamwambia bibi kuwa tumeokota kuku machungani na tumemfungia yumo jikoni. Bibi kwenda kuangalia! Lahaula! Alianza kupiga kelele za yowe kwa majirani, unajua umbali uliopo baina ya mji na mji. Aliendelea huku analia na kukimbiza huku na kule huku mvua ikiendelea kunyesha.

Baadhi ya watu waliendelea kujaa, na kutahamaki tukasikia ngurumo kubwa na miale ya radi iliipiga ile nyumba ambayo ndio huko tulipomfungia yule kuku. Wote tuliinama kwa yoga na baada ya mvua kukatika tukagundua kuwa yule kuku hakuwemo tena na alipotea ghafla baada ya Radi ile kutoweka, na haikuleta madhara makubwa sana.

Tukio la pili;-)
Nikiwa likizo last year Std Vii kama ilivyo kawaida nilimtembelea bibi na babu(R.I.P), katika mizunguko yetu ya hapa na pale, tulitenbelea mtoni kuogelea na kupiga stori mbili tatu na washkaji wa kunijibu, maana tulikuwa hatusomi pamoja tena,mimi nilikuwa nikija huku kwa ajili ya likizo tu.

Tukiwa tunaendelea kuogelea kea mbali kidogo niliona tukio kama lile lililotutokea miaka kadhaa nyuma na kufanya tupokee kichapo toka kwa babu, niliona jogoo wa dizaini ile ile! Mwekundu Tii! Akiwa pembeni ya mto akizamisha kichwa makini na kutoa mara kwa mara huku akipigapiga mabawa.

Mapigo ya moyo yalianza kunienda mbio kwa woga hofu! Kwani nilihisi kinachokaribia kutokea na pembeni kulikuwako na vijana wadogo wanachunga.

Kwa hofu tulikuwa tukimuangalia yule jogoo anaevutia sana na wenzangu wote tukiwa tumetoka mtoni tuko pembeni,ghafla ulisikika muungurumo na mitetemo kikubwa+ miale kadhaa ya mianga(Radi) na pale pale ng'ombe watatu walipigwa na Radi pale pale na kufa!.on the spot!.

Haya nimeyashudia mwenyewe kwa macho yangu,nikiwa na akili timamu!

Sayansi inaamini ni umeme wa asilia, lakini napata ukakasi nikiunganisha nilichokishudia kwa macho,na sayansi ya kufundishwa. Ktka radi napata kuuona uhusika wa hivi vitu, MUNGU yupo(imani) maana nimeona kitu kwa macho halisi, na kikapotea.

Maswali ni mengi najiulizaga, yule jogoo kea nini hupotea! Baada ya Radi!? Anaeenda wapi!? Na kea nini sayansi inakataa ukweli kwamba Radi ni kuku!?
Nyinyi ndio mnaishushq hadhi jf,unajua fika unasimumilia/unashuhudia uonge na still unafanya hivyo,hivi jf mmeifanya fb?,eti tukakamata Radi
 
Simulizi ya kuku kuhusishwa na radi ni mara ya pili naisikia kwako, toka niliposimuliwa hivyo miaka mingi iliyopita.
 
Story hii aliwahi kunihadithia bibi, akasema miaka yao wakiwa wadogo radi zilikua zinapiga Sana kuliko sasa hiv, na muda mfupi kabla ya Radi kupiga walikua wanaona jogoo na baada ya radi anapotea. Nilimuuliza mbona siku hiz hatumuoni jogoo akasema hajui Ila miaka yao waliona mengi ya ajabu na yameenda yanapungua kila mwaka
 
Option 1: tuamini tu maneno yako sababu umeona

Option 2: huenda una hallucination na unaona vitu ambavyo havipo...

Nadhani option 2 ni more plausible

Kwahiyo unataka kusema kuwa yeye, marafiki zake, bibi yake pamoja na wanakijiji wengine walikuwa wana hallucinate kwa pamoja.
 
Back
Top Bottom