mimi ni kijana wa makamo ya kati mkazi wa jijini dareslaam kinachonileta katika jukwaa hili ni kutaka ushauri kutoka kwa wanajamii wenzangu.nina mpenzi ambaye hatuna muda mrefu sana katika mapenzi yetu ni kama muda wa miezi miwili tu.kikubwa hasa ni kwamba wakati tukianza mahusiano hakunieleza kuwa alikuwa na mtu lakini leo hii takribani miezi miwili imepita ndio ananiambia kuwa ana mpenzi isipokuwa anataka kuchagua kati yetu ni nani anayecare zaidi ya mwenzie mwenye kujua utu wa mwanamke na mwenye heshima.kiukweli mimi binagfsi nampenda huyu msichana na yupo kwenye program yangu ya mahusiano ya muda mrefu si wa leo na kesho, kama ilivyozoeleka.mpaka sasa niko njia panda sijajua nifanye nini mawazo yangu pekee hayanitoshi nataka nipate mawazo ya wengine ili nipate uthabiti "consistence".yangu ni hayo kwa vijana wenzangu na wasio vijana naomba mnisaidie mawazo yenu.