Ushauri wako ni muhimu zaidi kwangu

Chiomaizwe

Member
Apr 9, 2015
24
41
Wana jamvi habari za siku tele,

Mimi nimekuwa naingia hapa jamvini kama guest baada ya kuelezwa na rafiki yangu juu ya uwepo wa hili jamvi. Nimekuwa msomaji wa mada mbali mbali ambazo kwa namna moja zimenifunza mengi sana.

Leo hii nimeamua kujiunga ili nilete swala langu japo mnishauri manake nimekuwa nalo kwa mdua sasa na sijaweza kuomba ushauri kwa mtu yeyote yule.Nianze hivi hii ni habari ya kweli na kama ukiona nimekuudhi naomba uniwie radhi lakni sina budi tu kuisema manake muda mwingine mwiba wa kujidunga mwenyewe unahusika.

Mimi ni mwanamke mwenye miaka 39 sasa, nikiwa na watoto wawili na ndoa ya kikristo. Kwa bahati njema sana Mungu alitupa watoto wazuri na wenye afya katika kipindi ambacho sote mie na mume wangu tukiwa chuoni tunasoma. Yeye alikuwa anasoma digree ya 2 na mie nilikuwa nasoma ya kwanza katika fani tofauti.

Maisha yetu japo yalikuwa ya kimaskin lakin tuliishi kwa raha amani na upendo furaha na heshima na yakawa yana afya za rohoni na mwilini pia. Kiukweli mume wangu ni miongoni mwa wanume ambao ni wazuri wana upendo wa kweli, anajali na mtu anayependa zaid familia kuliko kitu kingine chochote.

Mimi kama mama nilijitahd sana kuwa na heshima na kutimiza wajibu wangu kama mama na hata kusaidia katika kuijenga familia kiuchumi.Miaka 5 iliyopita mume wangu alipata safari ya kwenda masomoni na ukweli nilijitahdi sana kuhakikisha kila kilichotakiwa alikipata ili aende nikiamini kwamba anaenda kwaajili ya manufaa ya famili. Wakati anaondoka nilikuwa ni mjamzito hivyo nilimwambia aende tu mie sina neno.

Kwa bahati nzuri mtoto alizaliwa baada ya mwezi toka asafiri na ukweli alifurahi sana. Alipopata likizo alikuja akamkuta tayari mtoto ni mkubwa na alikuwa kama na miezi 11 hivi. Siku chache kabla ya yeye kurudi tena ulaya tulipata ajali mbaya sana ya gari na familia nzima ilihusika, ingawa majeruhi tulikuwa mimi na mtoto huyu mdogo.

Nililazimika kumruhusu mume wangu kurudi shule kwasababu ticket yake ilikuwa hawez kuiahirisha kwa siku nyingi zaid, na nilijitahd sana japo mgonjwa kuhudumia wanangu akiwemo huyu mdogo ambaye alikwua amevunjia mguu.Hata hivyo maisha yalikwua mazuri na tuliishi kwa mapenzi sana, na kila alipopata likizo alikuja nyumban kutuona.

Sasa tatizo lilianza mwaka juzi kuna hela amabzo alinipa kwaajili ya kujengea mie nikazitumia hazikuwa nyingi sana ila pia zingeweza kufanya jambo kwenye ujenzi hata kama ni dogo, fedha zile sikuzitumia ivyo ila nilizitumia kwa kumtibu mtoto mguu na matumiz ya nyumban, alipokuja akakuta sikuzitumia nilimuelewesha akaelewa maisha yakaendelea.

Sikujua kama mume huyu ameweka kinyongo ila alipoondoka sasa toka mwaka 2013 hadi leo hajawah kuwasiliana na mimi wala watoto. Mara ya kwanza nilijua ni utan lkn nikashangaa miezi iankatika simsikii mara akanibock skype, tweeter na kila kitu, mara nikipiga hapokei simu yangu, mara email zangu kablock nikaishiwa nguvu kabisa.

Nikaona isiwe tabu wala sina sababu ya kuanza kuitisha vikao vya ukoo kujadili haya nikaamua sasa kuwa siriazi na watoto wangu wasome, wavae, na waishi maisha mazuri. Mungu bariki nikapata kazi kwenye kampuni moja ya utafiti na ushimbaj wa gesi.

Maisha yakaanza kuenda vizuri zaid kwa upande wangu. Ila mume nikawa bado sina mawasiliano naye. Mwaka ukakatika sijampata kwenye mawasiliano mama yake anaongea naye na dada zake lkn mie mkewe hapana niaksema siwez kununiana na wakwe zangu mie kisa yeye nikaachana na hayo mambo.

Huu sasa ni wamaka wa 3 sijamtia machoni ingawa kuna kipindi alikuja Tz akapokelewa na dada yake akakaa siku alizokaa na kurudi huko ulaya kwake mie hata sikuumiza kichwa nikasema watoto wangu ni bora zaid kuliko huyo aliyeko huko so niakjipa moyo maisha yakaendelea.Niliamuaga kawa na mchepuko ili nipate liwazo lakin pia vikanishinda manake sikupata ambaye tuko compatible nikaona nitulize akili kazini na kwenye malezi ya watoto manake hawa ndio watakao nitoa baadae.

Mwaka 2012 mwezi dec nilipata nafasi ya kwenda SA kwenye makao makuu ya kampuni ninayofanyia kazi, kulikuwa na mkutano wa wadau wakuu wa uchimbaj wa mafuta nagesi dunian nilikutana na watu wengi sana akiwemo Bwana mmoja DB ambaye ni mhadisi wa petroleum. Kama kawaida kwenye mikutano kunakupeana contacts basi na mie nikawa nimepata za watu wengi tuu.

Mwaka 2014 june kukafanyika mkutano mwingine Ghana nilipokwenda nikakutana na almost watu wengi niliokutana nao huko SA akiwemo DB hivyo network ikazidi kukomaa katika kazi. Mwaka huu mwezi jana pakafanyika kongamano la gesi la mafuta lililoandaliwa na ubalozi wa Canada hapa nchini mie nikawa naiwakilisha kampuni nikakutana tena na watu almost wale wale hivyo kibiashara nikawa nina watu wengi zaid kwenye huu upande ambao nawajua sana na tumezoeana.

Jambo la ajabu sna Bwana DB alikuwa ni mtu wangu wa karibu kikazi na yeye huyu tulikuwa tunawasiliana hasa pale ninapokwama kikazi kuomba ushauri nk na amekuwa akinimentor sana kwenye huu upande. japo kuwa tulikwa karibu lakin hatukuwah kupata muda wa kuongea maswala yetu ya kijamii kwa muda wote toka nimfahamu. Alipokuja hapa Tanzania sasa kwa mara ya kwanza akaniomba tutoke dina mie na yeye nikamkubalia.

Kweli kwenye dina tuliongea sasa mambo ya kijamii zaid kuliko ya kazi ndipo aliponieleza mkasa wa maisha wote, na kwamba mkewe ni marehemu, na anayemtoto wa kuasili muafrica wa Ghana, jamaa alifunguka sana na mie nikamwambia ukweli juu ya maisha yangu kwamba niko kwenye hali ya sintofahamu ya ndoa yangu.

Basi katika kuongea akaniambia kwamba anapenda basi kama nitaridhia anioe na yuko tayari kuwa na mimi na awe baba mlezi wa watoto wangu. Sikumjibu kwa haraka manake mie sijielewi na naogopa sana kutoa ahadi za uongo. Ila nilimkaribisha nyumban kwangu siku moja kabla hajasafiri kurudi kwao akawaona wanangu na akala chakula cha jion kisha akaondoka kurudi hotelin kwake.

Toka ameondoka DB amekuwa akinitumia salam anachat na mie kila mara kwenye messenger nk, pia amekuwa akiwasalimu watoto na kuonyesha nia ya dhati kabisa ya kua na mimi. Mie bado sijampa jibu manake sijui hatima yangu, ingawa kutoka kwa dada wa mume wangu nimeambiwa mume wangu kaoa binti huko anaish nae. Nilishtuka sana lakin nikasema maisha ndivyo yalivyo sina ujanja zaid.

Leo asubuhi nimefika tu ofisini DB akanipigia anataka kuja Tanzania kuniona na hapa amenipa email adress ya kampuni anayofanyia kazi niwatumie email kuwaomba wamruhusu aje kuniona na niseme kwamba namuhitaj kwa haraka sana. Nimejikuta napata kigugumizi nimjibuje wapendwa wangu.

Ugumu kwangu unakuja hapa, bado nampenda sana mume wangu ingawa amekosea. Pili kuanza maisha na mtu mwingine mgeni kabisa katika uzee huu najionea kama nitapata shida kwenye kuishi.Kitu ambacho nakiamini kutoka kwake ameniambia yuko tayari kulea watoto wangu, yeye anachotaka ni kupendwa, kujaliwa na kuheshimiwa tu katika maisha yake yaliyobaki. Yeye ana umri wa miaka 48.
 
Ooooouuuh pole sana kiukweli hii dunia ina mambo sana..? Me nadhani si vyema watu tukurupuke kutoa ushauri but tuwe na plan B kwa kila ushauri..? Cha muhimu ndoa ni ya kikristo that means kwa L.M.A hairuhusu kuolewa tena but kwa upande mwingne tuseme wewe ni female unahitaji farijiko la moyo na kama ulivumila vya kutosha kwa upande wangu i'll advice as follows" follow your Heart

and keep the prayers above the skies, HE above us knows the guilty an sorrows we face" kama unadhani huna cha zaidi ya kumkubali huyu anayekuta just do it but if still unadhani its not a ryt time just chill..? We say "in the middle of difficulties lies an opportunity" wats yours
 
Chiomaizwe sijui nani wewe
Kwakweli nilidhan mie ni mvumilivu lakin wewe mwenzangu umezidi na kunipita mbali sanaaa.

ushauri wangu kwako ni huu hapa

a) usijicomit kwanza mpaka umehakikisha kwamba ni kweli mumeo kaoa huko alipo

b) focus zaid kwenye kulea watoto wako haya ya kuchomwa msumari wa kati ebu usiyape kipaumbele kwanza kwa sasa manake yatakuchanganya

c) mwambie uyo db akupe muda zaid wa kufikiri juu ya uamuzi wako wowote ule

d) usiwaambie kwanza familia yako kwasaas jipe muda

e) usiongee jambo lolote lile na wakwe ama mawifi kwasasa

sijui lini ndio mwisho wa hiyo sasa lkn nijuavyo mimi time will tell

mweeeeh!!!!!!!!!!...................ila una bahati sana bibie sawa na kuokota dhahabu kkoo
 
Last edited by a moderator:
Ooooouuuh pole sana kiukweli hii dunia ina mambo sana..? Me nadhani si vyema watu tukurupuke kutoa ushauri but tuwe na plan B kwa kila ushauri..? Cha muhimu ndoa ni ya kikristo that means kwa L.M.A hairuhusu kuolewa tena but kwa upande mwingne tuseme wewe ni female unahitaji farijiko la moyo na kama ulivumila vya kutosha kwa upande wangu i'll advice as follows" follow your Heart

and keep the prayers above the skies, HE above us knows the guilty an sorrows we face" kama unadhani huna cha zaidi ya kumkubali huyu anayekuta just do it but if still unadhani its not a ryt time just chill..? We say "in the middle of difficulties lies an opportunity" wats yours

I can imagine a lady being in such situation for such duration daaah!!!
Ila sijui bhanaa mie kiukweli nisingekurupuka katika hili na hasa kama anakiri bado anampenda mumewe wa ndoa, though ni ngumu sanaaaa

af sasa apa ukitaka kujua binadamu ni wabaya akiamua kutoka na db wake, tu watasema alimtekeleza mume kisa mue kaenda akusoma akatoroka na wtoto. Ila akiwa kwenye shida hakuna anayemsaidia
 
.........huyp mumeo keshaoa/kavuta kimwana ndani na kukutafutia sababu, hela ingekuwa umetapanya kwenye kichen parti kweli anganuna, ila hata kuwajulia hali wanae ????

ndugu za mumeo(hususan huyo dada mtu aliyempokea ndugu yake ilhali anajua ni mtu mzima mwenye mji wake anasemaje?)

hebu fanya jitihada za kujua hatima ya ndoa yako kwanza.... mwanaume kama hakutaki si akupe talaka? uwe huru? kwa nini akuweke kiporo ili vikimtibukia arudi????

kuhusu DB..............nitarudi.....


 
hivi gfsonwin na BADILI TABIA, Mtu miaka 3+ hakuna barua wala nini halafu eti asijicommit hadi ajue hatma? Kama uko na ndoa hamna mawasiliano, umekuwa blocked kwa maneno na matendo, na mtu amerudi hadi mtaa wa tatu hana habari na wanae wala wewe. Halafu ati unaendelea kumpenda? Unampenda nini hapo kwa mfano?
 
Last edited by a moderator:
.........huyp mumeo keshaoa/kavuta kimwana ndani na kukutafutia sababu, hela ingekuwa umetapanya kwenye kichen parti kweli anganuna, ila hata kuwajulia hali wanae ????

ndugu za mumeo(hususan huyo dada mtu aliyempokea ndugu yake ilhali anajua ni mtu mzima mwenye mji wake anasemaje?)

hebu fanya jitihada za kujua hatima ya ndoa yako kwanza.... mwanaume kama hakutaki si akupe talaka? uwe huru? kwa nini akuweke kiporo ili vikimtibukia arudi????

kuhusu DB..............nitarudi.....



BD mie najiuliza ivi huyu dada kwanza ni mzima ama ni ndondocha?

mwanaume miaka 5 sijui 3 hana mawasiliano?? ..............................

alee wanae baasi aachane nae kama vipi aka file divorce basi.
atavumilia ndo yale ya mtu anamjia na visukari na presha
 
hebu fanya jitihada za kujua hatima ya ndoa yako kwanza.... mwanaume kama hakutaki si akupe talaka? uwe huru? kwa nini akuweke kiporo ili vikimtibukia arudi????

kuhusu DB..............nitarudi.....


[/B][/FONT][/SIZE][/COLOR][/QUOTE]
Hili ni wazo zuri pia kama anaweza kumpata koz kama nlisoma poa jamaa kafanya Desertation na ukisoma L.M.A ni kati ya vitu vinavyoweza kuvunja ndoa..! Soo akimpata kwa mawasiliano aombe talaka ili awe huru kuishi na mr DB
 
Mi naona DB asipewe nafasi bila taarifa, taarifa ninayoiongelea hapa, ni wewe kwenda kwa wazazi wa mume wako na kuwajulisha situation ya ww na mumeo kwa kipindi chote, na kama pia unampenda DB basi ni wakati muafaka wa mumeo kukupa talaka kwasababu katika hali ya kawaida ata kama ndoa za kanisani hawaachani lakini still huwezi kukaa na mume katika maisha ya ukatili, mume hajui watoto wake wala mkewe hiyo sio kweli,

so take advantage ya kumwagana kabisa na huyo Hubby umpendae na amishia feelings kwa DB inawezekana DB akawa faraja na pumziko la moyo wako, wanaume wa bongo wengi wakienda Ulaya wanaishia kwa style hiyo sijui ni ulimbukeni au upuuzi, lakini mwisho wasiku wanarudi kupiga magoti,

hivo unampigiaje magoti mwanamke uliemjeruhi kiasi hiki? atakusamehe lakini hayataisha kichwani kuna mambo mengine psychologically hayaondokagi kichwani na yanajenga chuki sana ukiyakumbuka, my advise ni kuwa lazima uweke clear upande wa mumeo ndio uanze maisha na DB ili kuhepuka maneno, maana hapo yatasemwa mengi ya mtoto wao hayatoonekana
 
hivi gfsonwin na BADILI TABIA, Mtu miaka 3+ hakuna barua wala nini halafu eti asijicommit hadi ajue hatma? Kama uko na ndoa hamna mawasiliano, umekuwa blocked kwa maneno na matendo, na mtu amerudi hadi mtaa wa tatu hana habari na wanae wala wewe. Halafu ati unaendelea kumpenda? Unampenda nini hapo kwa mfano?
ivi sasa King'asti unategemea nini akisema ajicommit kwa DB ?
hebu niambie kwa jinsi alivyosema ni wazi wanawe ni wakubwa atawaambia nini?? Lakin jamani muda mwingine anahitaj tu kuwa huru, ayafurahie maisha yake yeye kama yeye, kama kweli mume hana mawasiliano na watoto, kwa muda wote huo tusemeje sasa??
BTW ivi akienda kumripoti kwa dawati la wanawake ubalozi wa nchi aliyopo hauwez kumsaidia??
aaarrgggggggggggghhhhhhh.....................jamani aachanae nae tuu kama alivyoachwa akajianzie maisha yake.

(sijui hata kama nimeeleweka manake nimeandika kama naongea vile)
 
Last edited by a moderator:
bahati iyo mmeo usikute kaoa kibibi huko ili apate uraia

Nilivyoambiwa na uhakika ninao toka kwa rafiki zake ambao walikwenda nae masomoni ni kweli anaish na mwanamke wa kizungu huko. Mimi japo niliumia sana sikuona pakuelekea manake mume wangu ni jeuri sana na hata mama yake mzazi huwa hamsikilizi kabisa. Yaani anweza kumjibu mama adi mimi nikaogopa kwanini anamjibu mama ivi.

Kutokana na hili hata mama yake mzazi anamuogopa kiasi kwamba hawez kuongelea jambo lolote linalomuhusu mwanae huyu.
 
daaaaaaaaaaah pole sana,ushauri wangu pata kwanza muafaka wa mumeo unless otherwise utajuta,pia kwa umri wako kukaa bila tendo la ndoa ni mtihani utajikuta siku unaangukia pabaya,kuwa na huyo jamaa lakini usije jiroga kuongopa let him know nini kinaendelea kwan naamin hata mumeo huko atakuwa na mtu but sijui kama anawaza kuoa au laaaah,all in all muombe sana mungu huenda hili jaribu lina maana katika mapito yako,yeye akupe majibu ya hayah.
asante
 
Ooooouuuh pole sana kiukweli hii dunia ina mambo sana..? Me nadhani si vyema watu tukurupuke kutoa ushauri but tuwe na plan B kwa kila ushauri..? Cha muhimu ndoa ni ya kikristo that means kwa L.M.A hairuhusu kuolewa tena but kwa upande mwingne tuseme wewe ni female unahitaji farijiko la moyo na kama ulivumila vya kutosha kwa upande wangu i'll advice as follows" follow your Heart

and keep the prayers above the skies, HE above us knows the guilty an sorrows we face" kama unadhani huna cha zaidi ya kumkubali huyu anayekuta just do it but if still unadhani its not a ryt time just chill..? We say "in the middle of difficulties lies an opportunity" wats yours

Sasa iyo L.M.A hairuhusu na mie ninavyo vyeti vya ndoa hapa nilipo manake hakuondoka navyo lakin je nitasaidika vipi ikiwa ndo amesha zamia huko na huyo mwanamke mwingine? Natamani arudi nyumban hata leo.
DB ukweli japo ndo ivyo sijampa msimamo wangu lakin ukweli amekuwa akinishauri vingi sana na hasa juu ya hatma ya hii ndoa yangu manake yeye amesema kama kaoa basi na wewe nikuoe kwakua hatuna haja ya watoto wengine tulepo maisha basi.

Ugumu kwangu mpendwa wangu unakuja kwa wanangu, ivi ninaanzaje kuwaambia kwamba nimeachana na baba yao na sasa watalelewa na baba mwingine?
 
Chiomaizwe sijui nani wewe
Kwakweli nilidhan mie ni mvumilivu lakin wewe mwenzangu umezidi na kunipita mbali sanaaa.

ushauri wangu kwako ni huu hapa

a) usijicomit kwanza mpaka umehakikisha kwamba ni kweli mumeo kaoa huko alipo

b) focus zaid kwenye kulea watoto wako haya ya kuchomwa msumari wa kati ebu usiyape kipaumbele kwanza kwa sasa manake yatakuchanganya

c) mwambie uyo db akupe muda zaid wa kufikiri juu ya uamuzi wako wowote ule

d) usiwaambie kwanza familia yako kwasaas jipe muda

e) usiongee jambo lolote lile na wakwe ama mawifi kwasasa

sijui lini ndio mwisho wa hiyo sasa lkn nijuavyo mimi time will tell

mweeeeh!!!!!!!!!!...................ila una bahati sana bibie sawa na kuokota dhahabu kkoo
uhakika ya kwamba mume wangu kaoa ninao toka kwa dada yake alompokea alipokujaga pamoja na rafiki yake walikwendaga wote masomoni lakin yeye amesharusi baada ya kumaliza.

DB yuko na haraka sana manake hapa nilipo anataka kuja Tanzania kuniona na kuwaona wazazi wangu ili aoe kabisa na yeye tayari kesha nitumia email ya kampuni yake ili nimuombee ruhusa
 
Mmmmmmmmmmmmh! KUNA APPROACH 2 HAPO!

1. KATE MIDLETON APPROACH! Hii ilimlipa sanaa Kate, hii unatuliza mpapa tuliiiiiiiiiiiii kama unanyolewa vuzi mpaka hio siku isio na jinaaa atakaporudi huyo mume. Believe atarudi even fter 10 years. Mungu anajibu japo kwa kuchelewa mda mwingine lakini anajibuuu. Akirudi hio siku iso na jina na kukuta umekituliza mambo byeeeeeeeeeeee! Akikuta umekitembeza ana ghairi. Kate aliachana na prince akakituliza tuliiii, wenzie wanaolewa miaka ishirini na ngapi huko yeye anafukuza upepo wa prince tu, siku iso na jina ikafika bwanaa. Angtia tamaa kujichulia looser si ingekula kwake?

2. MTAANI UNTD! Hii unakuwa a woman of double faces. Huku kwa wanao kujua unajitia kuendelea kumngoja mumeo kwa unyonge, huku kwa bwana BD mnakandamiza mavituz kama kawaidaaaaaaaa. Kwa raha zenu. Unacheza ligi international! Dubai, South, Nairobi hivo yani. Unapata kitu roho inapenda huku unafukia tracks zako. Siku iso na jina ikifika kama sio yule uliejiachia na boloyanki la DB! Hahahaaaaaa! HII NI WIN WIN! Ila usiwe mzembe tu, na uwe na roho ya korosho hubby akirudi unamuangalia usoni kama sio yule ulieshika mic ya DB! Hahahaaaaaaaaaaa!
 
.........huyp mumeo keshaoa/kavuta kimwana ndani na kukutafutia sababu, hela ingekuwa umetapanya kwenye kichen parti kweli anganuna, ila hata kuwajulia hali wanae ????

ndugu za mumeo(hususan huyo dada mtu aliyempokea ndugu yake ilhali anajua ni mtu mzima mwenye mji wake anasemaje?)

hebu fanya jitihada za kujua hatima ya ndoa yako kwanza.... mwanaume kama hakutaki si akupe talaka? uwe huru? kwa nini akuweke kiporo ili vikimtibukia arudi????

kuhusu DB..............nitarudi.....



Huyu wifi yangu hatuongei nae kwasasa manake alisema kabisa kwamba kwasasa kaka yetu ameoa mzungu na siku akija nitakuita uje eapoti kumuona aliyasema hayo kwa jeuri sana nikakasirika na kuamua kufuta mawasiliano yangu na yeye kabisa
 
Back
Top Bottom