Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,765
- 218,386
Baada ya leo kushindikana kwa Mahojiano yaliyopangwa kufanyika kwenye Studio za Wasafi FM , Baina ya Watangazaji wa kituo hicho na Tundu Lissu , imekubaliwa kwamba itapangwa siku nyingine kwa ajili ya jambo hilo
Ukweli ni kwamba Sababu zilizotolewa na Wasafi media kama utetezi wa mkanganyiko huo hazitoshi hata Chembe , na baada ya uchunguzi wetu tumeanza mara moja kutilia mashaka jambo hili iwapo litafanyika wakati mwingine .
Sababu kuu iliyotolewa na Wasafi Media ni kwamba HAWAKUJIPANGA , mahojiano muitishe nyie halafu mnasema hamkujipanga ! mwataka kujipangaje , ili iweje ?
Ushauri wetu kwa Tundu Lissu asithubutu kuhudhuria mahojiano mengine kwenye studio hiyo , au kama ni lazima ahudhurie basi ni muhimu na ni lazima aende na mic yake pamoja na kiti chake , hii ni kwa sababu za kiusalama .
Naomba kuwasilisha .