USHAURI: Rais Magufuli vunja ATCL. Anzisha Tanzania Airways ama Kilimanjaro Airways

Hakika hii ndio siasa ya maendeleo,umebainisha sababu nzuri.Ni kweli linahitaji jina jipya hasa ukizingatia serikali inalipa madeni yote,fikra mpya pia ni muhimu.

Hongera Comrade!
Shirika la ndege ni zaidi ya kuwa na ndege. ATCL ilinyongwa kabisa pale walipolikabidhi kwa makaburu na South African Airways. Kutokana na njama chafu shirika lilipoteza njia (routes muhimu) lililokuwa nazo pamoja na haki za kutua kwenye viwanja muhimu kama Heathrow, London. Nadhani hata regional routes kama ya Johannesburg ilichukuliwa. Sasa hata shirika likipata ndege mpya litapata shida kupata na kushindana katika routes mpya. Na hiyo ni bila kutaja changamoto zingine kama kukosa karakana, wafanyakazi wazee/wachovu, taswira mbovu/hasi na ushindani katika sekta ya usafiri wa anga kwa sasa (angalia yanayotokea kwa Kenya Airaways, Precision Air na hata Fastjet). Mimi naunga mkono hoja ya kulivunja ATCL na kulipumzisha kwa amani. Kama ni muhimu kuwa na shirika la ndege la taifa kwa sababu za sifa (prestige) tuangalie uwezekano wa kuunga mkono sekta binafsi au ubia katika ya serikali na sekta binafsi (PPP). Kabla serikali haijakurupuka kuzika fedha zaidi katika ATCL inapaswa kujiuliza kwa nini sekta binafsi, amabayo husukumwa zaidi na kutengeneza faida, haijaona fursa katika soko ambalo ATCL inatarajia kulihudumia.
 
nitafurahi siku nikiona ukija na hoja ya kuitupilia mbali ccm, chama cha zamani,chama cha majipu, chama cha majambazi,chama kilichoifanya nchi yetu kuota majipu kila kona
nakushangaa kamanda ukitaka kuitupilia mbali ccm inabidi uwe umejiandaa na chama mbadala cha kuongoza dola. sasa ukishatupa utaweka chama gani kwa sasa. chama kikuu chadema tunachokitegemea kilishauzwa kwa watuhumiwa wa ufisadi unategemea nini. mawazo yako haya yangekuwa kipindi kile cha Dr Slaa ningekuunga mkono. but now its impossible. cuf nayo ndio kwishney, nccr haijitambuli, TLP majanga, labda ACT naona wanakuja kwa strategy inayoeleweka kwa sasa. katibu mkuu chadema Dr ., amesema chama sasa kiache siasa za kupayuka payuka na zile siasa za matukio.hazina tija.
 
Naunga mkono hoja. Hili jina ATCL ni la kufuta kabisa. Jina Tanzania Airways ingependeza zaidi na ni utambulisho tosha. Tuifanye hii thread active hadi tuone mabadikiko.
 
Kabla hatujamaliza kuhamia Dodoma na kulipa stahiki zote za uhamisho watumishi tunataka kustaafisha wafanyakazi na kuwalipa stahiki zao zote. Kisha tunaunda shirika jipya. Kwa nini tusibadili jina na kufanya kazi kwa taaluma zao? Hao walifanya zero kwa ajili ya uongozi. Badili uongozi, weka sera zifuatwe shirika litaleta tija
 
Ushauri mzuri..Jina Tanzania Airways limekaa vizuri...Ndege zitakua na majina ya vivutio kama Kilimanjaro , Zanzibar, nk
tena aivunje yote na tutafute uongozi mpya na timu mpya kabisa. tunao vijana wengi wamesoma hawana kazi na wana ari ..tuwape nafasi
ile ATCL ivunjwe na walipwe mafao yao tuachane nao...wametula sana..kila nikikumbuka miaka ile nikienda kukata ticket ofsini kwao wanakwambia zimejaa ...ukienda kwa agents nafasi zipo na ndege tupu...
sasa hawa wengi bado wapo na mentality zao ni zile zile....TUANZE UPYA
 
Kuna tofauti kati ya "legal name" na "trading name". Air Tanzania Company Limited (ATCL) ni legal name, wakati "Air Tanzania" ni trading name ndiyo maana ndege zinaandikwa Air Tanzania.
Kubadili trading name hakutaleta faida wala hasara kwa sababu tatizo ni management na siyo jina.
Air Tanzania iendeshwe na watu hata foreigners wenye uzoefu na ujuzi katika biashara ya ndege; si busara kung'ang'ania uzalendo wakati hatuwezi.
 
Umenena vyema Lizabon. Upo umuhimu wa kubadili jina ili kwendana na kasi ya maendeleo
 
Kuna tofauti kati ya "legal name" na "trading name". Air Tanzania Company Limited (ATCL) ni legal name, wakati "Air Tanzania" ni trading name ndiyo maana ndege zinaandikwa Air Tanzania.
Kubadili trading name hakutaleta faida wala hasara kwa sababu tatizo ni management na siyo jina.
Air Tanzania iendeshwe na watu hata foreigners wenye uzoefu na ujuzi katika biashara ya ndege; si busara kung'ang'ania uzalendo wakati hatuwezi.
Branding ni muhimu. Kuna bidhaa nzuri ambazo zilishindwa sokoni kwa sababu ya taswira -branding. ATCL ni tayari taswira hasi. Hakuna gharama kubwa kuibadilisha na kuanza upya.
 
Ila mkuu hatokubali jina liwe Air Kilimanjaro sanasana atapendekeza Air Victoria au Air Serengeti.
Ushauri wako mzuri, asipouchukua nitashangaa.
 
Naunga mkono hoja kwa 100%, hata nembo ya twiga haujakaa vyema maana Twiga wapo kila nchi hata hata Dubai wanazo twiga..nembo nzuri ya taifa ingekuwa Mlima Kilimanjaro au Ngorongoro/Serengeti...Ningeshauri tuondoe Twiga tuweke Kilimanjaro maana ndio utambulisho mzuri wa Mtanzania. Zamani KQ walianza kuweka Kilimanjaro ila naona sasa wamekuwa wapole baada ya kuona tunakuja kwa kasi...
 
Naunga mkono hoja, itakuwa safi sana kuvunja majina machafu ambayo yamelilifilisi taifa letu kama ATCL !!
 
HONGERA LIZABON.

Jina jipya la Shirika liwe: TANZANIA AIRWAYS

C.E.O wake mpya nampendekeza: BOSS ALIYEWAHI KUPIGA KAZI AKAONDOLEWA NA WAZIRI MWAKYEMBE KWA FITINA NA UNDUGUNIZATION.

NAAMINI SHIRIKA LITA KUWA JIPYA NA LENYE KASI YA MAGUFULI.
 
Back
Top Bottom