Ushauri kwa uongozi wa majiji hasa Dar; nyumba za bati zote eneo la jiji lazima zipakwe rangi ya paa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Naomba kutoa ushauri kwa uongozi wa halmashauri za majiji yote ya Tanzania, na ikiwezekana hata mikoa na wilaya.

Zitungwe sheria kwamba nyumba yeyote iliyoko ndani ya eneo la jiji au mjini, kila baada ya miaka mitano ni lazima ipakwe rangi ya paa (roof paint) ili kupendezesha mji na pia kuendana na mazingira.

Kwa mfano hapa Dar, ukiwa unatua kwa ndege, Dar es Salaam inaonekana chafu sana kwa juu, na tatizo ni mabati ambayo yameathiriwa na kutu.

Halmashauri za majiji na miji zinaweza kuamua utaratibu wa rangi uweje, labda kutegema eneo.

Na sisi watu binafsi tuliojenga mijini, basi ukiwa na nyumba ya bati jitahidi angalau uipake rangi ya bati kama bati zako sio za rangi. Tusingoje kusukumwa na sheria.
 
Nilidhani unataka mabati yadumu zaidi na kuokoa pesa za watu kumbe ni ule urembo wakati unatua na ndege.
 
ni kweli kabisa uko sahihi. Paa kama halijapakwa rangi nilinaashiria nyumba haijaisha. Hi kutu hii kutu hii inapunguza maisha ya nyumba. Mabati ya kiwanda chaMwenge hata kama umenunua yenye rangiyatapauka mara moja. wanatuibia.

Jiji litunge sheria sawa kuthibiti.
 
Nilidhani unataka mabati yadumu zaidi na kuokoa pesa za watu kumbe ni ule urembo wakati unatua na ndege.

Ha ha ha! Mkuu, basi umeongeza na faida nyingine nzuri tu ya kupaka mapaa rangi. Si unaona penye wengi haliharibiki neno!
 
Posta.jpg
 
Nyumba zimejengwa kiholela mkuu hata hizo paa zikitiwa rangi bado tu ukiwa juu utaona uchafu uliopakwa rangi...
 
Ukishaona tu ramani haieleweki na nyumba ziko katika mpangilio mbovu ujue ya kuwa unaingia bongo
 
Back
Top Bottom