Ushauri kwa Serikali: Nashauri Serikali iwanyang'anye passport za kusafiria wale wote waliotukana, kudhihaki na kumsema vibaya Rais wetu

Kwako serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Mimi ni kijana mzalendo, niliyepata mafunzo ya kijeshi nikafundishwa kupenda taifa letu, nikafundishwa kulinda upendo na amani ya nchi yetu.

Ninao uchungu mkubwa juu taifa langu. Nimekuwa nikikerwa sana juu ya ndugu zetu wengine ni viongozi wale wanaoishi ughaibuni.

Hawa mabwana wamekuwa wakitukana, kudhihaki na kumdharau sana Rais wa nchi yetu na wamekuwa wakifanya hivyo kupitia mitandao ya kijamii.

Binafsi nimekuwa nikikerwa sana na hawa watu waliokosa hekima na hata chembe ya heshima na adabu ndani ya mioyo yao.

Pengine ni mihemuko ya kiasiasa walio nayo kutokana kujenga mifumo ya siasa za kishabiki ndani yao.

Mimi kama raia mwema na mzalendo wa kweli, nimekuwa nikiwaza kitu kwamba mbali na adhabu za kuwapeleka mahakamani naishauri serikali yangu iwaongezee na adhabu nyingine ya kuwanyang'nya passport zao za kusafiria kwasababu passport ni mali ya serikali kupitia taasisi yetu ya uhamiaji.

Hivyo nawaomba uhamiaji wawanyang'anye passport hizo kwasababu wemeshindwa kuzitumia kwa heshima na adabu.

Lakini pia nawashauri TCRA watafute vijana wabobezi kwenye fani ya mitandao ili wawafuatilie watu kama hawa popote walipo. Kwasababu haya mambo yanawezekana.

Mbali na kufuatilia wezi wanao tutapeli fedha kwenye mitandao, tafadhali TCRA isaidieni serikali kufuatilia taarifa za watu wanamna kama hiyo. Kama mmekosa vijana hao mnaweza kuomba ushauri kwenye kitengo cha mawasiliano nchini China wao wanafanyaje.

Ningependa swala la kunyang'nya passport lihusiane na watuhumiwa ambao wanaitukana Serikali wakiwa nje ya Tanzania. Pamoja na watuhumiwa ambao wanamtukana Rais wakiwa nje ya mipaka ya Tanzania.

Mfano mtuhumiwa anayewaita waandishi wa habari na kumtukana Rais pamoja na serikali ya Tanzania mbele ya waandishi wa habari hao nje ya mipaka ya Tanzania. Sasa kwa vile passport ambayo ni mali ya serikali ndio imempeleka huko na hiyo passport ni mali ya serikali, sio vibaya mtuhumiwa huyo akanyang'anywa hiyo passport.

Pili mtuhumiwa anaye kwenda kwenye kituo cha kurusha matangazo ya habari nje ya mipaka ya Tanzania na kuanza kulisimanga vibaya taifa letu pamoja na kumsimanga vibaya Rais wetu.
Sasa kwa vile passport ambayo ni mali ya serikali ndio imempeleka huko na hiyo passport ni mali ya serikali, sio vibaya mtuhumiwa huyo akanyang'anywa hiyo passport.

Kwa hivyo ili kumfunza adabu mtuhumiwa huyo inatakiwa anyang'anywe passport ili abaki ndani ya mipaka yetu ajifunze jinsi kuheshimu taifa lako akiwa nje ya mipaka ya taifa letu.

Mtuhumiwa mwengine ni yule ambaye anatukana viongozi kwa njia ya mtandao ila akiwa nje ya mipaka ya Tanzania. Anapata uhuru wa kufanya hivyo eti kwa vile yuko nje ya Tanzania.
Sasa huyu naye inatakiwa anyang'anywe passport ya serikali ili atulie ndani ya mipaka yetu ajifunze jinsi ya kuheshimu taifa letu.

Kama hujanielewa naomba urejee hii attachment
View attachment 1514597
Wenu katika ujenzi wa taifa,
Meneja wa Makampuni.
Mtu akiwa nje ya nchi akamtukana Raisi kuna compromise vipi National Interest or National Security? Watu wana maoni tofauti na mitazamo tofauti ya ki sera na kiuongozi, kukosoana kwenye dunia hii ya sasa hakukwepeki!!
 
Mtu akiwa nje ya nchi akamtukana Raisi kuna compromise vipi National Interest or National Security? Watu wana maoni tofauti na mitazamo tofauti ya ki sera na kiuongozi, kukosoana kwenye dunia hii ya sasa hakukwepeki!!
Mkuu naomba uwaze mara mbili mfano wewe umeenda kwa Trump. Then unaanza kumwambia Trump habari za kiongozi aliyepo madarakani huku ukimtusi Rais huyo, huoni kama unavujisha usalama wa taifa mkuu. Hahuoni kama unahamishia ikulu ya Tanzania Marekani.

Na unavyokwenda huko wewe unadhani lengo lako linakua ni lipi? kama sio kuomba, msaada hao beberu wakusaidie kumtoa huyo madarakani kwa interest zako wewe mwenyewe?
 
Kwako serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Mimi ni kijana mzalendo, niliyepata mafunzo ya kijeshi nikafundishwa kupenda taifa letu, nikafundishwa kulinda upendo na amani ya nchi yetu.

Ninao uchungu mkubwa juu taifa langu. Nimekuwa nikikerwa sana juu ya ndugu zetu wengine ni viongozi wale wanaoishi ughaibuni.

Hawa mabwana wamekuwa wakitukana, kudhihaki na kumdharau sana Rais wa nchi yetu na wamekuwa wakifanya hivyo kupitia mitandao ya kijamii.

Binafsi nimekuwa nikikerwa sana na hawa watu waliokosa hekima na hata chembe ya heshima na adabu ndani ya mioyo yao.

Pengine ni mihemuko ya kiasiasa walio nayo kutokana kujenga mifumo ya siasa za kishabiki ndani yao.

Mimi kama raia mwema na mzalendo wa kweli, nimekuwa nikiwaza kitu kwamba mbali na adhabu za kuwapeleka mahakamani naishauri serikali yangu iwaongezee na adhabu nyingine ya kuwanyang'nya passport zao za kusafiria kwasababu passport ni mali ya serikali kupitia taasisi yetu ya uhamiaji.

Hivyo nawaomba uhamiaji wawanyang'anye passport hizo kwasababu wemeshindwa kuzitumia kwa heshima na adabu.

Lakini pia nawashauri TCRA watafute vijana wabobezi kwenye fani ya mitandao ili wawafuatilie watu kama hawa popote walipo. Kwasababu haya mambo yanawezekana.

Mbali na kufuatilia wezi wanao tutapeli fedha kwenye mitandao, tafadhali TCRA isaidieni serikali kufuatilia taarifa za watu wanamna kama hiyo. Kama mmekosa vijana hao mnaweza kuomba ushauri kwenye kitengo cha mawasiliano nchini China wao wanafanyaje.

Ningependa swala la kunyang'nya passport lihusiane na watuhumiwa ambao wanaitukana Serikali wakiwa nje ya Tanzania. Pamoja na watuhumiwa ambao wanamtukana Rais wakiwa nje ya mipaka ya Tanzania.

Mfano mtuhumiwa anayewaita waandishi wa habari na kumtukana Rais pamoja na serikali ya Tanzania mbele ya waandishi wa habari hao nje ya mipaka ya Tanzania. Sasa kwa vile passport ambayo ni mali ya serikali ndio imempeleka huko na hiyo passport ni mali ya serikali, sio vibaya mtuhumiwa huyo akanyang'anywa hiyo passport.

Pili mtuhumiwa anaye kwenda kwenye kituo cha kurusha matangazo ya habari nje ya mipaka ya Tanzania na kuanza kulisimanga vibaya taifa letu pamoja na kumsimanga vibaya Rais wetu.
Sasa kwa vile passport ambayo ni mali ya serikali ndio imempeleka huko na hiyo passport ni mali ya serikali, sio vibaya mtuhumiwa huyo akanyang'anywa hiyo passport.

Kwa hivyo ili kumfunza adabu mtuhumiwa huyo inatakiwa anyang'anywe passport ili abaki ndani ya mipaka yetu ajifunze jinsi kuheshimu taifa lako akiwa nje ya mipaka ya taifa letu.

Mtuhumiwa mwengine ni yule ambaye anatukana viongozi kwa njia ya mtandao ila akiwa nje ya mipaka ya Tanzania. Anapata uhuru wa kufanya hivyo eti kwa vile yuko nje ya Tanzania.
Sasa huyu naye inatakiwa anyang'anywe passport ya serikali ili atulie ndani ya mipaka yetu ajifunze jinsi ya kuheshimu taifa letu.

Kama hujanielewa naomba urejee hii attachment
View attachment 1514597
Wenu katika ujenzi wa taifa,
Meneja wa Makampuni.
we nikikuita ni mjinga nafikiri unastahili huwezi kuwa na mawazo mufilisi kama haya hata kujipendekeza kumezidi kipimo
 
Mkuu naomba uwaze mara mbili mfano wewe umeenda kwa Trump. Then unaanza kumwambia Trump habari za kiongozi aliyepo madarakani huku ukimtusi Rais huyo, huoni kama unavujisha usalama wa taifa mkuu. Hahuoni kama unahamishia ikulu ya Tanzania Marekani.

Na unavyokwenda huko wewe unadhani lengo lako linakua ni lipi? kama sio kuomba, msaada hao beberu wakusaidie kumtoa huyo madarakani kwa interest zako wewe mwenyewe?
Piece of written masturbation! For how long you been flicking that bean?!
 
Huwezi ukampora mtu passport bila kufwata sheria ,haitauwa kirahis kama unavyofikir wewe
 
Kwako serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Mimi ni kijana mzalendo, niliyepata mafunzo ya kijeshi nikafundishwa kupenda taifa letu, nikafundishwa kulinda upendo na amani ya nchi yetu.

Ninao uchungu mkubwa juu taifa langu. Nimekuwa nikikerwa sana juu ya ndugu zetu wengine ni viongozi wale wanaoishi ughaibuni.

Hawa mabwana wamekuwa wakitukana, kudhihaki na kumdharau sana Rais wa nchi yetu na wamekuwa wakifanya hivyo kupitia mitandao ya kijamii.

Binafsi nimekuwa nikikerwa sana na hawa watu waliokosa hekima na hata chembe ya heshima na adabu ndani ya mioyo yao.

Pengine ni mihemuko ya kiasiasa walio nayo kutokana kujenga mifumo ya siasa za kishabiki ndani yao.

Mimi kama raia mwema na mzalendo wa kweli, nimekuwa nikiwaza kitu kwamba mbali na adhabu za kuwapeleka mahakamani naishauri serikali yangu iwaongezee na adhabu nyingine ya kuwanyang'nya passport zao za kusafiria kwasababu passport ni mali ya serikali kupitia taasisi yetu ya uhamiaji.

Hivyo nawaomba uhamiaji wawanyang'anye passport hizo kwasababu wemeshindwa kuzitumia kwa heshima na adabu.

Lakini pia nawashauri TCRA watafute vijana wabobezi kwenye fani ya mitandao ili wawafuatilie watu kama hawa popote walipo. Kwasababu haya mambo yanawezekana.

Mbali na kufuatilia wezi wanao tutapeli fedha kwenye mitandao, tafadhali TCRA isaidieni serikali kufuatilia taarifa za watu wanamna kama hiyo. Kama mmekosa vijana hao mnaweza kuomba ushauri kwenye kitengo cha mawasiliano nchini China wao wanafanyaje.

Ningependa swala la kunyang'nya passport lihusiane na watuhumiwa ambao wanaitukana Serikali wakiwa nje ya Tanzania. Pamoja na watuhumiwa ambao wanamtukana Rais wakiwa nje ya mipaka ya Tanzania.

Mfano mtuhumiwa anayewaita waandishi wa habari na kumtukana Rais pamoja na serikali ya Tanzania mbele ya waandishi wa habari hao nje ya mipaka ya Tanzania. Sasa kwa vile passport ambayo ni mali ya serikali ndio imempeleka huko na hiyo passport ni mali ya serikali, sio vibaya mtuhumiwa huyo akanyang'anywa hiyo passport.

Pili mtuhumiwa anaye kwenda kwenye kituo cha kurusha matangazo ya habari nje ya mipaka ya Tanzania na kuanza kulisimanga vibaya taifa letu pamoja na kumsimanga vibaya Rais wetu.
Sasa kwa vile passport ambayo ni mali ya serikali ndio imempeleka huko na hiyo passport ni mali ya serikali, sio vibaya mtuhumiwa huyo akanyang'anywa hiyo passport.

Kwa hivyo ili kumfunza adabu mtuhumiwa huyo inatakiwa anyang'anywe passport ili abaki ndani ya mipaka yetu ajifunze jinsi kuheshimu taifa lako akiwa nje ya mipaka ya taifa letu.

Mtuhumiwa mwengine ni yule ambaye anatukana viongozi kwa njia ya mtandao ila akiwa nje ya mipaka ya Tanzania. Anapata uhuru wa kufanya hivyo eti kwa vile yuko nje ya Tanzania.
Sasa huyu naye inatakiwa anyang'anywe passport ya serikali ili atulie ndani ya mipaka yetu ajifunze jinsi ya kuheshimu taifa letu.

Kama hujanielewa naomba urejee hii attachment
View attachment 1514597
Wenu katika ujenzi wa taifa,
Meneja wa Makampuni.
Kwa kweli una muda was kupoteza kuandika huo utumbo.wanyang'anywe passpot ili iweje.passport ni mtu,taasisi au ni Mali ya watz wote?kila mtu Ana uhuru wa kutoa mawazo yake na huo uhuru uko kikatiba ili mradi tu haivunji hiyo katiba.
 
Kumbuka passport sio kadi ya kliniki kusema kuwa watu wanapewa bure.
Passport zinanunuliwa kwa pesa 150K,JMT imedhamini raia wake kupitia passport.
Na hiyo serikali inayotukana viongozi wa upinzani na wananchi wenye kutofautiana nao kiwawazo tuwanyang'anye nini??
Nakushauri mleta mada weka jina lako halisi viti maalumu bado kuna nafasi za kumwaga.
 
Mkuu naomba uwaze mara mbili mfano wewe umeenda kwa Trump. Then unaanza kumwambia Trump habari za kiongozi aliyepo madarakani huku ukimtusi Rais huyo, huoni kama unavujisha usalama wa taifa mkuu. Hahuoni kama unahamishia ikulu ya Tanzania Marekani.

Na unavyokwenda huko wewe unadhani lengo lako linakua ni lipi? kama sio kuomba, msaada hao beberu wakusaidie kumtoa huyo madarakani kwa interest zako wewe mwenyewe?
Sawa, hebu twende taratibu. Nadhani kupinga kilicho kibaya kwenye ngazi ya kimataifa sio kosa na wala sio kudhalilisha. Inawezekana nafasi ya kukipinga mkiwa ndani ya Nchi haiwezekani tena, lazima utumie njia mbadala.

Sasa chukulia mfano mtu kama Tundu Lissu alivyonyanyaswa, amefunguliwa kesi za ajabu ajabu, za uchochezi wakataka na kumpima mkojo juu . Amepigwa risasi ndani ya makazi ya wabunge, waligoma kumtibu mpaka Bunge lipate ruhusa kutoka kwa Rais, polisi hawajafanya uchunguzi wanasema mpaka victim mwenyewe arudi nchini (maana nyingine ni kwamba angekufa kusingekuwa na uchunguzi), walizuia maombi kwaajili yake, wamekamata watu waliovaa Tshirt za "Pray for Lissu", wamezuia watu wasitoe damu hospitalini,,,haya yote amefanyiwa yeye unategemea akiwa huko nje atamuongelea vipi Raisi wa Nchi na vile yeye ndiye mhanga wa matendo ya Serikali??


Alafu chukulia mfano mwingine - unaongozwa na Serikali ambayo haifuati utawala wa sheria, watu wanabambikiziwa kesi za uongo, wenye mawazo mbadala wanaonewa na kunyanyaswa, watu wanawekwa mahabusu miaka zaidi ya saba kesi zao haziamuliwi (Masheikh), wafanyabiashara wananyanyaswa kwa kunyangwa mali zao (wa bureau de change Arusha) au kufunguliwa kesi za uhujumu uchumi ili tu kukwapua mali zao kwa nguvu, wabunge wanafutwa uanachama alafu spika hawaondoi bungeni kama sheria inavyotamka wazi, chaguzi haziwi huru (mfano chaguzi za serikali za mitaa), alafu Serikali hiyo hiyo ikaondoa haki ya mtu binafsi au taasisi kuishitaki kwenye Mahakama ya Afrika (African Court on Human and Peoples' Rights). Unategemea watu watakimbilia wapi kuomba msaada?
 
Back
Top Bottom