meeku
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 569
- 108
Kwanza nianze kuwapongeza madaktari kwa kazi nzuri waliyoianza. Ni wazi kuwa kazii hii ikifanikiwa vyema itaokoa maisha ya watanzania wengi ambao hawana fedha za kutibiwa Apolo. Anayeona kuwa madaktari wanafanya vibaya basi vyema akaelimishwa.
Ni ajabu kuambiwa kuwa hospitali za serikali zina City scan moja tu iliyopo Muhimbili na ambayo imeharibika miezi saba iliyopita. Ni aibu kwa taifa ambalo viongozi wake wanazii kujilimbikizia mali kila kukicha huku wananchi wakifa kwa kukosa matibabu stahiki. Kwanza ni machungu ya muda na wananchi tunapaswa kuunga mkono juhudi hizi ili kuwajibisha viongozi hawa ambao kwa lugha rahisi tunaweza kuwaita "majizi".
Ombi langu. Wananchi tuunge mkono juhudi za madakatari na zifanyike juhudi za kuchangia ili mwanamapinduzi kiongozi r. Ulimboka apate matibabu na aweze kurudi kwenye vita. Lakini wapo madaktari ambao wameanza kutolewa kafara. Ningeomba zifanyike juhudi za maksudi ili wachangiwe chochote cha kuwafanya waendelee na mapambano. Hizi ni mbinu za kudhoofisha na ni vyema tuwe nao pamoja. Leteni namba za Tigo pesa na M-pesa tuchangie.
Tatu Dr Ulimboka aenziwe kwa mchango wake na ikibidi historia iandikwe.
naomba tujiulize ufisadi ni kiasi gani umefanyika hapa nchini ambao ungekomboa nchi hii. Ni aibu kwa viongozi wa nchi hii.
Noamba kuwakilisha.
Ni ajabu kuambiwa kuwa hospitali za serikali zina City scan moja tu iliyopo Muhimbili na ambayo imeharibika miezi saba iliyopita. Ni aibu kwa taifa ambalo viongozi wake wanazii kujilimbikizia mali kila kukicha huku wananchi wakifa kwa kukosa matibabu stahiki. Kwanza ni machungu ya muda na wananchi tunapaswa kuunga mkono juhudi hizi ili kuwajibisha viongozi hawa ambao kwa lugha rahisi tunaweza kuwaita "majizi".
Ombi langu. Wananchi tuunge mkono juhudi za madakatari na zifanyike juhudi za kuchangia ili mwanamapinduzi kiongozi r. Ulimboka apate matibabu na aweze kurudi kwenye vita. Lakini wapo madaktari ambao wameanza kutolewa kafara. Ningeomba zifanyike juhudi za maksudi ili wachangiwe chochote cha kuwafanya waendelee na mapambano. Hizi ni mbinu za kudhoofisha na ni vyema tuwe nao pamoja. Leteni namba za Tigo pesa na M-pesa tuchangie.
Tatu Dr Ulimboka aenziwe kwa mchango wake na ikibidi historia iandikwe.
naomba tujiulize ufisadi ni kiasi gani umefanyika hapa nchini ambao ungekomboa nchi hii. Ni aibu kwa viongozi wa nchi hii.
Noamba kuwakilisha.