Ushauri kwa Jeshi la Polisi Tanzania kitengo cha Intellejensia na Upelelezi kwenye masuala ya Mita

Civilian Coin

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
2,305
4,334
Ushauri kwa Jeshi la Polisi Tanzania kitengo cha Intellejensia na Upelelezi kwenye maswala ya Mitandao ya kijamii.

Jeshi la Polisi ni kama bado hawajajua jinsi ya kukabiliana na tuhuma za uhalifu wa mitandao ya kijamii. Kitendo hiki cha mapungufu kwa jeshi letu upande wa mitandao watajikuta kila mtu wanamfunga au kumpa adhabu asiyositahili.

Nimeona na kujifunza mengi kupitia makosa ya wengine na ya kwangu. Nini ambacho jeshi la polisi linapaswa kufanywa.......

1. Hakikisheni mnaifahamu mitandao yote iliyopo Duniani mfano...facebook, twitter, whatsap, instragram, linkeldn, spice, n.k baada ya kuifahamu ndipo mtajua mnapambana na nini.

2. Mnapashwa kujiunga na mitandao hii ya kijamii ili kujua Dunia inaendeshwa vipi.

3. Mnatakiwa kujua jinsi mitandao hii inavyofanya kazi kama Comment, Like, Share, tweet, post, status, memory status, love, n.k kwa kujua hivi mtajua ni wapi mtu mnaweza kumuokoa mtu anayetuhumiwa.

4. Kuvamiwa Akaunti za wengine..HACK....jeshi linapashwa kujifunza kuzijua program zote za ku hack na jinsi yaku hack ili kuepuka kuwaweka Sello kina Deogratius Kisandu kwa makosa ya kuhakiwa.

5. Nje ya kuchunguza simu za wahusika ni lazima mjue kwanza tabia za mitandao.

6. Mnapshwa kujua kuwa Mitandao ya kijamii habari zake nyingi huwa ni Nusu ukweli mpaka pale zitakapozihirika. Na hivyo msiwe watu wakukurupuka kukamata watu. Huko majuu Mh. Trump akikashifiwa mitandaoni na yeye anawajibu mitandaoni, fatilieni Akaunti zake ndio mtajua nini kinachoendelea huko majuu.

7. Mtu mwingine kutumia simu ya mwingine kuposti mambo ambayo sio safi, kesi kama hizi kwa mitandao ya kijamii hazina maana maana siku hizi mtu kama ana uadui na Fulani anamtegeshea simu yake halafu anapost anachokijua na mnaenda kuhukumu mtu ambaye hajahusika kisa tu simu yake imetumika. Hapa muwe makini katika kumsikiliza mwenye simu.

8. Siku hizi kuna tabia ya watu kutengeneza Akaunti fake kwa jina la mtu Fulani ili tu kumuaibisha mtu Fulani na baada ya hapo hizo akaunti hutoweka ghafla baada ya uchafuzi. Ndio maana utasikia Mbunge Fulani analalamika kuwa mimi sina akaunti facebook ya namna hiyo.

9. Mnapashwa pia kuzijua tabia za michezo michafu ya kisiasa ili wakati mwingine msiingilie mambo yao bali fanyeni kazi kwa yale yanayowahusu tu. wanasiasa siku zote kazi yao ni kuchonganisha na kufitinisha mkijakushituka mmetesa watu bila kutarajia.

Kwa leo tuanze na hayo.

Deogratius Nalimi Kisandu

Mtemi Kiongozi wa chama tarajiwa cha ACA.
 
Deo una akili Sana na unaona mbali watu wanaokuchukulia umechanganyikiwa ni wazembe wa kuelewa.

Wanasema nimechanganyikiwa kwa kuwa nasema UKWELI, unafikiri nikiongea PUMBA watasema mimi nimechanganyikiwa.....hakuna kitu kama hicho.
 
Wanasema nimechanganyikiwa kwa kuwa nasema UKWELI, unafikiri nikiongea PUMBA watasema mimi nimechanganyikiwa.....hakuna kitu kama hicho.
SAWA Ila nakushauri hoja zako nzuri Sana Ila usiingize Sana mambo binafsi hasa ya familia kwani ni rahisi Kwa maadui kukushambulia.. Baki kwenye hoja za utaifa.. Ubarikiwe Sana
 
Huyo nae anawafundisha kazi polisi.Kuna mijitu imebobea katika masuala ya IT huko polisi.Kuna watu wanapiga patrol mitandaoni kama askari wanavyo patrol mitaani.
 
I also kudu be IGP.....deriva your passport here...... u have your pass here?? I will show u ooohhhh.....wish I kudu be CDF!
 
Deogratius Kisandu please brother go back Dodoma...kuleeee barabara ya Chang'ombe. Go there and try to finish what you have just started.


Please kaka nakuomba.
 
Mhh! kwa hiyo zile harakati zoote ya ACA kumbe zilikuwa ni kazi ya hackers?
 
Back
Top Bottom