Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,509
- 9,296
Kila jambo huja na maajabu yake! Katika hali ya kushangaza, mwanaume mmoja anashikiliwa na polisi nchini Urusi kwa kosa la kuwafyatulia risasi na kuwaua watu watano kwa madai kuwa waligoma kupunguza sauti zao wakiwa karibu na nyumba yake, huku kukiwa na marufuku ya kutembea nchini humo.
Tukio hilo linadaiwa kutokea katiak Kijiji cha Yelatma katika mkoa wa Ryazan ulioko Magharibi mwa nchi hiyo. Eneo hilo liko katika marufuku ya kutoka nyumbani, wakati nchi hiyo ikiwa inapambana na kusambaa kwa virusi vipya vya corona (covid-19).
Kamati ya Upelelezi ya Urusi imeliambia Shirika la Habari la TASS kuwa Mwanaume huyo alianza kubishana na jirani zake akiwa amesimama kwenye kibaraza (balcony) ya nyumba aliyokuwa anaishi, wakati wao wakiendelea kuongea kwa sauti ya juu.
Ilieleza kuwa waliouawa ni pamoja na wanaume wanne na mwanamke mmoja. “Aliwataka vijana hao wanne na msichana mmoja ambao walikuwa wanaongea kwa sauti ya juu karibu na nyumba yake kuacha mara moja, lakini walipoendelea aliwafyatulia risasi na kuwaua wote,” ilieleza.
“Maafisa wa Polisi walifika katika eneo la tukio na kumkamata wanaume huyo mwenye umri wa miaka 32,” taarifa ya Idara ya Wizara ya Mambo ya Ndani ilikaririwa na TASS, Jumapili, Aprili 5, 2020.
============
A man in Russia has shot dead five people for talking loudly outside his house late in the evening.
Police said the shooting happened in the village of Yelatma, in the Ryazan region about 200km (124 miles) south-east of Moscow.
The area is currently under lockdown due to the coronavirus.
Investigators say the man initially complained to the group from his balcony, and an argument broke out. He then opened fire with a hunting rifle.
The four men and one woman “died of their injuries on the spot” at around 2200 on Saturday, the Investigative Committee said.
The suspect, who has not been named, was later arrested.
His apartment has been searched and the weapon seized.