Urais wa ZZK 2015 Kupitia Chadema: Kwa nini Wanatetemeka!, Kuweweseka! na Kutishika?!.

Status
Not open for further replies.


Kwani ni Nani Anatetemeka? ni Nani Anaweweseka? na ni Nani Anatishika?
Ni wewe ndie Unayeweka UPUUZI wa UDINIl UKABILA kwenye MASUALA ya ZITTO KABWE Ni wewe ndie Unayeweweseka kama ZITTO KABWE si kiongozi asiyefaa...

Embu tueleze ni tangu lini ZITTO KABWE amefanya MIKUTANO ya KUZUNGUKA nchini kama VIONGOZI wenzake wa CHADEMA kutafuta WANACHAMA WAPYA zaidi ya KUZUNGUKA kwa NDEGE na MTUKUFU RAIS? au MAMA SPIKA?

EMBU TUAMBIE ni lini AMEONGELEA kuhusu CHADEMA zaidi ya kuongelea U-MIMI KUGOMBEA URAIS? Sasa ni kwanini Unamkumbatia MBINAFSI; MPEKEE; MCHOYO; ILI AKIVURUGE CHAMA cha UPINZANI kinachoitwa CHADEMA?

Wa CCM wapo WENGI wanaotaka kugombea URAIS; lakini UMESIKIA wanaongelea UDINI; UKABILA ? ni Kwanini wewe UNAONGELEA UPUUZI HUO? INAONYESHA JINSI ULIVYOFILISIKA KISIASA...



What I'm telling you is this; Remember what Julius Nyerere Once Said... And then the harder they come...The harder they fall...One and for all

Did you know what kind of people NYERERE was referring to????

Mkuu huyu Pasco na mwenzake wako kwenye mission maalum ya kuangamiza CDM.Sasa wamepanic baada ya kuona wanachadema wamesimama kidete kuhami chama chao.Pia wameshtuka kuona mwasisi wa chama ameingia ulingoni kukemea uhuni wowote wa kutaka kuvuruga chama.
Niwaeleze Pasco na wenzake kwamba CDM ipo macho usiku na mchana na kitengo cha Intelejensia kimeongezewa masaa ya kufanya kazi.Mungu alivyo mkuu wameanza fujo zao mapema sana.Pasco anajidhalisha kupita kiasi.
 

Hitimisho.
2015 inakuja, kuna vyama vinajipanga kuchukua nchi huku vingine vinajipanga kutetea viti vyao. Katika
kutimiza azma hiyo, viko vyama vinajipanga kimipango mkakati huku vikieleza vitafanya nini, na kuna
vyama vinaendeleza mahubiri, kucheza makida makida na kuchezea shilingi chooni!. Siku ya siku ikifika,
hatutaki watu waje kutulilia tena humu as if hawakuambiwa!.
ZZK ametangaza tuu nia, msitetemeke,
msiweweseke wala msitishike, just do the right thing and and in doing that right thing, make sure you do it
right!.


Naomba kuwasilisha.

Asante.

Pasco.
[/QUOTE]
 
Ban refu lililo nipata nadhani litakuwa ni la mwisho sasa,zitto ni mwana ccm alijivika koti la chadema na akijifanya ana harakati za kivyake vyake ndani ya ccm nadhani anapangawishwa na ule ulikuwa unampenda pindi akiwa bungeni akipiga mabomu mafisadi,lakini kwasasa tangu aanze urafiki na dhaifu na magamba watu tumeona sasa nini anacho kitaka na nyuma yake yupo nani,analeta tabia za uccm chadema za kutengeneza makundi ndani ya cdm akidhani atawea kukidhoofisha chadema ili kule walikomwahidi vijiela na nafasi za uwazir mkuu atafanikiwa,kifupe tunamtaka Dr.slaa tu!yeye na uroho wake haoni hata aibu slaa anapendwa na watu wote sio yeye ndumilakuwili fisadi mkubwa huyu wa ccm
 
Mkuu pasco salaam,
Kwanza nikupongeze kwa mawazo yako mazuri na yenye nia na kusudi jema,pamoja na maelezo yako ambayo msingi wake ni kujenga hoja napena nami niseme lango.

Kwanza nakubaliana nawe juu ya watu wanao mpinga Mh.Zitto kwa kutangaza nia yake ya kugombea urais 2015 kwa tiketi ya CDM,mimi ni mwanachama wa CDM pasi na kificho lakini tuwe wakweli kwa dhamira zetu na si kwa hisia ama husuda kwa Mh.Zitto,kazi ya ujenzi wa chama haijakwisha,chama hakijapata kile kinachotakiwa,chama bado kinaendelea kutoa elimu na bado kinajitambulisha ili kieleweke kwa watz walio wengi,ni kweli mwitikio ni mkubwa nasi twawapongeza viongozi wetu Mh.Zitto akiwemo kwa kazi hii ya kujivunia.Na mafanikio haya hayana mwenye hodhi nayo bali watoa elimu na wapokeaji kwa mwitikio then team hiyo inaendelea kusambaza elimu hii kwa wengine.

Ndugu pasco,napenda pia kusema kama ambavyo umelisemea kuwa jambo la mtu mwenye nia ya kujenga nchi yake atonesha nia ya kujijenga kuanzia nyumbani,japo kuna msemo kuwa Nabii hasifiki kwao lakini kwa Mh.Zitto alikuwa anakubalika sana ktk chama,bado ankubalika sana katika chama na bado ni imani yangu kama atkuwa msikivu ataendelea kukubalika ndani ya chama.Binafsi sichangii hoja yako kwa kigezo cha Udini,Ukabila,Ukanda,woga,Umri ama vyovyote kwa maana ya ubaguzi but kwa kusukumwa na uzalendo wangu kwa Taifa langu.

Ndugu Pasco,Mh.Zitto amekuwa na nia ya kuwa Rais wa Tanzania kwa muda mrefu na naamini hajasukumwa na udini,wala ukabiala ama ukanda isipokuwa utashi wake,Mh.Zitto awali alionesha nia yake kwa vitendo,alichapa kazi usiku na mchana na amekuwa akifanya kazi ya kujenga chama kwa moyo mmoja TATIZO kwanini anatumia nguvu kujinadi ilihali anatambua huu si muda wa watu kutangaza nia?Kwanini wakati mgombea Urais kupitia chama chake mwaka 2010 wakat anapita kuzungika kutafuta kura yeye alianza kutangaza nia ya kugombea Urais 2015?Mimi huwa nakubali pia uwezo wa wenzangu katika mambo wanayoyaweza,lakini kwa Mh.Zitto imedhihirika ni tofauti,anajiona yeye ni ni mjuvi wa kila kitu je?aikiwa Rais atakubali kushauriwa?Kama kabla ya kuingia ktk nafasi kubwa ya utumishi katika nchi ameanza kuanza kuonyesha kupuuza wengine mapema je akiwa huko ndani itakuwaje?,Sikatai Rais si lazima achukue uamuzi wa mtu but si ktk kila jambo,anyways eneo hili tulihitaji kumuona Mh.Zitto akishirikiana na wenzake ktk kujenga chama kama ambavyo wakati wa Operation Sangara ilikuwa,but yeye sasakazi yake ni kujenga makundi kwa nin watu wasiogope,haya makundi kwa faida ya nani?Kiongozi ambaye watz twamtaka ni yule anashirikiana na wenzake pasi kuwa na mashaka nae.

Mh.Zitto ameanza kupoteza imani miongoni mwa wanachama na hata viongozi wake,alianza kuleta hoja ya umri wa mgombea upungue akiwa na lake jambo mfukukoni,kuwa kigezo cha umri katika katiba mpya kikipita basi yeye aweze kugombea,huu ni uchoyo wa kweupe,kuna maana gani CDM kupinga ufisadi wakati nasi tunapika mafisadi maana kwa tabia ya kujitazama kuwa muda ukifika nitakuwa sina sifa kugombea na kuanza kutengeza mazingira yake kupenyeza ajena zake siafiki,mi nadhani angekuwa ni mwenye nia njema angesubiri muda ufike Watz si vichaa kama yeye angeonekana ndiye mwenye sifa zaidi wangempa,kutangaza nia sio tusi lakini umetangaza wakati stahiki?


Pasco,naheshimu mawazo yako na nina haki ya kukusikiliza pia una haki ya kuzungumza jambo lolote ilimaradi hauvunji sheria je kusema Tanzania kwasasa inahitaji kiongozi atakaye jenga uchumi lakini kazi hii kamwe haitoweza kufanywa na mtu aliyezaliwa kabla ya UHURU,inamaana gani?Kuzaliwa kabla ya uhuru kuna maana gani na kuzaliwa baada ya uhuru kuan maana gani katika kujenga uchumi wa nchi?umri wa mtu unajengaje uchumi kwa nchi?Uzalendo si kugawa watu kwa namna yoyote ile isipokuwa kwa manufaa ya Taifa.So mtu anaekuja na kauli za Ukanda(Kafulila),Umri(Mh.Zitto) na wengine na hoja za mara udini n.k iantusaidia nini kama Taifa,kwanini tusiogope?Kwanini tusiwe na mashaka nae?

Mkuu pasco,wanaCDM wanapata mashaka na si woga toka kwa M.Zitto kwa kuwa muda mwingi anaonekana anpinga na wezake hadharani ama kwa matendo yake,Msimamo wa chama Mh.Zitto amekuwa kinyume nao,anapenda kuwa na mamboa yake pekee yake.Katika chama hakuana maamuzi ya mmoja BALI maamuzi ya PAMOJA,ndivyo nchi inavyoongozwa,serikali haiongozi na maamuzi ya mtu kulala na kuamka na kuto hisia zako bali mawazo ya wengi na KUKUBALIANA.So bro mawazo yangu mimi si maandiko ya Vitabu Vitukufu kwamba ndiyo mwisho naamini jamvi lina watu wengi na wenye mawazo bora zaidi.Ila watz wa sasa ni watu makini kila aina ya tukio wanalichukulia uzito na si kupokea tu kama vile wananunua Mbuzi kwenye guni.So hayo yote uliyotaja kama watz wanajenga hoja kwa misingi ya Uoga,Udini,Ukabila,ukanda,Umri na n.k pia tambua kuwa watz wasingependa kurudia makosa.

Mwisho,Kwa nature ya position ya Urais mtu akitiliwa mashaka tu ameondokewa na sifa ya kuwa Rais so kama mtu makini sasa ni niwakat muafaka kwake kuendelea kuuota urais kwa kuwa mzalendo katika nchi hii si MhZitto pekee labda atuelze kuna biashara gani anataka kwenda kuifanya kwa mfumo anaotumia kuutaka Urais,Katu hatuwezi kumwamini mtu mroho wa madaraka,maana anatumia kila njia kifikia azma hiyo.Maana kazi anayoifanya kwa sasa mara kutumia jamaa zake kumjengea hoja na kuhakikisha anachafua wenzake kitu ambacho sio kizuri kwa mtu mwenye busara ya kuutaka urais.
 
PASCO NIMEKUSOMA!! ndio maana siku zote nasema human psychology ni kitu very complex. JAMBO moja ninalo kushangaa ni kwanini unamuunga mkono ZZK agombee Urais wakati hata kutunza familia ya mke na mtoto mmoja hajawahi.tamaa ya kwenda DISCO bado anayo.ukimsoma vizuri ZZK utagundua kuwa anadhani yeye ni mashuhuri kuliko CHADEMA kumbe siyo.
ZZK yafaa aelewe kuwa ndani ya CHADEMA kuna watu wanojua kuchambua mambo na kwamba hawana papara.yeye anabebwa na ccm wakati yupo CHADEMA anategemea nini? ukiona mtu anapendwa na hasimu wako ni lazima uchukue tahadhari.kwanini anapigiwa chapuo na wao (CCM)? Funzo kubwa CDM walipata kule MBEYA wakati wa uchaguzi mkuu wa2010 mtu akajitoa dakika za mwisho ili kupisha mgombea wa ccm apite,bila shaka alkuwa mamluki au alihongwa.huyu nae ana kila dalili kuwa huko tuendako atafanya hivyihivyo.
Humu jf kuna kura ya maoni inaendelelea,kwa taarifa yako ameachwa kwa mbali sana na Dr wa ukweli.Nadhani hata akishindanishwa na TUNDU LISSU atatupwa mbali hivyohivyo.kifupi kura za maoni ndani ya CHADEMA zitapigwa na wana CDM.Aidha kuto shiriki katika mikutano ya M4C kwasababu yoyote ile kumemtoa katika kundi la watu makini na ambao wako focused.
ndani ya CHADEMA hakuna udini,ukabila,ukanda, wajuaji na nk.kuna wana chama wenye dhamira moja tu kuiondoka ccm madarakani ifikapo 2015. nani atapeperusha bendera atajulikana baadae lakini SIYO ZZK. NEVER.
 
Pasco unahangaika sana,unakoelekea ni kupoteza credibility tu au tukubali ndo kutumiwa? Umekazana sana na Zitto haujapita muda ulishaibuka na thread ile ya "....ngoma ikilia sana". Una tatizo gani? Saa ingin yafaa kutulia na kuangalia mambo yanavokwenda
 
UKWELI HUSEMWA:

Pasco, kwanza nakubaliana na baadhi ya maoni yako, halafu niseme, wewe pia unaonekana uko kwenye kundi la wakweli lakini wanaotawaliwa na uoga.

ZZK anaendesha siasa mpya zinazoendana na dunia hii ya sasa. ZZK anatenda kwa kusukumwa na kauli mbiu ambayo walatini wanasema, audere est Facere au kwa kimombo, To Dare Is to Do.

Wengi humu wanamtaka afanye siasa za mazoea ambazo ndizo zinaitafuna CCM na ambazo ndiyo hizo hizo wanazozipigia kelele humu JF na kusema kwa siasa hizi CCM imefilisika.

Halafu naomba ujue kuwa, Kwa taratibu na katiba ya CDM, Chama hakimshauri mtu kugombea kama unavyopenda iwe na kama kikifanya hivyo kitakuwa kimevunja taratibu za demokrasia ndani ya chama. Kazi ya chama ni kumteuwa mgombea ndani ya taratibu zake kati ya waliojitokeza kutaka kuteuliwa.

Remember, politics is about opportunism and smartness. na kwa hili, ZZK anacheza vizuri karata.

Maswala ya 'kuonyesha nia na kutangaza rasmi nia' yanaangukia kule kule kwenye siasa za mazoea ambazo kusema kweli tumezichoka na hatuzihitaji tena nchini.

Katika nchi za demokrasia, rabsha anazozipata ZZK njiani ni za kawaida kabisa kwa sababu 'Mr President' ni jina analoitwa mtu mmoja tu katika kila nchi duniani.

Hii ndiyo demokrasia, acha hao wengine wasubiri chama 'kiwashauri' kugombea.
 
Hitimisho.
2015 inakuja, kuna vyama vinajipanga kuchukua nchi huku vingine vinajipanga kutetea viti vyao. Katika
kutimiza azma hiyo, viko vyama vinajipanga kimipango mkakati huku vikieleza vitafanya nini, na kuna
vyama vinaendeleza mahubiri, kucheza makida makida na kuchezea shilingi chooni!. Siku ya siku ikifika,
hatutaki watu waje kutulilia tena humu as if hawakuambiwa!.
ZZK ametangaza tuu nia, msitetemeke,
msiweweseke wala msitishike, just do the right thing and and in doing that right thing, make sure you do it
right!.

Naomba kuwasilisha.

Asante.

Pasco.
[/QUOTE]

Kwa kweli umenishangaza sana angali ahapo penye red. Hivi huyo ni nani anayemwogopa ZZK? Mbona namwona ni mtu mwepesi tu na mbona kukuruka zake zimezoeleka? Alijaribu uenyekiti 2008, akapigwa chini, akaja pupa zake kutaka Uongozi wa kambi ya upinzani bungeni akapigwa chini, sasa hili nalo asubiri tu aone kitakachotokea. Sio kwamba hatumpendi lakini kwa sasa (2015) hatufai ajaribu 2020 na kuendelea kama bado atakuwa kwenye siasa kwani natabiri tutakapompiga chini safari hii atakimbia siasa for good.

No!! No!! Zitto atusubiri kwanza, kama ana akili asikilize hili. Najua Kigoma Kaskazini hawamtaki tena, aseme tu atafutiwe jimbo lingine asimame kwenye Ubunge, lakini U-Amri Jeshi mkuu bado bado bado sana tu. Tunahitaji mtu bora zaidi, Akiona ngumu aende CHAUMA huenda akakubaliwa watakapopata usajili wa kudumu.
 
Nafikiri Pasco ana points kwa mtu ambaye kweli amesoma hii habari. Ninachokiona kwneye hizi comments ni hayo makundi tofauti ambayo ameyataja kweneye hiyo habari. Tujifunze kupevuka kisiasa na kuvumilia kweli anayoisema mwenzako hata kama ikiwa inakuudhi.
 
hilo la udini,ukabila,ukanda ni hisia tu
(umeungana na mtaji huo wa ccm)

haujasikika/kuonekana dhahiri kama upande wa pili
(lile tamko la uvccm pwani)
 
Pasco" Pasco,
UNAKUMBUKA MANENO YA MAMA MZAZI WA ZITTO “Namfahamu mwanangu. Ni mkorofi. Si msikivu.” JE HUYU ANATUFAA KUWA RAIS..Tafakari..


ZITTO Kabwe, naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amekuwa na mawasiliano ya karibu na na mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, imefahamika.
Kufichuka kwa taarifa za mawasiliano kati ya Zitto na Rostam kumekuja wiki moja baada ya gazeti hili kuchapisha mawasiliano kati ya Zitto na Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini (TISS), Jack Zoka.
Aidha, kufichuka kwa mawasiliano kati ya Zitto na Rostam kumekuja siku mbili baada ya mama mzazi wa Zitto, Shida Salum kunukuliwa akisema, “Mwanangu ni mkorofi.”
Mama Zitto alikieleza kikao cha Kamati Kuu (CC) ya chama chake kilichofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, “Namfahamu mwanangu. Ni mkorofi. Si msikivu.”
Kwa mujibu wa rekodi ya mwingiliano wa simu za mdomo na maandishi (sms) kutoka kwa Zitto kwenda kwa baadhi ya vigogo wa ngazi ya juu serikalini, TISS na Rostam, watu hao wawili wamekuwa wakijadiliana mambo kadhaa.
Miongoni mwa mambo ambayo yamekuwa yakijadiliwa na viongozi hao, yanahusu CHADEMA, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na taifa kwa ujumla.
Rostam ambaye CHADEMA imekuwa ikimtuhumu kuhusika katika kashfa mbalimbali za ufisadi, ni mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya CCM.
Gazeti hili limeshindwa kujua mapenzi ya Rostam kwa CHADEMA hadi kujipa jukumu la kujadiliana na Zitto juu ya “uhai bora” wa chama hicho.
Kwa mfano, Zitto na Rostam walifanya mawasiliano ya simu mara tano hapo tarehe 11 Agosti 2010. Simu iliyotumika katika mawasilino hayo, ni Na. +255756809535 ambayo hutumiwa na Zitto na +255754555555 ambayo hutumiwa na Rostam.
Mawasiliano hayo yalifanyika saa 07:08:35, saa 22:09:02, saa 22: 28: 39, saa 22:49:54, saa 22:44:37 na saa 22:45:09.
Wakati mawasiliano hayo yanafanyika simu ya Zitto ilikuwa inasomeka kuwa yuko Uzunguni, Dodoma, huku simu ya Rostam ikisomeka kuwa ilikuwa Area D, Dodoma.
Mawasiliano mengine yalikuwa katika maeneo tofauti. Mathalani mawasiliano ya Zitto na Rostam yalyofanyika 30 Novemba 2010 yalionyesha kuwa Zitto yuko Ohio, Ilala, Dar es Salaam. Yalifanyika saa 14:58:42, saa :16:41:58, saa 15:38:00, saa 16:09:56 na 17:48: 35.
Mawasiliano mengine ya Zitto na Rostam yalifanyika siku mbili kabla ya wabunge wa CHADEMA hawajakutana Bagamoyo.
Mawasiliano hayo yalifanyika tarehe 7 Desemba 2010 saa 07: 57:27, saa 14:32:08, saa 09:44:36 na saa 14:07:07.
Haijaweza kufahamika pia kiini cha mawasiliano kati ya Zitto, Zoka, Rostam na vigogo wengine wa serikali, CCM na usalama wa taifa.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu kutoka ndani ya kikao cha CHADEMA, awali mama Zitto alieleza masikitiko yake kuhusiana na taarifa mbalimbali zinazomhusu mwanawe.
“Najua mwanangu ni mkorofi. Lakini kuna njia ya kufanya kuliko kukitia chama msukosuko…Kila mara Zitto, Zitto, Zitto. Haya mambo hayana faida kwa chama,” alieleza.
Hata hivyo, vyanzo huru vya taarifa vimeeleza MwanaHALISI kuwa mpango uliopo ni kumtumia Zitto “kusambaratisha CHADEMA.”
“Kaka, nakuhakikishia kuwa upo ushahidi wa kutosha kwamba Zitto anatumika kuvuruga CHADEMA. Kuna baadhi ya vigogo ndani ya CCM na serikali, wanaomtia ujinga kwa kumueleza, ‘kwa hali ilivyo ndani ya CCM, wapo baadhi ya watu wanatamani kuondoka. Lakini hawawezi kwenda CHADEMA kwa sababu kinaongozwa na Mbowe (Freeman Mbowe),’” ameeleza mtoa taarifa.
Anasema, “Hivyo wanampampu Zitto kugombea uenyekiti. Wanataka Mbowe ang’oke na CHADEMA kisambaratike. Ni kwa sababu, wote wanaomtumia Zitto, wanajua kuwa huyu bwana mdogo hana uwezo wa kuongoza CHADEMA na haaminiki.”
Akiongea kwa kujiamini, mtoa taarifa anasema, “Ni mbinu zilezile zilizotumiwa NCCR- Mageuzi, ambapo baadhi ya vigogo wa idara ya usalama wa taifa walitumia fedha ili kumng’oa Marando (Mabere Marando), katika uongozi wa chama.”
Anasema taarifa kwamba wapo watu wanataka kuondoka ndani ya CCM na kujiunga na CHADEMA ni mkakati unaosukwa kwa ustadi mkubwa na baadhi ya vigogo wa serikali kwa kushirikiana na usalama wa taifa.
Inadaiwa ni katika mkakati huo, ndimo linapatikana jina la Rostam ambaye uongozi wa juu wa chama hicho umekuwa ukimtuhumu kuhusika katika kashfa mbalimbali za ufisadi nchini.
“Unajua ndugu yangu hapa Tanganyika, Rostam angependa sana awe na uwezo wa ku-control vyama vyote vinavyokua, hasa CHADEMA kwa sasa; ingawa uwezo wake wa kupenyeza unakuwa mgumu.
“Mkakati wake ni kumweka mtu wao katika uongozi wa juu wa CHADEMA ili waweze kumuendesha. Mpango huo ukifanikiwa, kina RA (Rostam) wataacha ugomvi na CHADEMA. Kwa sasa mtu wao ni Zitto. Na kuna mambo mengi ya siri ambayo RA amekubaliana na Zitto,” anaeleza mtoa taarifa mmoja ambaye yuko karibu na Rostam na Zitto.
Mjadala juu ya mwenendo wa mashaka wa maisha ya kisiasa ya Zitto, uliibuka baada ya katibu wa wabunge wa CHADEMA, John Mnyika kuwasilisha taarifa ya shughuli za kamati hiyo mbele ya Kamati Kuu.
Kikubwa kilichojadiliwa ni hatua ya Zitto kuongoza kikundi cha baadhi ya wabunge kusaliti maamuzi halali ya kamati ya wabunge wa chama hicho.
Zitto anatuhumiwa na wabunge wenzake kutotii agizo la kutoka nje wakati Rais Jakaya Kikwete anahutubia Bunge, 18 Novemba 2010.
Katika taarifa yake kwa CC, Mnyika alisema katika kushughulikia suala hilo, hakukuwa na lolote la kuviziana kama ambavyo baadhi ya wajumbe wamedai.
“Hakuna kanuni iliyovunjwa, wala hakuna kinachoitwa kuviziana. Wabunge walikuwa na hasira sana juu ya hatua ya Zitto na wenzake kutotii agizo la kamati na kupita katika vyombo vya habari kupotosha ukweli,” alisema Mnyika kwa sauti ya upole.
Akiongea kwa sauti ya kusisitiza, Mnyika alisema, “Mheshimiwa mwenyekiti, kwa kweli, wabunge walitaka hata kuwapiga wabunge walioasi makubaliano yao. Uongozi wa Kambi ukafanya juhudi kulipeleka mbele suala hili, angalau kupunguza munkari wa wabunge,” alieleza.
Ni katika kikao hicho cha wabunge kilichofanyika Bagamoyo, ndipo wabunge walipiga kura ya kutokuwa na imani na Zitto.
Kile kilichoitwa, “kuviziana” kiliibuliwa ndani ya kikao cha CC na Dk. Kitila Mkumbo, ambaye amenukuliwa akisema ameshutushwa na hatua ya wabunge kumhukumu Zitto wakati ni mgonjwa.
Alikuwa ni Benson Kigaila, mjumbe wa CC aliyeeleza viongozi wenzake umuhimu wa kujenga chama imara badala ya kuangalia mtu.
“Mtu aliyekosea, lazima aadhibiwe. Tusiangaliea kama ataanguka, au atanufaika. Kwa muda mrefu, chama hiki kimenufaika kwa makosa ya CCM, ambapo kutokana na makundi yanayokinzana, wameendelea kukumbatia maovu. Ni lazima chama kichukue hatua za kukabiliana na magenge haya,” alieleza.
Mjumbe mwingine wa CC aliyeongea kwa sharti la kutotajwa gazetini, ameliambia gazeti hili, “Yale mambo yalikuja kama taarifa, si vingenevyo. Jukumu sasa, liko kwa Zitto mwenyewe kujipima kama anaweza kuongoza watu ambao hawana imani naye.”
Baada ya kupeleka taarifa hiyo CC, wabunge wameeleza, “…Tunapeleka maamuzi yetu haya kwa Zitto. Anatakiwa kuamua ama kuachia ngazi au kusubiri hatua nyingine zinazofaa kuchukuliwa kwa mtu kama yeye katika kikao chetu kingine.”
Mara baada ya mjadala wa Zitto kwa CC kutoingilia maamuzi ya Kamati ya wabunge wake, ndipo uamuzi wa kuunda kamati ndogo ya “kumpa ushauri” Zitto ilipoundwa.
Kamati hiyo inaongozwa na Profesa Mwesiga Baregu.Wajumbe wake ni Nyangali Shilungushela, SylivesterMasinde na Mama Zitto.
Kazi ya kamati ya Baregu ni kufuatilia nyendo za Zitto, kumshauri jinsi ya kujibadilisha ili hatimaye arejee katika njia iliyonyooka.
 
Mkuu Pasco Mayalla

Pole sana nilikuwa sijakujibu muda mrefu maana naona kila siku anaangaika kwa ajili ya Zitto
Mimi ni CCM damu lakini nakuhakikishia kuwa Zitto anatumika wewe subiri true colour will show.......
Kama ilivyokuwa kwako baada ya kugundulika kuwa wewe ni mwanaCCM mwenzetu ukawa unasema
wewe ni independent advicer mara Political Analysist lakini yote kwa yote hakuna chochote na wewe your
true colour show at the end

Last:.................... Pasco Njaa Mbaya tujenge taifa letu tuache siasa za majungu................
i say its a true color thats why a i love it.njaa mbaya sana waungwana umempa ukweli wake kwa kweli sasa hivi tuko kule kwenye makanisa yaliyochomwa,na kusikitika kuh kamanda Barlow tulia kwanza na mambo ya zzk huyo mtoto bado hajafikisha 40yrs. mwambie aoe kwanza hatuchagui mabarchelor
 
PASCO Hongera kwa mawazo yako

Huyu jamaa i mean ZZK, ni mtu mwenye tamaa, mbinafsi, ndumilakuwili na sidhani HATA CCM YENYEWE WANAMTAKA kwa kiasi kikubwa namfananisha na wanasiasa wa KENYA....ni MROHO WAMADARAKA, siasa ZA KISASA ZINAENDESHWA NCHI ZENYE DEMOKRAISIA YA KWELI.

hUWEZI UKAENDESHA SIASA ZA KISASA KW A TAIFA KAMA LA tz ambapo wenye madaraka kila kukicha wanakandamiza wananchi achilia mbali wapinzani.. SASA HUYU MROHO WA MADARAAKA WENZAKE WANAJITAHIDI KUFUNGUA WANANCHI MACHO KWA KUW=AELEZA UKWELI YEYE ANATANGAZA KUGOMBEA URAISI

ZZK HISTORIA NA INIHUKUMU UTAISHIA KAMA KABURU na nakuonea huruma kwani bado kisiasa hujakomaa ila soon utasahaulika usipoacha UBINAFSI<MARINGO na kujiona wewe ni zaidi ya wenzako......kama bado unajiona jina lako i mean ZZK ni house hold kama azam products WAJIDANGANYA
 
i knew...only ben saanane and mchange would support hili bandiko!!!!huyu mtu pasco kweli mwandishi,manyuzi yake yanakuwaga marefu akiongelea point moja tu,.hawa walikuwaga mabingwa wa essay za history na gs enzi zile za high school..don't worry zitto is reading your posts,atakukumbuka kwenye ufalme wake atakapopewa uwaziri na ccm mwaka 2050
 
Kwenye mjadala ambao ni healthy kama huu sitashangaa kuona baadhi ya watu wakijadili ajenda za udini na ukabila zaidi.Kazi iliyopo Mbele ya CHADEMA nikuzidi kujiimarisha na kuahakikisha hatujiandalii mazingira magumu kisiasa huko mbele.Tutumie fursa hii iliyopo kwa kutazama na kujirekebisha sehemu inapotakiwa na kwa muda muafaka.Wapenda mabadiliko ambao ni great thinkers wanajua aina ya mijadala inayochochea mabadiiliko hayo na ni jukumu letu sote kushirikiana kwa kukosoa au kushauri namna bora ya kufikia malengo yetu

Pia kwa kawaida ili uwe objective/rational ni lazima mihemko iwe nyuma.Tutangulize reasoning.Siasa za Udini na ukabila zinapandikizwa kwa nguvu,ushabiki usio na dira nao ni tatizo katika kufanya maamuzi na hufifisha malengo makuu

We must discourage intra-party division, a proper example of shooting one's self in the foot....


Their inability to intellectually engage the truth about the Tanzanian situation is appalling.

Still more appalling is their recourse to ethnicity bigotry and character asssassination as the only way to gain political mileage.

This is the year 2012 remember
 
Pasco,

Kwa hiyo wewe mathalan una binti ana miaka 15 halafu mtu akakwambia kuwa akifikisha miaka 18 atakuja kumposa utajisikiaje? Kwa nini asisubiri mtoto afikishe hiyo miaka 18(umri wa mtu mzima) ndio aje kuposa?

Safari_ni_Safari:
Thank you for this Example about ZZK asiuelewa huu mfano lazima atakuwa na matatizo MFANO HUU unaeleza moja kwa moja kwanin Tunakerwa na huyu jamaa ZZK anatuletea mambo ya CCM kumpigana vikumbo vya urais mwaka mmoja baada ya uchaguzi hiyo sio destur ya CDM ndo maana huwa naona huyu jamaa katumwa 100% na CCM kuivuruga CDM...
 
Mpango huu ni miongoni mwa njama zinazoandaliwa kwa ajili ya Chama Tawala kuangamiza upinzani wa kisiasa nchini.

Mgombea binafsi wa kiti cha urais ama ubunge atakuwepo kwa mujibu wa Katiba Mpya ijayo. Zitto utashawishiwa kugombea nafasi mojawapo kati ya hizo mbili nje na Chama ulichopo sasa. Kisha utaahidiwa uwaziri wa fedha ama madini. Utategwa ujichagulie kati ya nafasi hizo. Lengo litakuwa ni kuhakikisha unajiengua CHADEMA ili kusababisha mgawanyiko katika idadi ya wapiga kura waliowaumini wa vyama vya upinzani, CHADEMA ikilengwa.

Nawe Zitto utashawishika kwenda huko, utagombea urais, utashindwa lkn utakuwa umefanikiwa kuleta mgawanyiko ktk suala zima la wapiga kura. Ila hutaachwa hivi hivi, utapewa ubunge wa kuteuliwa kama ilivyo kwa Mtu Makini Joseph Mbatia, kisha utaingizwa Serikalini kuchukua mojawapo ya hizo nafasi nilizokutajia hapo juu.

Sasa hilo litakuwa ndiyo ANGUKO lako la jumla katika siasa za Tanzania, nawe utafuata nyayo za Waridi Amani Kaborou.

Yawezekana hulijui hilo lkn laandaliwa na laja kwa ajili yako. Tafakari wewe ni kijana mwenye uwezo mkubwa wa kufikiti. FIKIRIA

Mimi tu kukuletea habari.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom