Upotevu wa Mafuta bandarini: Mtendaji Mkuu WMA, Meneja Vipimo wasimamishwa kupisha uchunguzi

Ila nikimsikiliza huyu mama ...(unless awe anasema uongo) kuna possibility ya kuwa innocent...
Na hii incidence nadhani iwa alert waheshimiwa wasipende sana kuvamia maofisi wakiwa na wana habari...wataja umbuka siku moja wakikutana na mtendaji hamnazo...
Prof ametajwa na kila mtu ametafsiri kutajwa kwake anavyotaka yeye...
Bila ma camera aibu hii isingetokea...

Jipu hili ni la muda mrefu! Lakini kwa vile tulikuwa na Raisi Mtalii-majipu yaliendelea kukua na yako mengi.



Ripoti ya Jumla ya Mashirika ya Umma 2013/2014
PAU-SWAHILI.pdf


Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

Ripoti ya Mashirika ya Umma 2013/2014



3.6 Mapendekezo ambayo hayajatekelezwa kwa mwaka 2012/2013



3.6.2

Mita za Kupima Mafuta Zilizotelekezwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania Mamlaka ya Bandari Tanzania ilinunua mita nane kwa ajili ya kudhibiti upimaji wa shehena za mafuta yanayoingia nchini. Mita hizo ziliwekwa tayari kwa matumizi kwenye bandari za Tanga na Dar es Salaam kwa ajili ya kusaidia kudhibiti mapato yanayopotea kutokana na kutokuwa na vifaa vizuri vya kupimia shehena za mafuta zinazoingia nchini.

Vifaa hivyo vilinunuliwa na kuwekwa kwenye bandari hizo baada ya serikali kuagiza ununuzi wake kwa ajili ya kupata vipimo sahihi na hatimaye kutoza viwango sahihi vya kodi. Hata hivyo, mita hizo zimetelekezwa kwa miaka kadhaa sasa. Sababu iliyotolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa vipimo ni kwamba vifaa hivyo havikidhi viwango vinavyotakiwa. Baada ya matatizo hayo kushindikana, Mamlaka ikaamua kuendelea kutumia njia zisizo za kielektroniki (“deep stick”)fimbo ya kutumbukiza kwenye matangi ya mafuta) kwenye kupima shehena za mafuta yanayoingia nchini.
 
Inaelekea hii haikuwa siri bali ilijulikana kabisa kuwa tokana na msuguano wa serikali na hawa wafanya biashara iliamuliwa kuwa mashine zisitumike...
Kosa la msingi ni kwa nini wananunua mita zisizofaa...na si kwa nini zimezimwa...
Au ni ku establish kama ni kweli zilikuwa hazifai au ni njama...
Tukumbuke power waliyokuwa nayo wafanya biashara za mafuta...
tukumbuke waliotolewa uhai wao kwa kuchokonoa mambo ya hawa matajiri...
Huyu mama tusimuhukumu kisiasa...unless pia awe na mimali isojulikana kapata wapi ...
Otherwise kwa utawala ulopita nani angeweza kufurukuta mbele ya matajiri????!!!!
 
Inaonekana una ufahamu mdogo sana kuhusu hii nchi.. Na hasa utaratibu wa kazi serikalini.
Kama hujui tatizo sio watendaji bali wanasiasa ndo wanaiharibu hii nchi..

ChaterMaster,na ndiyo sababu Warioba alilion hilo akaamua kulifanyia kazi.Wezi wa mali za umma waliona wakifanya alivyosema Warioba wataaibika.

Elimu yetu imeshuka sababu ya wanasiasa,ndiyo sababu sitaona kama wanasiasa wataweza kutusaidia kuvuka
 
Hapana mkuu naona unachambua mambo vizuri ila kwa kusema wasomi wetu ni wabovu unakosea sana.
Sijui unafanya kazi wap ila ukweli ni kuwa tz tuna mfumo mbovu sana wa kusimamia mambo, kinachosababisha yote haya ni pale tulipoacha azimio la Arusha na sasa tunaongozwa kimzimumzim hali inayofanya watu kupiga pesa mnoo..
Sasa labda nikwambie kwann watendaji sio wa kulaumiwa.. Kiutaratibu serikalini kazi huwa zinafanywa kwa maagizo top to bottom.. Ni vigumu sana kutekeleza jambo bottom Up
Hivyo ni wazi kabisa hawa watendaji hubaaki kuambiwa fanya hv na usifanye hivi na ukijidai kupingana na maagizo hayo jua utawekwa pembeni na kuambulia kushushwa cheo au kupelekwa kantalamba kabsa upotelee huko..
WANACHOKIFANYA HAWA WATENDAJI NI KUTII AMRI ZA WAKUBWA WAO ZIWE NI MBAYA AU NZURI HAWANA JINSI MAANA NDIO WANAPOPATIA MKATE WA KILA SIKU.. hata ingekuwa ni wewe Tetty ktk mfumo huu ambao kila mtu ni mpigaji na hakuna kuchukuliwa hatua kwa ufisafi... usipopiga unaambulia kufa njaa wakati wenzako wanachanua kirahisi..
Kwa ufupi hakuna uwajibishwaji katika mfumo wa serikalink kwa kipindi kirefu.
Sasa kama huo mfumo wa uwajibishwaji umeeanza basi asiangaliwe mtendaji wala mwanasiasa aliyeteuliwa wote washtakiwe na sio kuwaonea watendaji tu.

Umejibu vyema.Na ndiyo sababu hatuna JD kwenye taasisi zetu za umma tokea kwenye wizara mpaka kwenye vitaasisi vidogo.Kuwa na JD maana ni kumpa mtu uhuru wa kufanya maamuzi.Usipokuwa na JD si rahisi kufanya maamuzi.Ninakuelewa.Lakini wengi wa wanasiasa wetu leo ni wasomi je kuna cha maana walichotusaidia???Hivi Magufuli ataweza kurekebisha mtindio wa ubongo wa TAIFA kwa watu wale wale???
 
Itapita Mkuu huwa hawashindagi ila wanaiba na kutumia nguvu ya jeshi..

Kinachoniudhi ni kumfanya RAIS kama ni watanzania wanachama wa CCM tu.Na bahati mbaya zaidi na RAIS anaimba wimbo huo huo.Anajiona ni RAIS wa wanaCCM zaidi kuliko wa watanzania wote.

I wish tupate RAIS amabaye atarecognise WATANZANIA kwa wasifu wao bila kujali ITIKADI zao,DINI zao na MAKABILA yao.HAijalishi toka chama gani,lakini RAIS ambaye atajiondoa na kujiweka kuwe very neutral akawafanyia kazi watanzania bila kujali hasa ITIKADI zao.

Tumeona namna Kampeni zilivyoenda,Samia Suluhu hakuficha cha moyoni alisema ukweli kabisa WAPINZANI hawana nafasi kwenye serikali yao,na tumeona hilo likitendeka,wameuawa vijana wa upinzani ,serikali inaona kama ni kuku tu wamekufa.NAjiuliza kesho akiuawa kijana wa CCM tutaambiwaje???

Tumesikia kwenye sherehe za CCM akijinadi vyema kama RAIS wa CCM zaidi kuliko RAIS wa watanzania,lakini linapokuja swala la kuombewa anasema watanzania niombeeni,haiingi akilini watanzania wepi???WanaCCM tu???Tumeona mabango ya kibaguzi ya kipita mitaani hatuoni yakikemewa na wenye nafasi za juu maana siyo wao,na wale wapinzani,hatujui kesho akibaguliwa mwanaccm tutaelezwa nini.
 
Hii sijaelewa


Meseji ilikuwa hivi na taasisi zote zilizotajwa kwenye hiyo meseji walitumiana kuweka msisitizo.
wa kutekeleza agizo.


"ACTING MD TPA - MATUMIZI YA FLOW METER: Wizi wa mafuta umekidhiri huku matumizi ya flow meter hayapo hapo Bandarini. Ipo flow meter ya zamani nashauri ianze kutumika kuanzia kesho, Jumatano, 10 Feb 2016. TPA ndiye Mhusika Mkuu kwenye hili suala. TRA na Weights and Measures watoe ushirikiano mzuri. PBPA (Wizara ya Nishati na Madini) ifuatilie kwa makini. KASI INAHITAJIKA KUEPUKA WIZI WA MAFUTA.
S. Muhongo"

Asante.Kwahiyo Waziri huyu anajua mengi kuliko tunavyojua.Kwa nini hasemi ukweli???Au kwanini anaficha ukweli???
 
Huyo waziri ni wa sasa wa uchukuzi. Maswala yanayohusu bandari yanasimamiwa na waziri wa uchukuzi ambae ni Mbalawa. Unajua kwa kuwa wewe ni mjinga usifikiri kila mtu humu atakutilia maanani wewe....kwanza wanaume tunakushangaa mwanamke gani kutwa nzima upo JF? Una tatizo gani wewe!?

Wanaume wanaonishangaa ni wale tu wanaosubiria wanawake wawatunze kama ulivyo wewe hapo.Kama unataka wanawake siyo JF nenda maenao husika watakununua tu,lakini siyo mie,sina haja na wanaume wakununua kama wewe.

Na pili yake MJINGA ni yule tu badala ya kutoa hoja yuko busy kutukana na kudhalilisha wengine.BAba fanya kazi JF hawalipi.

Ninaongea mawazo yangu yanayojitegemea hayajashikwa na ACCOUNT ya watu wengi mliyofunguliwa na UVCCM.Kama wewe Mwanaume kweli toka nje ya hiyo ID Account tupamambe.Usijifiche kwenye ID za maelekezo ya nini muandike.

Matatizo yangu ni UZALENDO wangu period
 
Muhongo anahusikana kivipi na suala hili?? Kwa nini baadhi yetu tuko overly obsessed na binadamu huyu!!



Haupo mkuu, basi tu watasema lolote kumkandia Prof.

Unaweza kuona ahusiki lakini ndiye aliyetuma meseji.Pili issue ya MAFUTA yeye ndiyo muhusika mkuu.Hapo tu.Sina shida na Muhongo.Inawezekana pia anajua mambo mengi juu ya huo wizi ila amefungwa mikono na midomo kwenye issue ya kuwa na siri za serikali.

Siwezi kumlaumu pie.
 
Back
Top Bottom